Mpendwa huyu katushirikisha ushuhuda toka inbox yetu ya facebook.
MAOMBI
YA KILA SIKU YAMELETA MABADILIKO MAKUBWA NYUMBANI KWANGU
Ndugu,
Nakusalimuni katika
jina la Yesu.
Nina ushuhuda ambao
ningependa kuwashirikisha wapendwa.
Katika familia yetu
tumekuwa tukiishi kama wakristo wengine ambavyo wamekuwa wakiishi. Kuna utofauti
sana kwa kweli wa maisha ya Ukristo ya kumaanisha kumuishia Mungu na ule
Ukristo wa mazoea. Tulizoea kwenda ibadani kama kawaida na kweli tumeokoka
kwa
sababu tumemwamini na kumkiri Yesu kama Bwana na Mwokozi wa maisha yetu. Lakini
kuna jambo moja ambalo mume wangu alikuja kulifanya nyumbani limeleta
mabadiliko makubwa sana katika familia yangu. Nalo ni MAOMBI YA KUMAANISHA YA
KILA SIKU.

Mume
wangu siku moja alikuja toka safari na kuleta mfumo mpya wa maombi na kujifunza
neno la Mungu nyumbani. Hatukujua nini kilimtokea huko safarini mpaka akaja na
mfumo huo. Lakini mfumo huo wa kuwa na maombi ya kila siku asbh na usiku na
kujifunza neno kila siku hasa usiku na kuomba kumeleta mabadiliko makubwa sana
katika familia yangu. Tumemuona Mungu kwanza akileta Amani na furaha kubwa sana
katika familia yetu. Sio kwamba majaribu na misukosuko mingine ya maisha
haitupitia, la hasha lakini inapotupitia neema ya Mungu imekuwa ikitufunika kwa
kiwango kisicho cha kawaida. Maana maandiko yasema “Mungu ni mwaminifu; ambaye
hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na
mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili”. Kwa hiyo amekuwa akitustahimilisha
tunapopita katika majaribu pia.
Lakini
pia kwa maombi haya ya kila siku tumekuwa tukimwambia Bwana mahitaji yetu ya
kila siku na Bwana amekuwa akifanya. Kweli tunamshukuru sana Mungu kwa
kutusaidia katika program yetu ya maombi na kujifunza neno kila siku. Imeleta matokea
chanya katika nyumba yetu.
Mungu awabariki
watumishi na tuendelee kuombeana.
Na pia napenda
nimshukuru Mungu kwa kazi mnayoifanya ya kuineza injili hasa kwa kupitia
mitandaoni.
Tungependa pia
kuwaulizeni je tukiwakaribisha kwa ajili ya huduma kama semina na mikutano ya
Injili mwaweza kuwa tayari kuja kuhudumu wapendwa? 
Comments