Na Mchungaji kiongozi Josephat Gwajima. Ufufuo na Uzima,Tanganyika parkers Kawe |
Danieli3: 1 Nebukadreza, mfalme, alifanya sanamu ya dhahabu, ambayo urefu wake
ulikuwa ni dhiraa sitini, na upana wake dhiraa sita; akaisimamisha katika
uwanda wa Dura, katika wilaya ya Babeli.
2 Ndipo Nebukadreza akatuma watu kuwakusanya maamiri, na manaibu, na maliwali, na makadhi, na watunza hazina, na mawaziri, na mawakili, na wakuu wa wilaya zote, ili wahudhurie wakati wa kuizindua ile sanamu, mfalme Nebukadneza aliyoisimamisha.
3 Ndipo maamiri, na manaibu, na maliwali, na makadhi, na watunza hazina, na mawaziri, na mawakili, na wakuu wa wilaya zote, wakakusanyika ili kuizindua ile sanamu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha; wakasimama mbele ya ile sanamu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha.
4 Ndipo mpiga mbiu akapiga kelele akisema, Enyi watu wa kabila zote, na taifa, na lugha, mmeamriwa hivi,
5 wakati mtakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, lazima kuanguka na kuiabudu sanamu ya dhahabu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha.
6 Na kila mtu asiyeanguka na kuabudu atatupwa saa iyo hiyo katika tanuru ya moto uwakao.
7 Basi wakati huo, watu wa kabila zote walipoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, watu wote na mataifa na lugha wakaanguka, wakaiabudu ile sanamu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha.
8 Basi baadhi ya Wakaldayo wakakaribia, wakaleta mashitaka juu ya Wayahudi.
9 Wakajibu, wakamwambia mfalme Nebukadreza, Ee mfalme, uishi milele.
10 Wewe, Ee mfalme, ulitoa amri ya kwamba kila mtu atakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, ni lazima aanguke na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu;
11 na kila mtu asiyeanguka na kuabudu atatupwa katika tanuru ya moto uwakao.
12 Wako Wayahudi kadha wa kadha uliowaweka juu ya mambo ya wilaya ya Babeli, yaani, Shadraka, na Meshaki, na Abednego; watu hawa, Ee mfalme, hawakukujali wewe; hawaitumikii miungu yako, wala kuiabudu ile sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.
13 Basi Nebukadreza akatoa amri kwa hasira na ghadhabu, waletwe hao Shadraka, na Meshaki, na Abednego. Basi wakawaleta watu hao mbele ya mfalme.
14 Nebukadreza akajibu, akawaambia, Enyi Shadraka, na Meshaki, na Abednego, je! Ni kwa makusudi hata hammtumikii mungu wangu wala kuisujudia sanamu ya dhahabu niliyoisimamisha?
15 Basi sasa, kama mkiwa tayari wakati mtakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, kuanguka na kuisujudia sanamu niliyoisimamisha, ni vema; bali msipoisujudia, mtatupwa saa iyo hiyo katika tanuru iwakayo moto; naye ni nani Mungu yule atakayewaokoa ninyi na mikono yangu?
16 Ndipo Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakajibu, wakamwambia mfalme, Ee Nebukadreza, hamna haja kukujibu katika neno hili.
17 Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na mkono wako, Ee mfalme.
2 Ndipo Nebukadreza akatuma watu kuwakusanya maamiri, na manaibu, na maliwali, na makadhi, na watunza hazina, na mawaziri, na mawakili, na wakuu wa wilaya zote, ili wahudhurie wakati wa kuizindua ile sanamu, mfalme Nebukadneza aliyoisimamisha.
3 Ndipo maamiri, na manaibu, na maliwali, na makadhi, na watunza hazina, na mawaziri, na mawakili, na wakuu wa wilaya zote, wakakusanyika ili kuizindua ile sanamu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha; wakasimama mbele ya ile sanamu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha.
