KIDOGO NIKANYAGE NYOKA ALIYEKUWA AMETUMWA.

      






  

Habari ndugu mchungaji,kuna document ambayo nilikutumia kwenye email yako, uliiona?  Ile document imeniongezea sana imani kwani mengi niliyopitia nilipata kujulishwa kupitia ujumbe wake wakati nasoma form 5 nikastaajabu sana yale yaliyomo hata leo nakiri kuwa MUNGU alinionesha hatari zote awali kabla hazijatokea .Najua ahadi yake kwetu haiwezi kuyumbishwa na dhoruba yoyote tunayoweza kuieleza kibinadamu. Naamini salama ambayo MUNGU hutupatia katika hatari ambazo hatuwezesha  kushinda.
Kwa hali ya kibinadamu Dunia imejaa dhoruba zenye kukatisha tamaa nazo huletwa na ndugu,rafiki,jirani hata wazazi lakini ushindi upo katika MUNGU wetu, tena  yeye ana nia njema,tudumu kumtanguliza yeye katika mipango yetu.
Hakika MUNGU anajibu magumu tunayopitia.  Nakumbuka mwaka 2008 wakati nimemaliza form 6 nasubiri matokeo MUNGU  alinionesha jambo kuu,niliamka mapema kama saa kumi na moja kasoro kujiandaa kwenda kuchukua cheti changu cha form 4 ndipo wakati nikipasha maji moto ili nioge maji yalivyochemka nikawa natoka jikoni kwenda kuchukua ndoo ya kuweka maji,lakini wakati natoka nikazima taa kabla ya kutoa mguu pale mlangoni wazo likanijia kuwa ‘’rudi uwashe taa usiache jiko likiwa giza’’ ndani ya sekunde ile nikatii, wakati nageuka kupeleka mkono kwenye swich nikaona mwale wa mwanga kama kijinga cha moto nikasema huo ni mwangwi tu kwani nilikuwa kwenye mwanga,hivyo sikutishika kitu ila wakati nageuka kutoka jikoni pale mlangoni nlipotaka kukanyaga ndipo nikamwona nyoka anagalauka huku anametameta na hii hali ndiyo iliyonifanya nimwone kwani pale mlangoni hapakuwa na taa ila ile nuru ndio iliyosababisha nikamwona  yule nyoka,sikutishika bali nikajiuliza swali moja kuwa nini kinatokea nikahoji nafsi yangu kipi kiliniongoza nisikanyage nje nikatii ile sauti iliyonijia,kwanini namwona huyu nyoka katika hali hii lakini awali sikumwona na wakati nataka kukanyaga pale wazo linanijia ndani ya sekunde na kulitii bila kuhoji ndipo nasema hakika MUNGU amekuwa nami katika hila zote za ibilisi dhidi yangu na familia pia Ndipo siku moja wakati nilipowiwa kumsimulia dada mmoja tuliyekutana chuoni akaongozwa kuongea haya,"Dickson MUNGU anakupenda sana ndio maana humtuma malaika wake kukuokoa katika hatari  zote,akasema hata kutii ile sauti moyoni mwako  akasema hata ile nuru iliyopatikana kwa kuwasha taa ilibadilishwa kuwa nuru ya rohoni ndio maana uliweza kumwona yule nyoka katika hali tofauti kwani macho ya rohoni yamepewa nuru kwa kutii sauti ile. Nilitumia maji yaliyobarikiwa kwa maombi  yule nyoka akatoweka bila kuacha masalia yoyote BWANA amenionesha makuu ndugu na ahadi zake ni bayana kwetu kwani hutuongoza katika hatari zote huwa kama kuna hatari fulan inakuja nachelewa kupata usingizi na mara zote nakuwa busy kupitia vifungu anuai katika Biblia Nakumbuka nilikuwa ninasoma bible ndipo ukanipitia usingizi muda wa sa 8 usiku ilipokaribia sa 9 nikajiwa na maono ambapo nikaamshwa na kuoneshwa jambo naoneshwa kibwengo mithili ya mzee wangu anaingia chumbani nilipolala lakini mkono mmoja upo kwa nyuma,nikawa natizama tu kuwa kitafanya nini? kikawa kinasogelea zaidi kitanda ambacho nililala huku mkono ukiwa nyuma,nikawa siogopi bali kuangalia kitu gani kingeendeleaindipo kikaanza kuurudisha taratibu ule mkono kumbe kilikuwa kimeficha kisu,lakini sikupata hofu kwani nilikuwa naoneshwa hatua moja hadi ingine, kilipojaribu kunichoma kisu kifuani nilipaza sauti kali ambapo wazazi wangu walipata hofu kuu wakashindwa kufika pale chumbani nikawasihi wasihofu waje niwasimulie ila vitu vilivyokimbia huko nje kwa mshindo mkuu baada ya ile sauti Ndipo walifika wakiwa na hofu kuu nikawasimulia basi nakaendelea kulala hadi saa kumi na 1 ndipo ikanijia ndoto hii, nimetoka shamba na mbwa wetu(alikuja na kufanya makaz), kabla ya kufika home akatokea mbwa mwingine ghafla na kumng'ata shingoni yule mbwa nliyekuwa nae,wakati naduwaa kwa ile hali kwani mbwa yule alitokwa damu nyingi hata kulegea wakati nasubiri mbwa afe nione kuwa ataning'ata mimi au vipi nikashangaa kuona na yule mbwa aliyemng'ata mbwa wangu amefia pale pale,nikaongozwa katika tafsiri hii huyu mbwa aliyekuwa nami ni ndugu wa karibu lakn si mwema kwangu na familia yetu,na huyu aliyevamia na kumng'ata ni watu wengne wanaonifahamu vema na familia yetu lakini ubaya wao ni shirika moja na huyu aliyekuwa karibu kama ndugu. Ndo maana wakati nawaza kuwa atanidhuru akafia pale na kuniacha
MUNGU aliniokoa maana nyoka Yule alikuwa anatisha sana na hakika sijui ingekuwaje lakini MUNGU aliniokoa. Pia mbwa Yule alikuwa anatisha lakini MUNGU aliniponya hata kibwengo alikimbia.
MUNGU akubariki sana.
Dickson Haji.
Morogoro.

Comments