|
Ndugu,
baada ya kuona tunavyopaswa kuishi
kwa kusadiki, kuadhimisha na kupenda,
ni wakati wa kuzama katika fumbo la Mungu kwa njia ya sala.
|
Roho Mtakatifu, anayetuwezesha kusadiki, kuadhimisha na kupenda,
ndiye pia anayetuongoza katika sala hasa,
kama alivyowafanyia Yesu, Maria na umati wa wenzetu,
hata wasiofahamu kweli zote tulizofunuliwa na Mungu.
|
Nyuma yao hata wewe funga safari ya Kiroho
ya kuongea na Mungu aliye hai,
Baba, Mwana na Roho Mtakatifu,
kwa imani, tumaini na upendo mkubwa zaidi na zaidi.
|
Hakuna mwingine ambaye ni muhimu uongee naye
kuliko Mwenyezi Mungu, Muumba na Mwokozi wako.
|
Maisha yako yote, ya sasa na ya milele, yamo mikononi mwake:
unamtegemea kabisa upande wa mwili, tena zaidi upande wa roho.
|
La ajabu ni kwamba ana hamu ya kuongea nawe
kuliko wewe mwenyewe,
kwa kuwa anakupenda zaidi:
daima ndiye wa kwanza katika upendo.
|
Kwa nini usinyamaze mbele yake ili kusikiliza sauti yake ya fumbo?
Kwa nini usimuitikie kama Yesu alivyofanya?
Kwa nini usiache Roho Mtakatifu ndani mwako
amlilie na kusema naye kwa dhati,
akimuita Baba kwa niaba yako na ya viumbe vyote?
|
Hapa mbele utakuta baadhi ya maneno ya sala
yaliyobubujika mioyoni mwa watu wa Mungu,
wanaume kwa wanawake, karne hata karne.
|
1
|
Kwa hakika utamu wake utakusaidia kutambua
jinsi mafumbo ya imani yalivyo hai na ya kuvutia;
siyo nadharia ya dini iliyo mbali na maisha,
bali ndiyo kiini chake.
|
Zama ndani ya Mungu kwa kuongea naye:
hapo utazidi kuishi kwa utulivu na furaha ya dhati!
|
SALA KUTOKA BIBLIA
|
ABRAHAMU (Mwa 18:27)
|
Nimeshika kusema na Bwana, nami ni mavumbi na majivu tu.
|
YAKOBO (Mwa 32:26)
|
Sikuachi, usiponibariki!
|
MUSA (Kut 33:18)
|
Nakusihi unionyeshe utukufu wako.
|
GIDEONI (Amu 6:15)
|
Ee Bwana, nitawaokoa
Israeli kwa jinsi gani?
Tazama, jamaa zangu ndio walio maskini sana katika Manase,
na mimi ndimi niliye mdogo
katika nyumba ya baba yangu.
|
SAMWELI (1Sam 3:10)
|
Nena, Bwana, kwa kuwa mtumishi wako anasikia.
|
DAUDI (2Sam 7:18)
|
Mimi ni nani, Bwana Mungu, na nyumba yangu ni nini,
hata umenileta
hata hapa?
|
DAUDI (2Sam 24:17)
|
Tazama, ni mimi niliyekosa,
ni mimi niliyepotoka;
lakini kondoo hawa,
wamefanya nini?
Mkono wako na uwe juu yangu, na juu ya nyumba ya baba yangu!
|
DAUDI (1Nya 29:10-13)
|
2
|
Uhimidiwe, Ee Bwana, Mungu
wa Israeli baba yetu, milele na milele.
Ee Bwana, ukuu ni wako, na
uweza, na utukufu, na kushinda, na enzi;
maana vitu vyote
vilivyo mbinguni na duniani ni vyako.
Ufalme ni wako, Ee Bwana, nawe umetukuzwa, u mkuu juu ya vitu vyote.
Utajiri na heshima hutoka
kwako wewe, nawe watawala juu ya vyote;
na mkononi
mwako mna uweza na nguvu;
tena mkononi mwako mna
kuwatukuza na kuwawezesha wote.
Basi sasa, Mungu wetu,
twakushukuru na kulisifu jina lako tukufu.
|
SULEMANI (1Fal 3:9)
|
Nipe mimi mtumwa wako moyo
wa adili niwahukumu watu wako,
na kupambanua
mema na mabaya;
maana ni nani awezaye kuwahukumu hawa watu wako walio wengi?
|
SULEMANI (1Fal 8:23)
|
Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe,
mbinguni juu wala
duniani chini!