4 Ndipo mpiga mbiu akapiga kelele akisema, Enyi watu wa kabila zote, na taifa, na lugha, mmeamriwa hivi,
5 wakati mtakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, lazima kuanguka na kuiabudu sanamu ya dhahabu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha.
6 Na kila mtu asiyeanguka na kuabudu atatupwa saa iyo hiyo katika tanuru ya moto uwakao.
7 Basi wakati huo, watu wa kabila zote walipoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, watu wote na mataifa na lugha wakaanguka, wakaiabudu ile sanamu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha.
8 Basi baadhi ya Wakaldayo wakakaribia, wakaleta mashitaka juu ya Wayahudi.
9 Wakajibu, wakamwambia mfalme Nebukadreza, Ee mfalme, uishi milele.
10 Wewe, Ee mfalme, ulitoa amri ya kwamba kila mtu atakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, ni lazima aanguke na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu;
11 na kila mtu asiyeanguka na kuabudu atatupwa katika tanuru ya moto uwakao.
12 Wako Wayahudi kadha wa kadha uliowaweka juu ya mambo ya wilaya ya Babeli, yaani, Shadraka, na Meshaki, na Abednego; watu hawa, Ee mfalme, hawakukujali wewe; hawaitumikii miungu yako, wala kuiabudu ile sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.
13 Basi Nebukadreza akatoa amri kwa hasira na ghadhabu, waletwe hao Shadraka, na Meshaki, na Abednego. Basi wakawaleta watu hao mbele ya mfalme.
14 Nebukadreza akajibu, akawaambia, Enyi Shadraka, na Meshaki, na Abednego, je! Ni kwa makusudi hata hammtumikii mungu wangu wala kuisujudia sanamu ya dhahabu niliyoisimamisha?
15 Basi sasa, kama mkiwa tayari wakati mtakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, kuanguka na kuisujudia sanamu niliyoisimamisha, ni vema; bali msipoisujudia, mtatupwa saa iyo hiyo katika tanuru iwakayo moto; naye ni nani Mungu yule atakayewaokoa ninyi na mikono yangu?
16 Ndipo Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakajibu, wakamwambia mfalme, Ee Nebukadreza, hamna haja kukujibu katika neno hili.
17 Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na mkono wako, Ee mfalme.
(Danieli6:1-28)
1 Ilimpendeza
Dario kuweka juu ya ufalme maliwali mia na ishirini, wawe juu ya ufalme wote;
2 na juu yao akaweka wakubwa watatu, na Danielii alikuwa mmoja wao; ili maliwali hawa watoe hesabu kwao, mfalme asipate hasara.
3 Basi Danielii huyo alipata sifa kuliko wakubwa na maliwali, kwa kuwa roho bora ilikuwa ndani yake; naye mfalme akaazimu kumweka juu ya ufalme wote.
4 Basi mawaziri na maamiri wakatafuta sana kupata sababu za kumshitaki Danielii kwa habari za mambo ya ufalme; lakini hawakuweza kuona sababu wala kosa; kwa maana alikuwa mwaminifu, wala halikuonekana kosa wala hatia ndani yake.
5 Ndipo wale watu wakasema, Hatutapata sababu ya kumshitaki Danielii huyo, tusipoipata katika mambo ya sheria ya Mungu wake.
6 Basi wale mawaziri na maamiri wakakusanyika pamoja mbele ya mfalme, wakamwambia hivi, Mfalme Dario, uishi milele.
7 Mawaziri wote wa ufalme, na manaibu, na maamiri, na madiwani, na maliwali wamefanya shauri pamoja ili kuweka amri ya kifalme; na kupiga marufuku, ya kwamba mtu ye yote atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme atatupwa katika tundu la simba.
8 Sasa, Ee mfalme, piga marufuku, ukatie sahihi maandiko haya, yasibadilike, kama ilivyo sheria ya Wamedi na Waajemi, isiyoweza kubadilika.
