BWANA YESU
asifiwe ndugu.
Inawezekana
unataka kumjua mtumishi au mwanafunzi wa kweli wa YESU KRISTO au yawezekana
kabisa ni wewe mwenyewe unataka kujipima ili ujue kama kweli wewe ni mwanafunzi
wa kweli wa BWANA YESU.
Biblia ina
majibu ya shwari hili. Na jibu la swali hili ni muhimu kwa kila mtu duniani.
Kipindi cha
mwanzo cha kuokoka kwangu nilikua na mitihani mingi maana haikua jambo rahisi
kuacha kwa mara moja tabia ambazo nilizizoea kuzifanya tangu utotoni. Na mara
nyingi niliamini MUNGU alikua anamueleza mchungaji wangu kila jambo baya ambalo
nimefanya, kama nimesema uongo siku hiyo nikienda kanisani mahubiri yalilenga
sana juu ya madhara ya uongo na hali hiyo ilinitisha na kuniogopesha sana
lakini MUNGU alikua ananiwazia mema sana, kwa kufundishwa kanisani nilijigundua
kabisa kwa wakati huo sikuwa mwanafunzi wa kweli wa YESU KRISTO bali nilikua
najaribu tu kuwa mwanafunzi. Neno la
MUNGU lina majibu ya kujua kama wewe au mimi ni wanafunzi wa kweli wa BWANA
YESU.
Ngoja nikupe
sifa za mtu kuwa mwanafunzi au mtumishi wa kweli wa BWANA YESU.
MTUMISHI WA
KWELI WA YESU NI HUYU.
1. Ni
mtu ambaye anajifunza sana kuendelea katika maombi. Yakobo 5:13-16 (Mtu wa kwenu amepatikana na mabaya? Na aombe. Ana moyo wa kuchangamka? Na aimbe zaburi.
Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la BWANA.
Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na BWANA atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.
Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.
)
2. Amejitoa kabisa kwa MUNGU ili MUNGU amtumie .
Warumi 12:1-2 ( Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa
huruma zake MUNGU, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya
kumpendeza MUNGU, ndiyo ibada yenu yenye maana.
Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya MUNGU )
3.
Mwanafunzi
au mtumishi yeyote lazima awe ana kusudi katika maisha yake. Wafilipi 3:7-11 (
Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya KRISTO.
Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu
mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua
KRISTO YESU, BWANA wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo
yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate KRISTO;
tena nionekane katika yeye,
nisiwe na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile
ipatikanayo kwa imani iliyo katika KRISTO, haki ile itokayo kwa MUNGU,
kwa imani;
ili nimjue yeye, na uweza wa kufufuka kwake, na ushirika wa mateso yake, nikifananishwa na kufa kwake;
ili nipate kwa njia yo yote kuifikia kiyama ya wafu.
).
4.
Kwa
neema ya MUNGU, BWANA ameondoa kila kikwazo ndani yake. Waebrania 12:1-2 (Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi
namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo
kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa
mbele yetu,
tukimtazama YESU, mwenye
kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha
iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye
ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha MUNGU.
)
Taji ya miiba kichwani mwa BWANA YESU ilikuwa na maana ya kuweka akili ya
ufalme wa MUNGU kwa wakristo ili wakilisikia neno la MUNGU lichome mioyo yao
ili wapate akili za uzima ulio katika KRISTO ambaye ni neno juu ya neno.
BWANA YESU asifiwe.
Shahidi wa kwanza wa maisha ya mtu ni mtu mwenyewe, ndugu yangu liweke
neno la MUNGU moyoni mwako na umpokee BWANA YESU ndipo utakuwa shahidi mwaminifu
na ambaye ushahidi wake ni wa uzima.
Ewe mteule wa KRISTO
Ndani yako kuna mwenyeji mmoja tu yaani YESU KRISTO , lakini wageni ni
wengi ambao ni vikwazo, dhambi na ukatishwaji tamaa lakini naomba utambue
kwamba lengo la hao wageni ni kuhakikisha hauendi mbinguni, Ndugu yangu
mwenyeji uliyempokea ana nguvu kuliko wageni wote na ukidumu na huyo mwenyeji
ndani ya moyo wako una uzima wa milele ambao pekee unatoka kwake. Songa mbele
na BWANA YESU na maadui watakimbia tu Warumi 3:23-26 ( kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa MUNGU;
wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika KRISTO YESU;
ambaye MUNGU amekwisha
kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake,ili aonyeshe
haki yake ,kwa sababu ya kuziachilia katika ustahimili wa MUNGU dhambi
zote zilzotangulia kufanywa. apate kuonyesha haki yake wakati huu, ili awe mwenye haki na mwenye kumhesabu haki yeye amwaminiye YESU.
).
Kwa leo naishia hapo,
MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea
BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na
atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu
kwa mafundisha kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana
makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani
aliko KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
MUNGU Akubariki.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
MUNGU Akubariki.
Comments