Ushikaye maagano na rehema
kwa watumishi wako,
waendao mbele zako kwa
mioyo yao yote.
|
ELIYA (1Fal 18:36-37)
|
Ee Bwana, Mungu wa Ibrahimu, na wa Isaka, na wa Israeli,
na ijulikane leo ya kuwa wewe ndiwe Mungu katika Israeli,
na ya kuwa mimi
ni mtumishi wako,
na ya kuwa nimefanya mambo
haya yote kwa neno lako.
Unisikie, Ee Bwana, unisikie,
ili watu hawa wajue
ya kuwa wewe, Bwana,
ndiwe Mungu,
na ya kuwa wewe umewageuza
moyo wakurudie.
|
ELIYA (1Fal 19:4)
|
Yatosha! Sasa, Ee Bwana, uiondoe roho yangu;
kwa kuwa mimi si mwema kuliko
baba zangu.
|
YEREMIA (Yer 15:16)
|
Maneno yako yalionekana,
nami nikayala;
na maneno yako yalikuwa
ni furaha kwangu,
na shangwe ya
moyo wangu,
maana nimeitwa kwa jina lako, Ee Bwana, Mungu wa majeshi.
|
AZARIA (Dan 3:37-40)
|
3
|
Sisi, Ee Bwana, tumekuwa
duni kuliko maìtaifa mengine yote,
na kudhulumiwa leo katika ulimwengu wote kwa sababu ya dhambi zetu.
Sasa hakuna mfalme
wala nabii wala kiongozi;
hakuna dhabihu wala
kafara wala sadaka wala uvumba,
wala mahali pa kukutolea
dhabihu na kuona rehema.
Lakini kwa moyo uliovunjika na kwa roho nyenyekevu tukubaliwe nawe,
na sadaka
yetu iwe machoni pako leo
kama dhabihu
za kondoo waume na ng’ombe,
na kama
kondoo wanono elfu kumi.
Nasi tukufuate kwa unyofu, maana wanaokutumaini Wewe hawataaibika.
|
VIJANA WATATU (Dan 3:52-56)
|
Umehimidiwa, Ee Bwana,
Mungu wa baba zetu,
wastahili kusifiwa na
kuadhimishwa milele.
Limehimidiwa jina lako
takatifu, tukufu.
lastahili kusifiwa na
kuadhimishwa milele.
Umehimidiwa katika hekalu
la fahari yako takatifu,
wastahili kusifiwa
na kutukuzwa milele.
Umehimidiwa juu ya kiti
cha ufalme wako.
wastahili kusifiwa na
kuadhimishwa milele.
Umehimidiwa utazamaye vilindi, uketiye juu ya makerubi,
wastahili kusifiwa na
kuadhimishwa milele.
Umehimidiwa katika
anga la mbinguni,
wastahili kusifiwa
na kutukuzwa milele.
|
BIBI ARUSI (Wim 8:6-7)
|
Nitie kama muhuri
moyoni mwako,
kama muhuri
juu ya mkono wako;
kwa maana upendo
una nguvu kama mauti,
na wivu ni
mkali kama ahera.
Mwako wake
ni mwako wa moto,
na miali yake
ni miali ya Bwana.
Maji mengi hayawezi
kuuzimisha upendo,
wala mito
haiwezi kuuzamisha.
Kama mtu angetoa badala ya upendo mali yote ya nyumbani mwake,
angedharauliwa
kabisa.
|
KUJIOMBEA HEKIMA (Hek
9:1-6)
|
Ee Mungu wa baba zetu, Bwana, mwenye kuihifadhi rehema yako,
umevifanya vitu
vyote kwa neno lako;
na kwa Hekima yako ukamwumba
mwanadamu,
ili avitawale viumbe
vilivyoumbwa nawe,
|
4
|
na kumiliki ulimwengu
katika utakatifu na kwa haki,
na kutoa hukumu
kwa unyofu wa moyo.
Nakusihi
unipe Hekima,
ambayo huketi karibu
nawe katika kiti chako cha enzi,
wala usinikatae mimi
miongoni mwa watumishi wako;
mimi niliye mtumwa wako,
na mwana wa mjakazi wako,
mtu dhaifu
asiye na siku nyingi,
wala sina nguvu ya
kufahamu hukumu na sheria.
Kwa maana mtu ajapokuwa ni mkamilifu miongoni mwa wanadamu,
pasipo Hekima itokayo
kwako atahesabiwa kuwa si kitu.
|
ZABURI YA 8
|
Wewe, Mungu, Bwana
wetu,
jinsi lilivyo tukufu jina
lako duniani mwote!