9 Basi mfalme Dario akayatia sahihi maandiko yale, na ile marufuku.
10 Hata Danielii, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu;) akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo.
11 Basi watu hao wakakusanyika pamoja, wakamwona Danielii akiomba dua, na kusihi mbele za Mungu wake.
12 Ndipo wakakaribia, wakasema mbele ya mfalme katika habari ya ile marufuku ya mfalme; Je! Hukuitia sahihi ile marufuku, ya kwamba kila mtu atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme, atatupwa katika tundu la simba? Mfalme akajibu, akasema, Neno hili ni kweli, kama ilivyo sheria ya Wamedi na Waajemi isiyoweza kubadilika.
13 Basi wakajibu, wakasema mbele ya mfalme, Yule Danielii, aliye mmoja wa wana wa wale waliohamishwa wa Yuda, hakujali wewe, Ee mfalme, wala ile marufuku uliyoitia sahihi, bali aomba dua mara tatu kila siku.
14 Basi mfalme aliposikia maneno haya alikasirika sana, akakaza moyo wake ili kumponya Danielii; akajitaabisha kumwokoa hata jua likachwa.
15 Ndipo watu wale wakakusanyika pamoja mbele ya mfalme, wakamwambia mfalme, Ee mfalme, ujue ya kuwa ni sheria ya Wamedi na Waajemi, lisibadilike neno lo lote lililo marufuku, wala amri yo yote iliyowekwa na mfalme.
16 Basi mfalme akatoa amri, nao wakamleta Danielii, wakamtupa katika tundu la simba. Mfalme akanena, akamwambia Danielii, Mungu wako unayemtumikia daima, yeye atakuponya.
17 Likaletwa jiwe, likawekwa mdomoni mwa lile tundu; naye mfalme akalitia muhuri kwa muhuri yake mwenyewe, na kwa muhuri ya wakuu wake, lisibadilike neno lo lote katika habari za Danielii.
18 Kisha mfalme akaenda nyumbani kwake, akakesha usiku kucha, akafunga; na vinanda havikuletwa mbele yake; na usingizi wake ukampaa.
19 Asubuhi mfalme akaondoka mapema, akaenda kwa haraka mpaka penye lile tundu la simba.
20 Naye alipolikaribia lile tundu, akamlilia Danielii kwa sauti ya huzuni; mfalme akanena; akamwambia Danielii, Ee Danielii, mtumishi wa Mungu aliye hai, je! Mungu wako, unayemtumikia daima, aweza kukuponya na simba hawa?
21 Ndipo Danielii akamwambia mfalme, Ee mfalme, uishi milele.
2 na juu yao akaweka wakubwa watatu, na Danielii alikuwa mmoja wao; ili maliwali hawa watoe hesabu kwao, mfalme asipate hasara.
3 Basi Danielii huyo alipata sifa kuliko wakubwa na maliwali, kwa kuwa roho bora ilikuwa ndani yake; naye mfalme akaazimu kumweka juu ya ufalme wote.
4 Basi mawaziri na maamiri wakatafuta sana kupata sababu za kumshitaki Danielii kwa habari za mambo ya ufalme; lakini hawakuweza kuona sababu wala kosa; kwa maana alikuwa mwaminifu, wala halikuonekana kosa wala hatia ndani yake.
5 Ndipo wale watu wakasema, Hatutapata sababu ya kumshitaki Danielii huyo, tusipoipata katika mambo ya sheria ya Mungu wake.
6 Basi wale mawaziri na maamiri wakakusanyika pamoja mbele ya mfalme, wakamwambia hivi, Mfalme Dario, uishi milele.
7 Mawaziri wote wa ufalme, na manaibu, na maamiri, na madiwani, na maliwali wamefanya shauri pamoja ili kuweka amri ya kifalme; na kupiga marufuku, ya kwamba mtu ye yote atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme atatupwa katika tundu la simba.
