|
|
SALA ZA WANAKANISA KARNE KWA KARNE
|
MWANDISHI WA DIDAKEE (80
hivi)
|
Tunakushukuru, Baba yetu,
kwa mzabibu
mtakatifu wa Daudi mtumishi wako,
uliotujulisha
kwa njia ya Kristo Mwanao.
Utukufu
ni wako hata milele…
Kama vile mkate huu
uliomegeka ulitawanyika vilimani,
nao kisha
kukusanywa umekuwa kitu kimoja,
vivyo hivyo Kanisa lako
likusanywe toka mipaka ya dunia
katika ufalme wako:
kwa kuwa
utukufu na nguvu ni vyako
kwa njia ya
Yesu Kristo hata milele…
Tunakushukuru, Baba mtakatifu,
kwa
ajili ya jina lako takatifu,
ulilolifanya likae mioyoni mwetu,
na pia kwa ajili ya
ujuzi, imani na uzima usio na mwisho
ulivyotufunulia
kwa njia ya Yesu Mwanao.
Utukufu
ni wako hata milele.
Wewe, Baba mwenyezi, uliviumba vyote kwa ajili ya jina lako,
ukawajalia wanadamu
chakula na kinywaji ili wakusifu;
lakini sisi
umetuneemesha chakula na kinywaji cha kiroh
na cha uzima wa
milele kwa njia ya Yesu Mwanao.
Kwanza
tunakushukuru kwa kuwa u Mwenyezi.
Utukufu
ni wako hata milele.
Ulikumbuke, Bwana, Kanisa lako,
uliokoe na kila uovu na
kulikamilisha katika upendo wako,
Ulitakase na
kulikusanya toka pepo nne
katika
ufalme wako uliloliandalia;
kwa kuwa nguvu na
utukufu ni vyako milele.
Neema ya Mungu
itufikie na ulimwengu huu upite.
Hosana, Mwana wa Daudi!
Aliye mtakatifu
aje, na asiye hivyo aongoke.
|
12
|
Maranatha! Amina!
|
MT. KLEMENTI I (30-96)
|
Wewe umefunua macho ya mioyo yetu, ili tukujue wewe Mungu pekee,
uliye juu
sana katika mbingu za juu,
mtakatifu
unayekaa kati ya watakatifu,
ambaye
unanyenyekeza ufidhuli wao wenye kiburi,
unabatilisha mashauri ya mataifa,
unawainua juu
wanyonge na kuwashusha wanaojikweza,
wewe ambaye
unatajirisha na kufukarisha, unaua na kuhuisha,
ambaye
peke yako unafadhili roho
na ni Mungu
pekee wa kila mwenye mwili,
unatazama vilindi,
unachunguza matendo ya wanadamu,
unawasaidia waliopo
hatarini na ni mkombozi wa waliokata tamaa,
ni muumbaji
na mtunzaji wa roho zote,
unazidisha mataifa duniani,
ambaye kati ya
wote umewachagua wanaokupenda,
kwa njia ya
Yesu Kristo Mwanao mpendwa,
ambaye kwa njia yake
umetulea, umetutakasa na kutuvika heshima.
Tunakusihi, Bwana,
uwe kwetu msaidizi na tegemeo.
Uwakomboe walio taabuni
kati yetu, uwahurumie wanyonge,
uwainue
walioanguka, ujidhihirishe kwa wahitaji,
uwaponye wagonjwa,
uwarudishe waliojitenga na taifa lako,
uwashibishe wenye
njaa, uwafungue wafungwa wetu,
uwaimarishe
walio dhaifu, uwatulize walio duni.
