Paulo Mtume akasema;
"Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo TULIOWAHUBIRI NA ALAANIWE...."
Gal 1:8-9.
Wapendwa wangu, ikiwa sisi ni wanafunzi wa Yesu, Imetulazimu kuyachunguza maandiko!
Tunaona nyakati za Paulo na Sila watu wa Beroya waliyachunguza maandiko
Mdo 17:10-11
Na hiyo ni haki ya kila mwanafunzi wa Yesu, Maana biblia
imetutahadharisha mapema, tusiziamini kila Roho bali tuzipime hizo Roho
kama zimetokana na Mungu au la
1Yoh 4:1
Na katika kuyachunguza maandiko hapo ndipo tutakapogungua kuwa TUMEZUNGUKWA NA WALIMU WENGI WA UONGO.
Yak 3:1
Hivyo basi; niwasihi wapendwa wangu katika Kristo Yesu! Tusibabaishwe na majina makubwa makubwa waliojipachika baadhi ya Watumishi wa Mungu: Mfano NABII, MTUME, MCHUNGAJI, ASKOFU,MWALIMU, MWINJILISTI NK
#Tutawafuata wao, na Majina yao, ikiwa wao nao wanafuata KWELI YA NENO LA MUNGU na siyo vinginevyo.
#Ukiona kiongozi wako anakuambia usifuate matendo yangu bali fuata neno la Mungu,
Tambua fika huyo ni kiongozi kipofu, hafai kukuongoza!
#Yesu alikuwa kielelezo chetu, alitenda kwanza ili nasi tumfuate
Mdo 1:1
#Paulo Mtume akasema; mnifuate mimi kama mimi nilivyomfuata Kristo
1kor 11:1
Sasa huyo anayekwambia usimfuate yeye ametoa wapi hayo mafundisho? Maana kiongozi yoyote yule, anapaswa kuwa Kielelezo kwa wengine!
UKIYAONA HAYO:
Ni thahiri shairi kuwa huyo ni wa baba wa uongo yaani Ibilisi,Hafai kukufundisha, atakuambukiza Roho za Ibilisi tuu, taka usitake!
USHAURI WNG KWAKO:
Kimbia ndugu yangu uiponye Roho yako!
Mungu akubariki, kwa kuusoma ujumbe huu!
Ni maombi yangu kwa Bwana kuwa utaanza kuwachunguza hawa viongozi wetu kwa kutumia Neno la Mungu (BIBLIA) Kisha utachukua hatua!
Mungu akupe macho ya Rohoni upate kuyaona haya dhahiri! Na akupe mwongozo wa nini ufanye! Ameen
Ubarikiwe na Bwana,
Shaloom Shaloom!
By Lucy Marandu.
Tunaona nyakati za Paulo na Sila watu wa Beroya waliyachunguza maandiko
Mdo 17:10-11

1Yoh 4:1

Yak 3:1
Hivyo basi; niwasihi wapendwa wangu katika Kristo Yesu! Tusibabaishwe na majina makubwa makubwa waliojipachika baadhi ya Watumishi wa Mungu: Mfano NABII, MTUME, MCHUNGAJI, ASKOFU,MWALIMU, MWINJILISTI NK
#Tutawafuata wao, na Majina yao, ikiwa wao nao wanafuata KWELI YA NENO LA MUNGU na siyo vinginevyo.
#Ukiona kiongozi wako anakuambia usifuate matendo yangu bali fuata neno la Mungu,
Tambua fika huyo ni kiongozi kipofu, hafai kukuongoza!
#Yesu alikuwa kielelezo chetu, alitenda kwanza ili nasi tumfuate
Mdo 1:1
#Paulo Mtume akasema; mnifuate mimi kama mimi nilivyomfuata Kristo
1kor 11:1
Sasa huyo anayekwambia usimfuate yeye ametoa wapi hayo mafundisho? Maana kiongozi yoyote yule, anapaswa kuwa Kielelezo kwa wengine!
UKIYAONA HAYO:
Ni thahiri shairi kuwa huyo ni wa baba wa uongo yaani Ibilisi,Hafai kukufundisha, atakuambukiza Roho za Ibilisi tuu, taka usitake!
USHAURI WNG KWAKO:
Kimbia ndugu yangu uiponye Roho yako!
Mungu akubariki, kwa kuusoma ujumbe huu!
Ni maombi yangu kwa Bwana kuwa utaanza kuwachunguza hawa viongozi wetu kwa kutumia Neno la Mungu (BIBLIA) Kisha utachukua hatua!
Mungu akupe macho ya Rohoni upate kuyaona haya dhahiri! Na akupe mwongozo wa nini ufanye! Ameen

Ubarikiwe na Bwana,
Shaloom Shaloom!
By Lucy Marandu.
Comments