8 Sasa, Ee mfalme, piga marufuku, ukatie sahihi maandiko haya, yasibadilike, kama ilivyo sheria ya Wamedi na Waajemi, isiyoweza kubadilika.
9 Basi mfalme Dario akayatia sahihi maandiko yale, na ile marufuku.
10 Hata Danielii, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu;) akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo.
11 Basi watu hao wakakusanyika pamoja, wakamwona Danielii akiomba dua, na kusihi mbele za Mungu wake.
12 Ndipo wakakaribia, wakasema mbele ya mfalme katika habari ya ile marufuku ya mfalme; Je! Hukuitia sahihi ile marufuku, ya kwamba kila mtu atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme, atatupwa katika tundu la simba? Mfalme akajibu, akasema, Neno hili ni kweli, kama ilivyo sheria ya Wamedi na Waajemi isiyoweza kubadilika.
13 Basi wakajibu, wakasema mbele ya mfalme, Yule Danielii, aliye mmoja wa wana wa wale waliohamishwa wa Yuda, hakujali wewe, Ee mfalme, wala ile marufuku uliyoitia sahihi, bali aomba dua mara tatu kila siku.
14 Basi mfalme aliposikia maneno haya alikasirika sana, akakaza moyo wake ili kumponya Danielii; akajitaabisha kumwokoa hata jua likachwa.
15 Ndipo watu wale wakakusanyika pamoja mbele ya mfalme, wakamwambia mfalme, Ee mfalme, ujue ya kuwa ni sheria ya Wamedi na Waajemi, lisibadilike neno lo lote lililo marufuku, wala amri yo yote iliyowekwa na mfalme.
16 Basi mfalme akatoa amri, nao wakamleta Danielii, wakamtupa katika tundu la simba. Mfalme akanena, akamwambia Danielii, Mungu wako unayemtumikia daima, yeye atakuponya.
17 Likaletwa jiwe, likawekwa mdomoni mwa lile tundu; naye mfalme akalitia muhuri kwa muhuri yake mwenyewe, na kwa muhuri ya wakuu wake, lisibadilike neno lo lote katika habari za Danielii.
18 Kisha mfalme akaenda nyumbani kwake, akakesha usiku kucha, akafunga; na vinanda havikuletwa mbele yake; na usingizi wake ukampaa.
19 Asubuhi mfalme akaondoka mapema, akaenda kwa haraka mpaka penye lile tundu la simba.
20 Naye alipolikaribia lile tundu, akamlilia Danielii kwa sauti ya huzuni; mfalme akanena; akamwambia Danielii, Ee Danielii, mtumishi wa Mungu aliye hai, je! Mungu wako, unayemtumikia daima, aweza kukuponya na simba hawa?
21 Ndipo Danielii akamwambia mfalme, Ee mfalme, uishi milele.
Hao walikuwa ni wafalme wanchi ingekuwa leo
ni Raisi nchi na hawa wanatoka katika ufamle ule ule na kwenye falme hizi hizi Nebukadreza
na dairo ikatokea siku moja jambo likatokea la ajabu na mfalme Nebukadreza
akatoa tamko la ajabu iletwe sanamu yake ya dhahabu na kutakuwa na dhifa ya taifa na mawaziri,
madiwani, wakuu wa mkoa na kutakuwa na mziki wa kinubi,santuri, na zeze na
utakapo sikika watu wote wanatakiwa waiabudu ile sanamu na atakaye kaidi atatupwa
katika moto na hii ilikuwa inawalenga watu fulani na mtu huwa anafanya hayo
pale anapokuwa katika utawala wake ndio maana anatumia uzoefu ule kuwaondoa na
hawa pasipokujua kuwa wao sio kama wale na uzoefu wao utakwama, sasa kulikuwa
kuna watu watatu Shadraka, Meshaki, na
Abednego ambao walikuwa hawayafuati masharti yao.