Mataifa yote wapate kujua
ya kuwa ndiwe Mungu, wewe peke yako,
na ya
kuwa Yesu Kristo ni Mwanao
nasi tu wako
wako na kondoo wa malisho yako.
|
MT. POLIKARPO (70-155)
|
Ee
Bwana, Mwenyezi Mungu,
Baba wa Mwanao
mpenzi na mbarikiwa Yesu Kristo,
ambaye kwa
njia yake tumekufahamu;
Mungu wa malaika na
wa wenye uwezo, wa kila kiumbe
na wa kizazi chote
cha waadilifu wanaoishi mbele yako:
mimi nakubariki kwa
kuwa siku hii na saa hii umenijalia
nishiriki kikombe cha
Kristo wako pamoja na wafiadini wote,
kwa ufufuo wa roho na
wa mwili katika uzima wa milele,
katika hali ya
kutoharibika kwa njia ya Roho Mtakatifu.
Niweze leo
kupokewa pamoja nao mbele yako
kama
sadaka nono na ya kupendeza,
kama vile wewe, Mungu usiye na hila na msemakweli, ulivyoiandaa
ukanionyesha
mapema na sasa umeitimiza.
Kwa sababu hiyo na kwa
mambo yote mimi nakusifu, nakuhimidi,
|
13
|
nakutukuza pamoja na kuhani wa milele na wa kimbingu Yesu
Kristo,
Mwanao mpenzi, ambaye kwa njia yake kwako na kwa Roho Mtakatifu
uwe utukufu
sasa na nyakati zijazo. Amina.
|
ORIGEN (185-253)
|
Yesu,
miguu yangu ni michafu.
Njoo kama mtumwa kwangu,
mimina maji katika beseni yako,
njoo
unitawadhe miguu.
Ninapoomba hivyo
najua kuwa nathubutu mno,
lakini naogopa
tishio lililotolewa uliponiambia,
“Nisipokutawadha
miguu, huna ushirika nami”.
Basi, osha miguu yangu, kwa kuwa naonea shauku urafiki wako.
|
MT. HILARI (315-367)
|
Mungu,
Baba Mwenyezi, najua vema kuwa
huduma kuu
inayonipasa kwako katika maisha yangu ni kwamba
kila
neno na wazo langu liseme juu yako.
Kipawa cha kusema
ulichonijalia hakiwezi kunipa furaha kubwa
kuliko ile ya kukutumikia kwa kuhubiri
na kuonyesha kwa ulimwengu usiokujua, au kwa mzushi
anayekukanusha,
jinsi ulivyo, yaani
Baba, Baba ambaye Mwanae pekee ni Mungu.
Lakini kwa kusema
haya, nasema tu ninachotaka kufanya.
Ili niweze kukifanya kweli nahitaji kuomba msaada wako na huruma
yako,
kuomba ujaze
upepo tanga nilizozipandisha kwa ajili yako
na
uzisukume mbele katika mwendo wangu,
yaani umvuvie Roho
wako katika imani yangu na katika kuiungama,
na
uniwezeshe kuendelea mahubiri niliyoyaanza…
Acha niseme nawe,
Mwenyezi Mungu, ingawa ni mavumbi na majivu tu,
acha niseme kwa uhuru kwa kuwa
nimefungamana nawe
kwa vifungo vya upendo.
Kabla sijakufahamu nilikuwa si kitu.
Nilikuwa na
bahati mbaya ya kutojua maana ya maisha,
nilikuwa sijielewi,
nilikuwa tofauti kabisa na jinsi nilivyo.
Huruma yako ndiyo iliyonipa uhai…
Muda wote ambao
nitaishi na kupumua kwa pumzi uliyonipa,
Baba Mtakatifu,
Mwenyezi Mungu, nitakiri kwamba tangu milele yote
wewe si Mungu tu, bali Baba pia.
Sitakuwa kamwe
na kichaa na uovu wa kujifanya hakimu
wa uwezo wako
usio na mipaka, wala wa mafumbo yako,
hata nipendelee
wazo langu maskini kuliko yale ambayo
dini inakiri
juu ya ukuu wako usio na mipaka
au imani
inafundisha kuhusu umilele wake…
Nakuomba,
utunze salama imani hiyo uliyonijalia,
na kunifadhilia
kwamba muda wote wa maisha yangu niweze tu
|
14
|
kuzingatia yale ambayo
dhamiri yangu inasema juu yake.
