
BWANA YESU
asifiwe.
MUNGU
ameutunza ujumbe huu ndani yangu kwa
muda mrefu sana, leo naomba tujifunze pamoja.
MWENDO WA
CHOMBO CHAKO UKOJE?
Mwendo ni
IMANI.
Chombo ni
WOKOVU.
Kwahiyo
ujumbe huu tunaweza tukauita kwamba ‘’IMANI YA WOKOVU WAKO IKOJE?
Kumbuka
kwamba tunapozungumzia Chombo na Mwendo ina maana kuna safari na tayari chombo
kipo njiani kikielekea sehemu Fulani.
Kwa habari
ya wateule wa MUNGU safari yetu haina kituo
na kituo chetu ni kimoja tu yaani
yaani mbinguni ukitaka kushuka
unashuka wewe lakini watakatifu safari badi inaendelea.
Waebrania
11:1,6 ''Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana, Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye
MUNGU lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale
wamtafutao''
Hapo kwenye
hilo andiko tunaona mwendo ambao mwanadamu anatakiwa atembee nao.
Imani ni
mwendo, imani ni ya muhimu sana. Wengi wana imani lakini imani zao sio za
kumwabudu MUNGU aliye hai anayepatikana katika KRISTO YESU pekee.
Imani ya
kweli ya uzima ni imani katika MUNGU aliye hai na Biblia katika Wakolosai 2:2 b
inasema ''KRISTO ni siri ya MUNGU '' maana yake ukitaka kumwabudu au kumfahamu MUNGU
wa kweli basi MUNGU huyo anapatikana katika KRISTO YESU.
Je wewe
ambaye uko kwenye Chombo(wokovu) mwendo (Imani) wako ukoje? Je unasua sua au
mawimbi yanataka kukuzamisha baharini(duniani?)
Katika
chombo chako ni changamoto gani unazokutana nazo?
Ufanye nini
ili uende salama kwenye chombo chako?
Ndugu yangu
mteule wa MUNGU nakuomba katika katika changamoto zako usisitesite wala kurudi
nyuma.
Mtegemee
YESU huyo huyo uliyemtumaini tangu
mwanzo.
Unapokutana na changamoto
katika safari yako ni kipi kinachokupa nguvu? Ni kipi unategemea Biblia
ina jibu juu ya nani wa kumtegemea wakati wa changamoto ndani ya chombo chako
Luka 4: 1-12 (''a YESU, hali amejaa ROHO MTAKATIFU, alirudi kutoka Yordani, akaongozwa na ROHO muda wa siku arobaini nyikani, akijaribiwa na Ibilisi. Na siku hizo alikuwa hali kitu; hata zilipotimia, aliona njaa.
Ibilisi akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa MUNGU, liambie jiwe hili liwe mkate.
YESU akamjibu, Imeandikwa ya kwamba mtu hataishi kwa mkate tu. Akampandisha juu, akamwonyesha milki zote za ulimwengu kwa dakika moja. Ibilisi akamwambia, Nitakupa
wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami
humpa ye yote kama nipendavyo. Basi, wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako.
YESU akajibu akamwambia, Imeandikwa, Msujudie BWANA MUNGU wako, umwabudu yeye peke yake.
Akamwongoza mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya kinara cha hekalu, akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa MUNGU, jitupe chini;
kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake wakulinde;
na ya kwamba,mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
YESU akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu BWANA MUNGU wako.''
=YESU
alimtegemea ROHO MTAKATIFU ambaye ndiye
aliyemuongoza.
BWANA YESU asifiwe.
=Huyo
unayemtegemea anapata faida gani au hasara.
Isaya 61:1-3 ''Roho ya BWANA MUNGU i juu yangu; kwa sababu BWANA amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao. Kutangaza mwaka wa BWANA uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha MUNGU wetu; kuwafariji wote waliao; kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya haki, iliyopandwa na BWANA, ili atukuzwe.''
Isaya 61:1-3 ''Roho ya BWANA MUNGU i juu yangu; kwa sababu BWANA amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao. Kutangaza mwaka wa BWANA uliokubaliwa, na siku ya kisasi cha MUNGU wetu; kuwafariji wote waliao; kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti ya haki, iliyopandwa na BWANA, ili atukuzwe.''
