BIBLIA MILIONI 5 KUSOMWA KOMBE LA DUNIA 2014 BRAZIL.


Dk. Rudi Zimmer wa chama cha Biblia Brazil akifafanua juu ya maono haya ya Chama Cha Biblia ambayo yamefanikiwa.

Chama cha Biblia cha Brazil kimesambaza Biblia mioni tano(5) katika jitihada zake za kuyafikia mamilioni ya watu walioingia nchini humo kutazama mashindano ya kombe la dunia.
Viongozi wa shirika hilo la kimataifa wamesema hawawezi kuyaacha mashindano hayo yapite hivi hivi bila wati kulijua neno la MUNGU.
Makisio ya shirikisho la mpira wa mguu duniani(FIFA) ni kwamba wageni zaidi ya milioni 1.5 wangeingia Brazil kwa ajili ya kushuhudia fainali hizo.
Pamoja nao, chama cha Biblia Brazil kilikisia kwamba wabrazil milioni3 wangeshiriki viwanjani kutazama mashindano hayo na hivyo wakatenga Biblia za kutosha  kwa ajili yao.
Dk. Rudi Zimmer wa chama cha Biblia Brazil alisema lengo lao ni kuyatumia mashindano haya kufanya uinjilisti ili kuwashirikisha watu ujumbe wa neno la MUNGU badala tu ya kusherekea masuala ya soka.
Maisha ya ushindi blog tunapongeza sana maono yaka ya chama cha Biblia cha Brazil.
Mbali na usambazaji wa Biblia hizo, nakala 20,000 za vitabu vya injili ya Yohana zitasambaza kwa lugha ya kireno pamoja na lugha zingine 7 za mataifa mbalimbali. Pia chama hicho kimechapisha matoleo ya Agano jipya na agano la kale yanayosambazwa kwa watazamaji.
Katika kufanikisha uinjilisti huo chama cha Biblia Brazil, makanisa 1,600 na mamia ya huduma za kiinjili nchini Brazil wameungana kugawa maandiko haya. Harakati hiyo ya kugawa maandiko matakatifu imepewa jina la FAIR PLAY BRAZIL.
Maandiko hayo ya neno la MUNGU hugawiwa wakati watazamaji wakijiandaa kuingia katika viwanja vya miji 12 vinavyotumika kwa ajili ya mashindano hayo.
Kombe la dunia 2014 limeanza tarehe 12 june  2014, katika uwanja wa sao Paulo, ambapo timu za taifa 32  duniani zinashiriki.
MUNGU awabariki sana chama cha Biblia cha Brazil.

Baadhi ya maandiko ya Biblia ambayo yana kava ambazo zinaonyesha miji 12 ambayo inaandaa kombe la dunia 2014.



Comments