Inawezekana tatizo ulilo nalo
limetengenezwa ili wewe uporomoke useme hii ni kazi ya Mungu useme Bwana alitoa
na Bwana ametwaa, unatakiwa ukatae kwa
jina la Yesu. Na yapo mambo mengi yanatengenezwa juu yako na hao wanao
yatengeneze wanadhani hapa ‘hatatoka tumemkamata’ lakini hawajui yakuwa “mimi
sio kama wale” na namna ya kushinda vita ni kupita katikati yao na jaribu
likija hutakiwi ulikwepe unatakiwa usimame mbele yake halafu unasema napita
katikati yao.
Wakakusanyika watu wakadondoka chini halafu
kina shadraka, meshaki, na Abednego wakasimama wakaonekana wamesimama na baada ya muda mfalme
akapewa taarifa kwamba kuna viyahudi havikusujudu na mfalme akaamuru waletwe
kwake na akawaambia ni kwamakusudi kweli ni nadhani bahati mbaya lakini sasa
naomba irudiwe tena zeze na vinubi ili msujudu lakini wakakataa na mfalme
akawaambia nawatupa kwenye moto lakini wakamjibu tuko tayari kuingia kwenye
moto na Mungu wetu atatuokoa na Biblia inasema mfalme akamuru moto uwashwe
marasaba zaidi kuliko ilivyokuwa desturi yake, inawezekana kuna watu wanakuwashiwa
moto kwenye maisha yao ili wakuteketeze lakini wewe sio kama wale. Basi mfalme
akaamuru wafungwe, na shetani akiamua kukufunga anakufunga vilevile ulivyo na
gari lako na nyumba yako, basi wao wanajua moto ulishawaunguza wengine iwe wao
ambao wamewashiwa mara saba zaidi pasipo kujua wao sio kama wale sema Mimi sio
kama wale. Basi mfalme akasema watupiwe kwenye moto na wale walio wabeba
wakatekea wao kwanza hata kabla hawajaingia kwenye moto.
Mwone yuda alimsaliti Yesu lakini yeye
alienda kujinyonga kabla Yesu hajafa. Biblia inasema aliyekupandia ubaya na yeye
ubaya hautatoka nyumbani mwake”. Sasa walipoingia kwenye moto wakaonekana wanne
na mmoja kama mwana wa Mungu na vifungo vyao vimefunguka na mfalme akawaita na
watu wote wakaogopa na kutukuza mbele ya Mungu wa shdraka, meshak, na abernego.
Huyu alikuwa ni mfalme Nebukadreza.
Mfalme Dairo yeye aliweka amri ya siku 30
mtu atakaye abudu Mungu mwingine atatupwa kwenye tundu la simba lakini
aliyekuwa analengwa ni Danieli na danieli alikuwa anaabudu kwa kujificha na
baadae akaamua kufungua madirisha na milango ili asikike na wale waliokuwa
wamepanga kwaajili ya kumuondoa na kumwangamiza walimsikia na kwenda
kumshitakia kwa mfalme na mfalme akaamuru atupwe kwenye tundi la simba. Zamani
simba waliwekwa kwenye mashimo marefu na waliohukumiwa kifo walikuwa wanatupwa
kwenye tundu hilo na simba walikuwa wanakula nyama za watu tu na safari hii
wakaamuru kubadilisha asiye mwabudu mfalme atupwe huku ndipo wakamtupa danieli
na mfalme akatia mhuri kwenye jiwe hilo. Ilikuwa ni kwasababu ya wivu tu na
mfalme baadae alifahamu kumbe aliye lengwa ni danieli na akaamua kujaribu
kumuokoa Daniel pale akijua kwamba kumbe ishu hii ni kwaajili ya mtu tu. kila
mbegu iwe ni mbegu iwe ya harage,au yeyote ina mti wewe hautakatizwa hadi utoe
