Na Peter M
Mabula
Maisha ya
Ushindi Ministry.
|
BWANA YESU
asifiwe.
Nakukaribisha
tujifunze somo hili la muhimu kwako na kwako, ni maombi yangu kwamba nguvu ya
MUNGU iliyo katika neno lake hili ikuzalie matunda katika maisha yako.
Kila mtu
amebeba taarifa katika moyo wake.
Askari
akiambiwa amlenge adui vitani, atamlenga na kumpiga adui kwa sababu ana taarifa
sahihi kuhusu silaha yake na pia ana taarifa kuhusu kupiga risasi. Ni tofauti
na yule ambaye hajui chochote kuhusu silaha na risasi, hawezi kufanya lolote
maana hana taarifa sahihi kuhusu silaha
Wewe umebeba
taarifa gani moyoni mwako?
Anayeuza
mchele anauwezo wa kuupembua mchele kilo 1 na kuuweka juu ya gunia la kilo 200
ili kila mteja akija aseme ‘’mchele huu ni mzuri sana’’ kumbe mchele mzuri ni
kilo moja tu ya juu. Huyu mfanya biashara ana taarifa sahihi katika biasahara
yake.
Najua
unataarifa ya jambo fulani lakini huwezi kufanya kazi hiyo ili ikutajirishe.
Wangapi
wanajua kushona kushona cherehani lakini kwa miaka 3 wamekosa pesa ya kukunua
cherehani?
Ili uwe na
taarifa sahihi moyoni mwako lazima kwanza uwe umebadilishwa na MUNGU. Ezekieli
36:26-27 ( Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa
moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama.
Nami nitatia roho yangu ndani yenu, na kuwaendesha katika sheria zangu, nanyi
mtazishika hukumu zangu, na kuzitenda.)
MUNGU
ametuahidi kutupa moyo wa nyama yaani moyo wa upole, moyo wa kusikiliza ushauri
mzuri,na ni moyo wa kumsikiliza ROHO MTAKATIFU.
Ndani ya
moyo wa mtu kuna siri nyingi sana, moyo ni kama nyumba yaani wakati mwingine
ndani ya nyumba hufanyika mambo mengi. Walio nje ya nyumba hiyo hawawezi kujua
kama ndani ya nyumba hakuna amani, ndani ya nyumba kuna mapigano.
Mazingira
mazuri ya kazi yako uitakayo yako ndani ya moyo wako.
Nina uhakika una taarifa njema kuhusu unavyokusudia moyoni mwako mtu wa MUNGU, Lakini vikwazo vimekukwamisha na kuna baadhi ya watu huabudu vikwazo badala ya kuendelea kuifanyia kazi taarifa njema walionayo ya baraka zao.
Nina uhakika una taarifa njema kuhusu unavyokusudia moyoni mwako mtu wa MUNGU, Lakini vikwazo vimekukwamisha na kuna baadhi ya watu huabudu vikwazo badala ya kuendelea kuifanyia kazi taarifa njema walionayo ya baraka zao.
VIKWAZO VYA
KUTOKUFANIKIWA KWA TAARIFA YAKO NI.
1.
Hufanyi maombi.
2.
Unawaza kushindwa tu.
3.
Unawaza
hasara tu ambayo unaweza kuipata kama mambo yakienda vibaya.
4.
Kujilinganisha
na wenginewaliofanikiwa..
Kutoka
4:1-7( Musa akajibu akasema, Lakini, tazama, hawataniamini, wala hawataisikia sauti yangu; maana watasema, BWANA hakukutokea.
BWANA akamwambia, Ni nini hiyo uliyo nayo mkononi mwako? Akasema, Ni fimbo.
Akamwambia, Itupe chini; akaitupa chini, nayo ikawa nyoka; Musa akakimbia mbele yake.
BWANA akamwambia Musa, Nyosha
mkono wako, kamshike mkia; (akaunyosha mkono wake akamshika, naye
akageuka kuwa fimbo mkononi mwake;)
ili kwamba wapate kusadiki ya kwamba BWANA, MUNGU wa Ibrahimu, MUNGU wa Isaka, MUNGU wa Yakobo, amekutokea.
BWANA akamwambia tena, Sasa tia
mkono wako kifuani mwako. Akautia mkono wake kifuani mwake; naye
alipoutoa, kumbe! Mkono wake ulikuwa una ukoma, umekuwa mweupe kama
theluji.
Akasema, Tia mkono wako kifuani
mwako tena. Akautia mkono wake kifuani mwake tena, na alipoutoa kifuani
mwake, kumbe! Umerudia hali ya mwili wake.
).
Kwanini Musa
aliambiwa maneno hayo?
