Meriam akiwa na mumewe (mwenye shati la manjano) na watoto wake pamoja na jamaa mara baada ya kuachiwa. ©Getty Images |
Mara baada ya mahakama ya rufaa
kwa kutoa uamuzi mpya unaopinga hukumu aliyopewa mwanamama Meriam Yahya
Ibrahim, aliyehukumiwa kifo kwa kunyongwa nchini Sudan kwa tuhuma za
kubadili dini, mwanamama huyo amekamatwa tena na polisi wa nchini humo
akiwa uwanja wa ndege kuelekea Marekani pamoja na mumewe, Daniel Mani,
ambapo aliamini angepata pumziko kutokana na misukosuko aliyopata.
BI Meriam |
Mumewe, ambaye ni raia wa Marekani ameelezea kuwa kulikuwa na mvutano
kwenye uwanja wa ndege wa Khartoum, ambapo alikuwa ameongozana na mkewe
pamoja na watoto wao wawili kuelekea Marekani, kabla wanausalama zaidi
ya 40 kujitokeza na kumkamata upya Meriam.
Hukumu ya Meriam ambayo imezua mijadala ya kimataifa, ilipelekea
mashinikizo kadhaa kutoka jumuiya mbalimbali, ikiwemo baraza la Congress
nchini Marekani, ambapo wajumbe 38 walisaini waraka wakitaka taifa lao
lichukue hatua kuhakikisha usalama wa Meriam na watoto wake wawili,
ambapo hivi karibuni alijifungua mtoto wa pili, Maya, akiwa gerezani -
huku ikiripotiwa kuwa akiwa kwenye uchungu, bado miguu yake ilikuwa
imefungwa minyororo.
Meriam, mwenye umri wa miaka 27 - alikamatwa kwa mara ya kwanza Agosti
2013, baada ya ndugu wa baba yake kuripoti kwamba amezini (baada ya
kuolewa na Wani, ambaye ni mkristo), ambapo katika utetezi wake, Meriama
ameeleza bayana kwamba yeye ni mkristo, kama ambavyo mama yake
amemkuza, baada ya baba yake, ambaye ni muislamu, kuiacha familia hiyo
tokea Meriam akiwa mdogo.
Miongoni mwa viongozi wa mataifa makubwa walioolani ni pamoja na waziri
wa mambo ya nje wa Australia, Bi Julie Bishop, waziri mkuu wa zamani wa
Uingereza, Tony Blair pamoja na waziri mkuu wa sasa, David Cameron.
Kiongozi mwingine ni katibu wa taifa la Marekani, Bi Hillary Clinton.
By Gospel kitaa.
Comments