JE NI SAWA KWA MWANAMKE KUVAA SURUALI?

Joyce Meyer Mhubiri huko marekani ambaye kanisa lake lina maelfu ya waumini, MUNGU anamtumia sana mama huyu lakini vazi lake mara nyingi ni suruali..
Nabii Flora ni mtumishi wa MUNGU anayefanya vizuri sana katika huduma, ni mmoja wa watumishi wa MUNGU ambao huvaa suruali.
BWANA YESU asifiwe! 
 
Nimekutana na swali jana ya kuwa "Je ni halali kwa mwanamke kuvaa suruali?" Nikapewa na andiko katika Kumbukumbu laTorati 22:5 
Haya Wapendwa tunasemaje juu ya hili!! 
Maoni yangu ni haya yafuatayo
Kwani Imeandikwa wapi kwamba Suruali ni Vazi la Kiume? 
Shalom ndugu zangu mimi nimesoma  swali hilo na nimebarikiwa sana na kufurahi sana na mimi pia naomba nichangie kidogo juu ya suala hili  nionavyo mimi kuvaa suruali kwa mwanamke sio dhambi  ila itakua dhambi tu kama itasababisha wengine kutenda dhambi katika mathayo 18:7 Biblia inasema ''Ole kwa ulimwengu kwa sababu ya mambo ya kukosesha, maana hayana budi kuja mambo ya kukosesha;LAKINI OLE WAKE MTU YULE ALILETAYE JAMBO LA KUKOSESHA.'' 
  kwa hiyo ndugu zangu Suruali  itakuwa dhambi kama itawashawishi wengine kuingia dhambini maana tukisema tu kuvaa nguo fulani  ni dhambi basi mvaaji hatakiwi kuvaa hata kama yuko chumbani na mmewe maana kuvaa nguo hiyo  ni dhambi. na dhambi zingine ni dhambi hata kwa kusababisha mfano unakuta kijana anaenda kutongozea kijana mwingine kwa binti na ukimuuliza atakwambia kutongoza sio dhambi ila dhambi ni kuzini lakini ukweli hiyo ni dhambi kubwa wote mnajua na hili pia la kuwavalia wengine nusu uchi ni dhambi. na kwa habari ya suruali  kuwa ndio vazi la kiume napata tafakari hii. Biblia iliposema mwanamke asivae mavazi yampasayo mwanaume haikutaja suruali. Na kwa upande wangu neno Suruali kwenye Biblia ninakuja  katika Danieli 3:21 ikizungumzia habari ya wale vijana watatu waliotupwa katika tanuri la moto huku wakiwa wamevaa suruali zao na joho zao. hawa walikua wanaume wote hata hivyo hapa haionyeshi kwamba hayo ndio mavazi ya wanaume.muhimu na cha kuzingatia ni kwamba biblia imeagiza wanawake wavae nguo za kujisitri na nguo hizi haijalishi ni sketi au suruali maana wapo wadada wengine huvaa sketi za kuwachora maungo yao utasema hata heri ya anayevaa suruali. pia hakuna haja ya kuiga kila mtindo maana kuna baadhi ya mitindo chanzo chake ni kuzimu  kumbuka pia tunaitwa wakristo yaani wanaomfuata KRISTO MATENDO 11:26,pia tukumbuke kuwa kama tutaupenda sana ulimwengu na mambo yake basi kumpenda MUNGU hakumo ndani yetu hivyo hakuna haja ya kuwaweka majaribuni wenzako na ukiangalia wengi wa wanaovaa nguo ambazo zinalalamikiwa ni wale ambao hawajaolewa na akiolewa anaacha hapo ndio unajua kwamba alikua anavaa zamani kwa sababu fulani ambayo ni dhambi.pia tukumbuke kuwa biblia inasema kwamba YATENDENI MAMBO MAMBO YOTE PASIPO MANUNG'UNIKO YOYOTE WALA MASHINDANO NA LISHIKENI LILILO JEMA ILI MPATE KUWA WANA WA MUNGU. hivyo kama nguo zako zinalalamikiwa kwa sababu unawatega watu ni vizuri kujirekebisha na wengine huvaa hivyo ili vijana wampigie miluzi sasa hiyo roho inayotenda kazi ndani ya dada huyo sio ya MUNGU bali ya shetani. wake za watu wengi wanajiheshimu isipokua tu hao wanaojiita wasanii ambao hufanya sio mapenzi ya MUNGU bali mapenzi ya wanadamu . kama watoto wa MUNGU tuliozaliwa sio kwa mwili bali kwa ROHO WA MUNGU basi na tuenende kama watakatifu wa MUNGU pasipo lawama. Natamani niendelee lakini mwisho kabisa Biblia katika waefeso 5:10 inasema ''MKIHAKIKI NI NINI IMPENDEZAYO BWANA'' .
MUNGU awabariki sana na kila mtu awe ni mwanamke au mwanaume kwa kila tendo lolote afanyalo ahaakiki kama anampendeza MUNGU maana tukitenda kwa kumpendeza MUNGU hatutalalamikiwa .
MUNGU awabariki sana 
Na nahitaji michango ya watumishi wengine hapa au kwenye page yetu ya facebook itwayo Maisha ya Ushindi FUNGUA HAPA KUTOA MAONI YAKO.
 Kwa leo naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
                     MUNGU akubariki sana .
                      Ni mimi ndugu yako
                       Peter M Mabula
                 Maisha ya Ushindi Ministry.
                           0714252292

                 MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.

 MUNGU Akubariki.

Comments