Ni kwa
sababu Musa hakuwa na taarifa sahihi juu ya MUNGU wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo.
-Musa
alikuwa na taarifa ya kuchunga kondoo tu.
-Musa hakuwa
na taarifa ya utumwa wa Waisraeli kwamba umefika mwisho.
-Musa hakuwa
na taarifa kwamba inawezekana kumshinda Farao.
-Musa
alikuwa na taarifa tu ya kwamba kama akienda Misri atakufa kwa sababu ya kumwua
Mmisri miaka ya nyuma.
-Musa hakuwa
na taarifa za kumalizika mika a430 za utumwa wa Waisraeli kule Misri.
Yoshua 1:8(
Kitabu hiki cha torati kisiondoke
kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate
kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana
ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.
)
Hapa Yoshua
anafundishwa utii wa neno la MUNGU.
Hata wewe umekutana na neno mara nyingi sana iwe ni kanisani,Radioni, Mtandaoni au hata kwenye simu kupitia SMS. Je ulibeba taarifa gani kutokana na mafundisho hayo ambayo itakuletea Baraka katika maisha yako?
Hata wewe umekutana na neno mara nyingi sana iwe ni kanisani,Radioni, Mtandaoni au hata kwenye simu kupitia SMS. Je ulibeba taarifa gani kutokana na mafundisho hayo ambayo itakuletea Baraka katika maisha yako?
-Yawezekana
umetaka kuwa mtu Fulani maishani mwako, lakini tambua kwamba direction ya
kuifikia hatima yako iko ndani ya neno la MUNGU.
Mwongozo
wako wa kukufikisha huko kwenye hatima nzuri ya maisha yako ni neno la KRISTO.
-Yawezekana
unataka kuwa rubani maishani mwako, neno la MUNGU linakuambia ‘’ Mshike sana
elimu, usimwache aende zake.’’ Kasomee urubani huku ukimwomba MUNGU akufikishe
kwenye taarifa yako hiyo ya kuwa rubani. Ni kweli taarifa ya kuwa rubani unayo
lakini ukipewa ndege leo uendeshe hutaweza kwa sababu hujasomea.
Taarifa
inatangulia kwanza kabla ya tukio.
Hebu
tujifunze kitu hapa Isaya 38:1-5 (Siku hizo Hezekia aliugua, akawa katika hatari ya kufa; na Isaya nabii,
mwana wa Amozi, akaenda kwa mfalme, akamwambia, BWANA asema hivi,
Tengeneza mambo ya nyumba yako; maana utakufa, wala hutapona.)
Mfalme
Hezekia alikuwa na taarifa ya kufa kwa sababu ya ugonjwa lakini Nabii Isaya
analeta taarifa mpya kwamba kama atarekebisha baadhi ya vitu na kumwomba MUNGU ataishi.
Wewe je una
taarifa gani katika moyo wako?
Kama una
taarifa njema ya kwenda uzima wa milele mpe BWANA YESU maisha yako.
Yoshua
akaambiwa alishike neno na aliishi neno ndipo atakapofanikiwa sana kihuduma, kimaisha na kikazi pia.
-Ukiona
nyumbani mwako una TV basi hiyo TV uliiona moyoni mwako kabla ya kuinunua, hiyo
ndio taarifa.
-Kama una
mafanikio Fulani maishani mwako, hakika uliyaona kabla hata ya kuyapata, hiyo
ndio taarifa. Taarifa hii inakuja kuwa kweli baada ya kuitendea kazi.Wengine
wanakaa nazo taarifa zao bila kuzitendea kazi, hiyo ni mbaya.
-Kama mama
anaenda kununua mwiko sokoni, na hata akiwa njiani ukimuuliza ‘’unaenda wapi’’ atakuambia ‘’naenda sokoni
kununua mwiko’’ Hiyo ndio taarifa na
mama huyo atanunua maana taarifa ilikuja kabla ya tukio na yeye kuifanyia kazi
taarifa hiyo.
AONAVYO MTU
NAFSINI MWAKE, NDIVYO ALIVYO-Mithali 23:7.
Je wewe
unaona nini moyoni mwako? Unachokiona katika BWANA ndio taarifa njema ya
mafanikio yako ya baadae.
Tambua hii
‘’PASIPO
MABADILIKO ,HAKUNA HATUA’’
‘’PASIPO
TAARIFA, HAKUNA TUKIO’’
Kwa leo naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku
nyingine.na kama
hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na
atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa
mafundisha kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana makusudi kabisa na
wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
MUNGU
akubariki sana .
Ni mimi
ndugu yako
Peter M
Mabula
Maisha ya
Ushindi Ministry.
0714252292
Comments