Wewe umeuweka utukufu wako
mbinguni.
Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao
umeiweka misingi
ya nguvu;
kwa sababu yao wanaoshindana
nawe;
uwakomeshe adui na mijilipiza
kisasi.
Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako,
mwezi na nyota ulizoziratibisha;
mtu ni kitu gain hata
umkumbuke,
na binadamu hata
umwangalie?
Umemfanya mdogo punde kuliko
Mungu;
umemvika taji ya utukufu
na heshima;
umemtawaza juu ya kazi
za mikono yako;
umevitia vitu vyote chini
ya miguu yake.
Kondoo, na ng’ombe
wote pia;
naam, na wanyama
wa kondeni;
ndege wa angani, na samaki
wa baharini;
na kila kipitiacho
njia za baharini.
Wewe, Mungu, Bwana
wetu,
Jinsi lilivyo tukufu jina
lako duniani mwote!
|
ZABURI YA 123
|
Nimekuinulia macho yangu,
wewe uketiye mbinguni.
Kama vile macho ya watumishi kwa mkono wa bwana zao;
kama macho ya mjakazi kwa
mkono wa bibi yake;
hivyo macho yetu humlekea
Bwana, Mungu wetu,
hata atakapoturehemu.
Uturehemu, Ee Bwana,
uturehemu sisi,
kwa maana tumeshiba
dharau.
Nafsi zenu zimeshiba
mzaha wa wenye raha,
na dharau ya
wenye kiburi.
|
5
|
ZABURI YA 130
|
Ee Bwana, toka vilindini nimekulilia;
Bwana, uisikie
sauti yangu.
Masikio yako na yaisikilize
sauti ya dua zangu.
Bwana, kama Wewe ungehesabu
maovu,
Ee Bwana, nani angesimama?
Lakini kwako kuna msamaha, ili Wewe uogopwe.
Nimemngoja Bwana, roho yangu
imemngoja,
na neno lake nimelitumainia.
Nafsi yangu inamngoja
Bwana,
kuliko walinzi waingojavyo
asubuhi,
naam, walinzi waingojavyo
asubuhi.
Ee Israeli, umtarajie
Bwana;
maana kwa Bwana kuna
fadhili,
na kwake kuna ukombozi
mwingi.
Yeye atawakomboa Israeli na maovu yake yote.
|
BIKIRA MARIA (Lk 1:38)
|
Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana;
na iwe kwangu kama ulivyosema.
|
SIMEONI (Lk 2:29-32)
|
Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi
wako,
kwa amani, kama ulivyosema;
kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako,
uliouweka tayari machoni
pa watu wote;
nuru ya kuwa mwangaza
wa Mataifa,
na kuwa utukufu wa watu
wako Israeli.
|
YOHANE MBATIZAJI (Math
3:14)
|
Mimi nahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu?
|
MKOMA (Mk 1:40)
|
Ukitaka, waweza kunitakasa.
|
MWANAMKE MSAMARIA (Yoh
4:15)
|
Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka.
|
WAGALILAYA (Yoh 6:34)
|
6
|
Bwana, sikuzote utupe chakula hiki.
|
MWANDISHI (Math 8:19)
|
Mwalimu, nitakufuata kokote uendako.
|
WANAFUNZI WA YESU (Math
8:25)
|
Bwana, tuokoe, tunaangamia.
PEPO (Mk 5:7,12)
|
Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu?
Nakuapisha kwa Mungu
usinitese...
Tupeleke katika nguruwe, tupate kuwaingia wao.
|
MWANAMKE MKANANAYO (Math
15:22,25,27)
|
Unirehemu, Bwana,
Mwana wa Daudi.
Binti yangu amepagawa
sana na pepo.
Bwana,
unisaidie.
Hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.
|
PETRO (Mk 9:5)
|
Rabi, ni vizuri sisi kuwapo hapa; na tufanye vibanda vitatu,
kimoja chako wewe, kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya.
|
BABA WA MTOTO ALIYEPAGAWA (Mk
9:24)
|
Naamini, nisaidie kutokuamini kwangu.
|
MWANAFUNZI WA YESU (Lk
11:1)
|
Bwana, tufundishe
sisi kusali,
kama vile Yohane alivyowafundisha wanafunzi wake.
|
MTOZAUSHURU (Lk 18:13)
|
Ee Mungu, uniwie radhi mimi mwenye dhambi.
|
KIJANA TAJIRI (Mk 10:17)
|
Mwalimu mwema, nifanye nini nipate kuurithi uzima wa milele?
|
BARTIMAYO (Mk 10:47,48,51)
|
7
|
Mwana wa Daudi, Yesu, unirehemu!