mti kwa jina la Yesu, ubuyu una mti ndani na ukichukua ubuyu ukaunyonya ukaweka
mfukoni mbegu yake jua kwamba una mti wa ubuyu ndani ya mfuko na ukienda
kuupanda unakuwa mti mkubwa. Kila mtu unaye mwona ana makusudi ya kufanikiwa
aliyopewa na Bwana. Watu wengi huwa wanawaza kufanikiwa ni kuolewa, kujenga nk,
hapana ni lile kusudi ulilowekewa ndani yako ulipokuja duniani na lile kusudi
likitimia unaitwa umefanikiwa na mtu anapofariki bila kufanya kusudi lake
anaitwa hajafanikiwa na kusudi haliwezi kuzuiwa na mwandamu na Ufufuo na uzima
kusudi letu ni kuigeuza Tanzania igeuke iwe Ufalme wa mwana kondoo na hakuna
atakaye weza kugeuza kusudi hili. Na Mungu amewaweka watu kwenye maisha yao
labda kutokuwapa mali nyingi kwasababu anajua kwa sampuli ya moyo huu huyu mtu
ataniacha nikimpa Gari mapema na Mungu anaruhusu jambo fulani likupate ili
akutengeneze na kwa kadiri unavyo barikiwa unatakiwa usonge mbele.
Sisi
tumeitwa kuihubiri injili hatujaitwa kuongea maneno sisi sio kama wale sisi ni
kizazi tofauti kuna watu wenye nia ya kukurudisha chini jua ya kwamba wewe sio kama wale
waliowarudisha chini. Anaye kuvuta kukushusha chini lazima yeye awe chini
kwanza lakini wewe hauetaenda chini kwa jina la Yesu, sema nakataa kurudishwa
chini na wanadamu, wachawi ,wasoma nyota, mashetani nakataa kurudishwa chini
kwa jina la Yesu.
Kuna baadi ya watu wamewekewa magonjwa na
watu ili wanataka wewe urudi chini na kama jambo hulifahamu lipime kwa wakati
na muda, na mambo yote ya shetani yana muda mfupi tu kila kilichotengenezwa na
wanadamu kina mwisho wake hatakama haupendwi na unapigwa vita na ndugu au
rafiki zako au wafanyakazi wako. Biblia imeandikwa tutamiliki milango ya adui
zetu, Mungu ni wa ajabu Yule mtu unaye mchukia ndiye anamweka mlangoni na
anaweza kuficha muujiza wako ndani ya mtu unaye mchukia. Modekai yupo mlangoni
waziri mkuu Hamani anapita ameamuru watu wote wainame anapopita. Na mfalme
alikuwa ana mungu wake na alikua anaabudu mizimu kila mwaka miezi mitatu
alikuwa anaabuddu mwenyewe bila mkewe wala mtu yeyote na haman akaongea
akaandika waraka wa kuharibu akamwambia mfalme kuna kabila moja hapa naomba
utoe amri wauliwe na akaweka ule muda mfalme alikuwa anaabudu mizimu na mfalme
akampa Yule mbaya na pete yake akaandika siku Fulani (wakati mfalme alikuwa
anaabudu mizimu yakee) akaitoa ikasambazwa ili wayahudi wauwawe. Basi haman
akaachiwa ikulu na wayahudi walipousoma waraka wa kifo, ’’ nakutaarifu kila silaha itakayofanyika juu
yangu haitafanikiwa, usifurahi ee adui yangu ninapo anguka nitainuka tena,
mabaya hayata nitapata tena’’. Wayahudi walipo uona waraka wakamlilia mfalme
ambaye hakuwepo imekuwaje lakini nakutaarifu kuachwa na watu sio kuachwa na
Mungu usiogope wakikuambia naacha kukusaidia mwambie acha usiogope Mungu tunaye
mtumikia anaweza kutuwezesha.
