BWANA YESU
asifiwe.
Baada kifo
cha Baba na Mama kutukimbia, tulichukuliwa na Bibi nikiwa na miaka 3 na nusu tu, nikiwa pamoja na kaka yangu Samwel na
mdogo wangu Kepha. Maisha awamu hii yalikuwa tofauti na mwanzo, tulihama kutoka
Mwanza mjini na kwenda kuishi kijiji cha Kibehe wilaya ya Biharamulo mkoa wa
kagera. Hali ilikuwa ni mbaya sana, kuna wakati nilidhani sikuzaliwa na watu
bali nilirushwa tu na malaika wa MUNGU kutoka mbinguni ndio maana ninaishi.ilikuwa
ni kipindi cha njaa. Babu kazi yake ilikuwa ni ulevi na akija nyumbani usiku ni
kumpiga tu bibi na kupelekea kila mtu ndani ya nyumba kulia, kwangu mimi
ilikuwa ni zaidi maana nilianza kuona aina ya maisha ambayo sitakiwi kuyaishi
na nilijua natakiwa kuishi maisha Fulani. Kuna siku nikiwa peke yangu
nilimwomba MUNGU kwamba naweka nadhiri na nadhiri hiyo ambayo nilimweleza MUNGU
ilikuwa kwamba Kama MUNGU akinipa Kazi nzuri serikalini harafu akanipa Mke
mzuri na akanipa Nyumba ya kumiliki mwenyewe basi mimi nitamtumikia MUNGU kama
kichaa ili watu wote waokolewe. Nadhiri hiyo ilikuwa ni maono yangu na maono
hayo kwa miaka zaidi ya 10 sauti yake ilikuwa inajirudia rudia ndani yangu
hivyo nilijua lazima nitimize nadhiri yangu hiyo kwa MUNGU wangu.
Leo
tunazungumzia maono.
Unapoacha
maisha maovu na kumpa BWANA YESU maisha yako unapokea maisha mapya, maisha
yaliyovuviwa na baada ya hapo utakuwa unatembea
na ROHO wa MUNGU ndani yako. Baada ya hapo utakuwa unapokea maono na
maelekezo kutoka kwa MUNGU.
Jua
linapochomoza huanza kuonekana kwanza
mwanga mdogo kasha nuru kubwa huja baadae.
Mwanzo
12:1-3 (BWANA akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;
nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka; nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.
).
MUNGU anampa
maono Ibrahimu na anamwonyesha kusudi lake.
MUNGU
anamwonyesha Ibrahimu mambo yajayo ya Ibrahimu.
Kabla na
hapo Ibrahimu hakujua anataka kupelekwa wapi lakini MUNGU alimwambia Ibrahimu
kwamba atamfanya kuwa Baraka na katika yeye watu wote watabarikiwa.
Na ni kweli
kabisa kupitia Ibrahimu watu wote hubarikiwa maana kupitia Ibrahimu BWANA YESU
alikuja (Mathayo 1:1-Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo, mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu.
) na kwa njia ya BWANA YESU watu wote watakaomwendea
wataokolewa, Uzima wa milele ambayo ndio Baraka kuu kuliko zote itapatikana kupitia
KRISTO pekee aliye Mwamba wa kabila la Yuda na yuda alitoka kwa Daudi na Daudi
alitoka kwa Ibrahimu aliyepewa maono na MUNGU.
Mwanzo
15:1-6( Baada ya mambo hayo neno la BWANA likamjia Abramu katika njozi,
likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa
sana.
Abramu akasema, Ee BWANA MUNGU,
utanipa nini, nami naenda zangu hali sina mtoto, na atakayeimiliki
nyumba yangu ni huyu Eliezeri, Mdameski?
Abramu akasema, Tazama, hukunipa uzao, na mtu aliyezaliwa nyumbani mwangu ndiye mrithi wangu. Nalo neno la BWANA likamjia likinena, Huyu hatakurithi, bali atakayetoka katika viuno vyako ndiye atakayekurithi.
Akamleta nje, akasema, Tazama
sasa mbinguni, kazihesabu nyota, kama ukiweza kuzihesabu. Akamwambia,
Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.
Akamwamini BWANA, naye akamhesabia jambo hili kuwa haki.
).
MUNGU
anapompa mtu kitu humpa na uwezo na kuona kitu hicho halisi.
Tabia moja
wapo ya ni kwamba MUNGU anafanya kazi na
mtu ambaye hazuiliwi na vitu vinavyoonekana.
2 Kor 4:18 ( tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.
).
Kitaalamu
Sarah alikuwa ni tasa lakini MUNGU neno aliloliona husimama siku zote.
Kwetu
usukumani zamani ilikuwa hivi. Watu waliogopa kupanda miti ya miembe maana
tamaduni na mila zao zilisema kwamba kila apandaye mwembe hatakula matunda ya
mwembe huo hadi kifo chake. Maana mwembe ukiupanda wewe utachelewa sana kuzaa mbele zako hadi kifo
chako, na ukitaka ule matunda ya mwembe ulioupanda wewe mwenyewe basi itokee
uwe unaukata mwembe uliupanda mwenyewe na mtu akukute ndio unaanza kuukata harafu
akukataze kukata mwembe huo basi utakula matunda ya mwembe huo.
Hiyo ilikuwa
ni desturi tu lakini vitu hivi vinavyoonekana viliwakwamisha wengi sana.
Na hii ni
mfano wa vitu ambavyo vinavyoonekana ambavyo vinawakosesha wengi haki zao.
Hata wewe
ndugu yawezekana kuna jambo ambalo hukukwamisha kuyatimiza maono yako ya
utumishi wako kwa MUNGU.
MUNGU
hapendi ukwamishwe na vitu unavyoviona ili kuyafikia maono au malengo
aliyokupangia yeye.
Ona hapa
hata baada ya Ibrahimu kuondoka, MUNGU aliendeleza kusudi lake kupitia Isaka
mwanawe Mwanzo 25:11 (Ikawa, baada ya kufa kwake Ibrahimu, MUNGU akambariki Isaka mwanawe. Naye Isaka akakaa karibu ya Beer-lahai-roi.
).
Ili kufikia
maono au malengo yake Ibrahimu. MUNGU alimwambia Ibarahimu ampe kwanza sadaka.
Hapa kwenye sadaka kuna nzuri ambayo hata wewe unaweza kutumia ili kutimiza
maono yako.
Usiiache
ahadi ya MUNGU kwako.
MUNGU
anamwambia Musa ‘’Nenda kawachukue
waisraeli uwapeleke katika nchi yao.’’
MUNGU
atakuletea mchumba wako baada yaw ewe kukaa vizuri mbele zake na tena kama vitu
vinanyoonekana havitakutisha.
Ukimpenda
YESU utamtumikia na kwa kumtumikia utakuwa umejiepusha na hatari nyingi sana.
Kwa leo naishia hapo,
MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea
BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na
atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu
kwa mafundisho kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana
makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani
aliko KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
Comments