DAVID ROBERT NDANI YA BERLIN


Kazi imeanza kwa mtumishi wa Mungu ambaye amepata neema ya kudondoka ndani ya Berlin. Hii ni changamoto kwetu sisi kuona mwimbaji kama huyu anapata channel za ulaya. Ninaamini ukiwa chini ya miguu ya Baba yetu wa mbinguni siku moja atakuweka mahali ambapo hukutegemea kufika.

Lakini jitihada zako pia zinahitajika, juhudi zako za kutimiza ndoto zako zikiwa kubwa ndipo milango ya mafanikio pia inafunguka. Tuzidi kuwa mwaaminifu mbele za Mungu na tusichanganye ya duniani na ya mbinguni kama shortcut ya mafanikio.

Muulize Mungu wako nini amekiweka ndani yako kwa kazi yake ili uanze kukitumia sasa. David aliona uimbaji kwake ni karama aliyopewa na Mungu na ndio maana akakaza buti na sasa anakaa na ngozi nyeupe akichangia maoni yake. Jikubali na sema ninaweza.


 David Robert
 David Robert akiwa ametulia katika jopo la wazungu

Comments