Waraka ukaandaliwa na anayetaka kukuua
atakufa kabla yako, Baadae kumbe mfalme huyu bila kujua kumbe mke wake yeye ni
myahudi na modekai naye alikuwa ni myahudi alikwenda kumwambia Esta unataarifa
waraka wa kuwaua wayahudi na esta akasema mfalme amekwisha kuingia kuabudu na
kwa desturi hairuhusiwi kuingia hukoesta akamwambia siwezi kuwasaidia na
Modekai akamwambia usipowaokoa wayahudi kwa njia hii Mungu atawasaidia kwa njia
nyingine na wewe pia usiposaidiwa na mtu umtegemeaye, Mungu atakusaidia na mtu
mwingine. Baadae esta akawaambia fungeni siku tatu na mimi nitaingia kwa mfalme
kinyume cha sheria na wakati huo amri inaendelea kuwepo na inawezekana wewe
kuna mpango umewekwa juu yako kukuangamiza na wewe huujui unatakiwa useme mimi
sio kama wale. Modekai akamwambia esta usipotuokoa wewe Mungu atatuokoa lakini
wewe utaangamizwa na familia yako ‘ kuna mambo hayatakiwi kubadilika na sisi
lazima injili isambae Tanzania nzima na kila mtaa usikiee majeshi majeshi
mlokole asiye kata tamaa’ sasa esta akawaambia natakam niingie kwa mfalme
kinyume cha sheria na wayahudi hawajui nini. Kila mtamgo ulio andaliwa na adui
zangu nauangamiza kwa jina la Yesu mpango wa magonjwa mpango wa ajali mahali
popote nauteketeza kwa jina la Yesu Amen.
Mfalme alivyo mwona Esta akamuuliza nini
esta akamwambia uache maombi yako ya kuabudu mizimu uje nikuandalie chakula mfalme
akatoka ndani akakaa na esta ” ukitaka kufungua moyo wa mtu mpe chakula kizuri
awe Rp au Ms wewe mpe chakula” sasa akamwambia njoo nikuandalie chakula na
mfalme akala akashiba na akamwambia naomba na kesho nikuandalie chakula lakini
safari hii naomba na waziri wako haman nayeye aje kwenye chakula hiki watatu tu
na biblia inasema haman alienda kuwaambia rafiki zake leo mimi ninakwenda kula
kwa mfalme na mkewe maana yake Mungu akitaka kuwaangamiza adui zako anaanza kuwasogeza
polepole na mwisho wao ni aibu wakati ule waraka wa kifu unatembea wayahudi
walikuwa hawajui kuna mpango wa kuwakomboa unaendelea maana yake wakati wewe
hujui shuda yako itaisha lini jua kuna mpango wa kukutoa kwenye tabu hiyo
unaendelea.
Basi
Esta wakati akila chakula na haman na mfalme Esta akamwambia kuna mpando
umeandaliwa wa mimi niuawe na tarehe imeandaliwa na mfalme akamuuliza ninani
huyo ndipo akamwambia ni huyu haman na kwa hasira akaanza kutembea kwenye
bustani na leo mfalme Yesu anatembea anaangalia. Na haman akaamua kumwangukia
Esta miguun mwake na walewale walio panga mabaya juu yako wale watakusujudia
kwa jina la Yesu maana yake shauri la
mtu mbaya huwa linageuka kuwa kitanzi kwa jina la Yesu. Yaleyale mlio
nifanyia yawe kitanzi kwa jina la Yesu. Mfalme aliporudi esta akamwambia na
Yule modekai ni mjomba wangu na nyumba ya nane haman amemuandalia msalaba wa
kumsulubushia ndipo mfalme akaamuru akasulubiwe yeye mwenyewe na leo kwa jina
la Yesu ule msalaba ulioandaliwa juu yangu uwasulubishe wao kwa jina la Yesu.