=Hasara kama
tukitumia akili zetu wenyewe
Mithali 23:4
''Usijitaabishe ili kupata utajiri; Acha kuzitegemea akili zako mwenyewe.''
=Hakika ni hasara kubwa kama tukizitegemea akili zetu wenyewe.
Mithali 23:4
''Usijitaabishe ili kupata utajiri; Acha kuzitegemea akili zako mwenyewe.''
=Hakika ni hasara kubwa kama tukizitegemea akili zetu wenyewe.
Je mwendo
wako ni wa kusitasita au ni wa kumaanisha pale unapopita kwenye mabonde au
milima?
Ayubu 5:1-2 ''Haya, ita sasa; je! Yuko atakayekujibu? Nawe utamwelekea yupi katika hao watakatifu? Kwani hasira humwua mtu mpumbavu, Nao wivu humwua mjinga.''
Ayubu 5:1-2 ''Haya, ita sasa; je! Yuko atakayekujibu? Nawe utamwelekea yupi katika hao watakatifu? Kwani hasira humwua mtu mpumbavu, Nao wivu humwua mjinga.''
=Ukiwa hapa
duniani mwangalie tu aliyekuita tu .
Hata dhahabu
lazima ipite kwenye moto ndipo iwe dhahabu safi
Yoshua 1:7 ''Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda sawasawa na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiiache, kwenda mkono wa kuume, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako''
Yoshua 1:7 ''Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda sawasawa na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiiache, kwenda mkono wa kuume, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako''
=Ndugu zangu
lazima tutambue kwamba kwenye safari yetu lazima tutakutana na nyakati tofauti
tofauti lakini nakuomba linda moyo wako kuliko yote uyalindayo harafu linda
macho yako na pia linda kinywa chako.
2 Timotheo 3:1 ''Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. ), Mhubiri 3:1 ( Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu. ), 2 Timotheo 3: 12-13 (Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika KRISTO YESU wataudhiwa. lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika. ''
2 Timotheo 3:1 ''Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari. ), Mhubiri 3:1 ( Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu. ), 2 Timotheo 3: 12-13 (Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika KRISTO YESU wataudhiwa. lakini watu wabaya na wadanganyaji wataendelea, na kuzidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika. ''
=Tukumbuke
kwamba safari yetu haina kituo na kituo
chetu ni kimoja tu yaani mbinguni. Ukitaka kushuka unashuka wewe tu lakini safari kwa watakatifu
inaendelea kama kawaida .
Mathayo 25:1-10.
Mathayo 25:1-10.
=Tuongeze
mafuta ya taa zetu ambayo ni kujitakasa
na kuongeza maombi
Isaya 61:10 '' Nitafurahi sana katika BWANA, nafsi yangu itashangilia katika MUNGU wangu; maana amenivika mavazi ya wokovu, amenifunika vazi la haki, kama bwana arusi ajipambavyo kwa kilemba cha maua, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vyombo vya dhahabu''
=Tufurahie wokovu wetu.
Isaya 61:10 '' Nitafurahi sana katika BWANA, nafsi yangu itashangilia katika MUNGU wangu; maana amenivika mavazi ya wokovu, amenifunika vazi la haki, kama bwana arusi ajipambavyo kwa kilemba cha maua, na kama bibi arusi ajipambavyo kwa vyombo vya dhahabu''
=Tufurahie wokovu wetu.
Katika
mwendo wa chombo chetu kuna ushindi mkubwa.
Ayubu 19:25 ''Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi''
=Kuna ushindi mkuu kwa wateule maana BWANA YESU alikwisha tushindia pale msalabani ndio maana hata majina yetu yakaandikwa kwenye kitabu cha uzima mbinguni maana tumeokoka na tunaishi maisha ya wokovu.
Ayubu 19:25 ''Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi''
=Kuna ushindi mkuu kwa wateule maana BWANA YESU alikwisha tushindia pale msalabani ndio maana hata majina yetu yakaandikwa kwenye kitabu cha uzima mbinguni maana tumeokoka na tunaishi maisha ya wokovu.
Wafilipi
4:4-7,13 ''Na amani ya MUNGU, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika KRISTO YESU.
Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.''
Comments