WANAWAKE WATAKA MAPADRE WARUHUSIWE KUOA

Papa Francis kiongozi wa kanisa katoliki

Kundi moja la wanawake walio na hisia za kimapenzi na mapadre wa kikatoliki wamemuandikia barua kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis ya kumtaka kubadilisha sheria za kanisa hilo zinazowazuia viongozi hao wa dini kuoa.

Wanawake hao 26 kutoka Italy na maeneo mengine wanasema kwamba wamekuwa wakishiriki ama wanataka kushiriki katika uhusiano wa kimapenzi na mapadre na kwamba wametoa ombi hilo kwa niaba ya wanawake wengine ambao wako katika hali kama hiyo.

Barua hiyo inazungumzia kuhusu uchungu wa kushindwa kuishi maisha yao kikamilifu mbali na kutaka kukutana na papa Francis.
Papa Francis amekuwa akiunga mkono utamaduni wa useja,lakini mwaka 2010 aliandika akisema kuwa huenda msimamo wake ukabadilika.

Papa francis amekuwa akimtembelea mjane wa aliyekuwa kasisi Jeronimo Podesta ambaye alijiuzulu katika utumishi wake na kuoa, zaidi ya miaka 40 iliopita.

Cardinals attend a mass in St. Peter's Basilica at the Vatican March 12, 2013. All cardinals, including those over 80 who will not vote in the conclave, celebrate Mass in St Peter's Basilica to pray for the election of the new pope. The Mass is called Pro Eligendo Romano Pontefice (For the Election of the Roman Pontiff) and is open to the public. REUTERS/Stefano Rellandini (VATICAN - Tags: RELIGION)
Makadinali wakiwa katika misa maalum
                                      Chanzo:BBC

Comments