Ndipo mfalme akaandika waraka mwingine wa kuwaruhusu wayahudi kuwa atakaye kuja
kuwaua wamuue wao wenyewe na sisi tumeruhusiwa kuwasambaratisha waliojipanga
kutuua kwa jina ya Yesu. Barua ikaandikwa na tareheh ilipofika wale maadui
hawajui wakaenda na kuna waraka unasema vita sio vyenu vita ni vya Bwana na wao
watataja magari na farasi sisi tuna mkono wa Bwana kwao kuna mkono wa wanadamu
sisi tuna mkono wa Bwana wayahudi walipokwisha kujiandaa walijua kuwa wao sio
kama wale na walisimama kupigana. Maisha yamejaa watu wabaya wenye nia ya
kukurudisha chini na kukufanya uumie moyo usiogope. Sema nakataa aibu kwa jina
la Yesu. Tumepokea waraka mimi ni rungu la Bwana na silaha zake za vita jeshi
lijapo jipanga kupigana nami moyo wangu hauta ogopa Bwana ni nuru yangu na wokovu
wangu ni mwogope nani ikiwa Bwana yuko upande wetu ni nani aliye juu yetu kama
vile mji wa Yerusalemu ulivyozungukwa na milima ndivyo Bwana alivyo wazunguka
watu watakatifu wake. MIMI SIO KAMA WALE WALIOANGUSHWA NA KUONEWA KWA JINA YESU.
MAOMBI:
Katika jina la Yesu nawarudishia wao aliye
andaa niharibu mimba namrudishia yeye aliye andaa mabaya imride yeye alieandaaa
mikosi imrudie yeye mabaya yote yalioandaliwa nawarudishia wao na familia zao
kwa jina la Yesu nawarudishia wao mauti iliyo andaliwa juu yangu nairudisha
kwao kwa jina la Yesu mimi ni rungu la Bwana na silaha za Bwana katika vita
nawafyeka kwa jina la yesu waliopanga vita name nawaponda kwa jina la Yesu wachawi walioniloga kwenye kazi yangu
nawafyeka kwa jina la Yesu nawateketeza kwa moto waroho Mtakatifu nawafyeka kwa
jina Yesu walionitengezea mikosi na balaa nawa fyeka kwa jina la Yesu mimi sio
kama wale.
Kwa jina la Yesu kuna mtu mahali aliyeandaa
ubaya kwaajili yangu na familia yangu na familia yangu na kazi ninaamuru
kuanzia sasa namfyeka aliyeandaa mabaya juu yangu aliye andaa mabaya juu ya
kazi yangu namfyeka kwa jina la Yesu aliyeandaa juu ya ndoa yangu, kazi, masomo,
ajali juu yangu na familia yangu namfyeka kwa jina la Yesu waliotega mitego
naamuru kuanzia sasa mabaya yote yawapate wao kwa jina la Yesu. Imeandikwa Moto
wa Bwana ni moto ulao naachilia moto uwale maadui wote kwa jina la Yesu
Wapo wanajua utakufa waambiee wewe hujafa
kwa jina la Yesu tarehe ya leo ninaagiza kuanzia sasa kila aliyepanga mabaya
kwaajili yako mabaya hayo yampate yeye na familia yake kwa jina la Yesu na kila
aliyeandaa matatizo na aibu juu yako aibu hiyo haitakupata wewe itawapata wale
walioiandaa kwa jina la Yesu na wanaotaka ufukuzwe kazi lakini wafuzwe wao kwa
jina la Yesu. SEMA NIMESHINDAA AMEN. WEWE SIO KAMA WALE WALIOZOEA VYA KUNYONGA
VYA KUCHINJA HAWAWEZI LAKINI WEWE UMESHINDA KWA DAMU YA MWANA KONDOO, MABAYA
HAYATAKUPATA WEWE WALA TAUNI HAITAKUPATA WEWE.
![]() |
Ufufuo na Uzima,Tanganyika parkers Kawe |
Comments