Mwana wa Daudi, unirehemu!
Mwalimu wangu, nataka nipate kuona.
|
MARTHA (Yoh 11:21-22,27)
|
Bwana, kama ungalikuwapo
hapa, ndugu yangu hangalikufa.
Lakini hata sasa najua ya kuwa yoyote utakayomwomba Mungu,
Mungu
atakupa...
Naam, Bwana, mimi nimesadiki ya kwamba wewe ndiwe Kristo,
Mwana wa Mungu,
yule ajaye ulimwenguni.
|
MHALIFU (Lk 23:42)
|
Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.
|
YESU (Math 11:25-26)
|
Nakushukuru, Baba, Bwana
wa mbingu na nchi,
kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili,
ukawafunulia watoto
wachanga.
Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako
|
YESU (Yoh 11:41-42)
|
Baba, nakushukuru
kwa kuwa umenisikia.
Nami nalijua ya kuwa
wewe wanisikia sikuzote;
lakini kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya,
ili wapate kusadiki
kwamba ndiwe uliyenituma.
|
YESU (Yoh 17:1-26)
|
Baba,
saa imekwisha kufika.
Mtukuze Mwanao, ili
Mwana wako naye akutukuze wewe;
kama vile ulivyompa
mamlaka juu ya wote wenye mwili,
ili kwamba wote
uliompa awape uzima wa milele.
Na uzima
wa milele ndio huu:
wakujue wewe, Mungu wa pekee
wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.
Mimi nimekutukuza duniani,
hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.
Na sasa, Baba,
unitukuze mimi pamoja nawe,
kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako.
Jina lako nimewadhihirishia
watu wale ulionipa katika ulimwengu;
walikuwa wako, ukanipa
mimi, na neno lako wamelishika.
Sasa wamejua ya kuwa
yote uliyonipa yatoka kwako.
Kwa kuwa maneno
uliyonipa nimewapa wao;
|
8
|
nao wakayapokea, wakajua
hakika ya kuwa nalitoka kwako,
wakasadiki
ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
Mimi nawaombea
hao; siuombei ulimwengu;
bali
hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako;
na wote walio wangu
ni wako, na walio wako ni wangu;
nami nimetukuzwa ndani yao.
Wala mimi simo tena ulimwenguni,
lakini hawa
wamo ulimwenguni, nami naja kwako.
Baba mtakatifu,
kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa,
ili
wawe na umoja kama sisi tulivyo.
Nilipokuwapo pamoja nao,
mimi naliwalinda
kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza;
wala
hapana mmojawapo wao aliyepotea,
ila yule
mwana wa upotevu, ili andiko litimie.
Na sasa naja
kwako;
na maneno
haya nayasema ulimwenguni,
ili wawe na
furaha yangu imetimizwa ndani yao.
Mimi nimewapa neno
lako, na ulimwengu umewachukia,
kwa kuwa wao si wa ulimwengu,
kama mimi nisivyo wa ulimwengu.
Mimi siombi
kwamba uwatoe katika ulimwengu;
bali uwalinde na yule mwovu.
Wao si wa ulimwengu,
kama mimi nisivyo wa ulimwengu.
Uwatakase kwa
ile kweli; neno lako ndiyo kweli.
Kama vile
ulivyonituma mimi ulimwenguni,
nami vivyo
hivyo naliwatuma hao ulimwenguni.
Na kwa
ajili yao najiweka wakfu mwenyewe,
ili na hao watakaswe katika kweli.
Wala si hao tu ninaowaombea;
lakini na wale
watakaoniamini kwa sababu ya neno lao.
Wote wawe na
umoja;
kama wewe, Baba,
ulivyo ndani yangu, nami ndani yako,
hao nao wawe ndani yetu,
ili ulimwengu upate kusadiki
ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma.
Nami utukufu ule ulionipa nimewapa
wao,
ili wawe
na umoja kama sisi tulivyo umoja.
Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja;
ili ulimwengu
ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma,
ukawapenda wao kama ulivyonipenda
mimi.
Baba, hao ulionipa
nataka wawe pamoja nami popote nilipo,
wapate na
kuutazama utukufu wangu ulionipa;
kwa maana ulinipenda
kabla ya kuwekwa msingi ulimwengu.
Baba mwenye haki, ulimwengu haukukujua;
lakini mimi nalikujua, na
hao wamejua ya kuwa ndiwe uliyenituma.
Nami naliwajulisha
jina lako, tena nitawajulisha hilo,
ili pendo lile ulilonipenda
mimi liwe ndani yao, nami niwe ndani yao.
|
9
|
YESU (Mk 14:36)
|
Aba, Baba, yote yawezekana kwako; uniondolee kikombe hiki;
walakini, si kama nitakavyo
mimi, bali utakavyo wewe.
|
YESU (Mk 15:34)
|
Eloi, Eloi,
lama sabakthani?
(maana yake, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?)
|
YESU (Lk 23:46)
|
Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu.
|
MARIA MAGDALENA (Yoh 20:16)
|
Raboni!
(maana yake, Mwalimu wangu!)
|
TOMA (Yoh 20:28)
|
Bwana wangu na Mungu wangu!
|
PETRO (Yoh 21:17)
|
Bwana, wewe wajua yote;
wewe umetambua ya kuwa nakupenda.
|
KANISA LA YERUSALEMU (Mdo
4:24-30)
|
Bwana,
wewe ndiwe Mungu,
ndiwe uliyefanya mbingu
na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo;
nawe ulinena
kwa Roho Mtakatifu
kwa kinywa cha
babaetu Daudi, mtumishi wako:
Mbona mataifa
wamefanya ghasia,
na makabila
wametafakari ubatili?
Wafalme
wa dunia wamejipanga,
na wakuu wamefanya shauri pamoja juu ya Bwana na juu ya Kristo wake.
Maana ni kweli, Herode na Pontio
Pilato
pamoja na
Mataifa na watu wa Israeli,
walikusanyika
katika mji huu
juu ya Mtumishi wako
mtakatifu Yesu, uliyemtia mafuta,
ili wafanye yote ambayo
mkono wako na mashauri yako
yamekusudia
tangu zamani yatokee.
Basi sasa,
Bwana, yaangalie matisho yao;
ukawajalie watumwa wako
kunena neno lako kwa ujasiri wote,
|
10
|
ukinyosha
mkono wako kuponya;
ishara na maajabu vifanyike kwa jina la Mtumishi wako mtakatifu Yesu.
|
STEFANO (Mdo 7:59-60)
|
Bwana Yesu, pokea roho yangu…
Bwana, usiwahesabie dhambi hii.
|
PAULO (Mdo 22:10)
|
Nifanye nini, Bwana?
|
WAZEE 24 MBINGUNI (Ufu
4:11)
|
Umestahili wewe, Bwana
wetu na Mungu wetu,
kuupokea utukufu
na heshima na uweza,
kwa kuwa wewe ndiwe
uliyeviumba vitu vyote,
na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa.
|
WENYE UHAI 4 NA WAZEE 24 MBINGUNI (Ufu 5:9-10)
|
Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake;
kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia
Mungu kwa damu yako
watu wa kila kabila
na lugha na jamaa na taifa,
ukawafanya kuwa ufalme na
makuhani kwa Mungu wetu;
nao wanamiliki
juu ya nchi.
|
WAFIADINI MBINGUNI (Ufu
6:10)
|
Ee Mwenyezi, Mtakatifu,
Mwenye kweli,
hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu
kwa hao wakaao
juu ya nchi?
|
WAZEE 24 MBINGUNI (Ufu
11:17-18)
|
Tunakushukuru wewe, Bwana Mungu Mwenyezi, uliyeko na uliyekuwako,
kwa sababu umeutwaa uweza
wako ulio mkuu, na kumiliki.
Na mataifa walikasirika,
hasira yako nayo ikaja,
na wakati ukaja
wa kuhukumiwa waliokufa,
na wa kuwapa thawabu yao
watumwa wako manabii na watakatifu,
na hao walichao jina
lako, wadogo kwa wakubwa,
na wa kuwaharibu
hao waiharibuo nchi.
|
WASHINDI MBINGUNI (Ufu
15:3-4)
|
Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi;
|
11
|
Ni za haki, na za kweli, njia
zako, Ee Mfalme wa mataifa.
Ni nani asiyekucha, Ee Bwana,
na kulitukuza jina lako?
Kwa kuwa wewe peke
yako u Mtakatifu;
kwa maana mataifa yote watakuja na kusujudu mbele zako;
kwa kuwa matendo yako ya haki
yamekwisha kufunuliwa.
|
ROHO MTAKATIFU NA BIBIARUSI (Ufu
22:20)
|
ITAENDELEAAAAA............
MUNGU akubariki sana.
By Dickson Haji.
Comments