Niweze daima kushika imani niliyoiungama nilipozaliwa upya,
Nishike ungamo lake
nililolitamka nilipobatizwa
kwa jina la Baba, na
la Mwana na la Roho Mtakatifu.
Niweze
kukuabudu wewe, Baba yetu,
na kumuabudu
Mwanao pamoja nawe;
niweze kuwa jinsi Roho
wako Mtakatifu anavyotaka niwe,
yeye atokaye kwako
kwa njia ya Mwanao pekee.
|
MT. EFREM (306-373)
|
Mwokozi wetu, msalaba wako ulikomesha uhai wa mwili.
Utujalie
tusulubishe kiroho nafsi yetu.
Ufufuko wako, Yesu, ukuze utu wa kiroho ndani mwetu…
Umbile duni la mwili
wetu linatuelekeza kufa.
Mimina juu yetu
upendo wako wa Kimungu,
ufute moyoni mwetu
matokeo ya sisi kuelekea kifo.
|
MT. GREGORI WA NAZIENZI (329-390)
|
Ee Bwana, umpokee
mikononi mwako kaka yangu aliyetuacha.
Kwa
wakati wake utupokee sisi pia,
kisha kutuongoza katika
hija ya duniani hadi lengo ulilotupangia.
Utujalie tuje
kwako tukiwa tayari na watulivu kweli,
si tumevurugwa na
hofu, si katika hali ya uadui nawe,
walau siku ya
mwisho, siku ya kufariki kwetu.
Utujalie tusijisikie
tunaondolewa na kung’olewa kwa nguvu
katika ulimwengu na maisha,
wala kwa hiyo
tusifunge safari shingo upande.
Bali utujalie
tuje kwa utulivu na utayari mzuri,
kama watu wanaoondoka kuendea uzima wa heri usio na mwisho,
uzima ule ulioma
katika Kristo Yesu, Bwana wetu,
ambaye apate
utukufu milele na milele. Amina.
|
MT. MAKRINA (330-380)
|
Ee Bwana, wewe
umetuondolea hofu ya kifo.
Mwisho wa maisha yetu hapa umeufanya mwanzo wa uzima wa kweli.
Kwa kitambo tu
utaacha miili yetu ilale usingizi,
halafu kwa tarumbeta ya
mwisho utaiamsha kutoka usingizini.
Wewe unaukabidhi
udongo ukutunzie udongo wako huu
ulioufinyanga kwa mikono yako;
nawe utauchukua tena na
kutoka fungu la kufa, lisilo na muundo,
utaugeuza
kuwa na uzuri usiokufa.
|
MT. GREGORI WA NISA (335-394)
|
15
|
Ee Mchungaji
mwema, unakwenda wapi kuchunga,
wewe
unayebeba mabegani kundi lako lote?
Kwa kuwa kondoo yule pekee
anawakilisha
ubinadamu wote uliobeba mabegani mwako.
Unionyeshe mahali pa pumziko,
unifikishe
kwenye majani mema ya kunilisha,
uniite kwa jina, ili
mimi pia, niliye kondoo, niweze kusikia sauti yako
na kwa hiyo
niweze kupata uzima wa milele:
“Unionyeshe mpenzi wa roho yangu”.
Ndivyo ninavyokuita, kwa
kuwa jina lako liko juu ya kila jina na uelewa,
wala ulimwengu wote wa viumbe wenye akili hauwezi kulitaja
nakulielewa.
Basi, jina
lako, ambamo wema wako unajitokeza,
unawakilisha upendo wa roho yangu kwako.
Kwa kuwa ningewezaje
kutokupenda, baada ya wewe kunipenda mno?
Ulinipenda hivi hata
ukatoa uhai wako kwa kundi la malisho yako.
Haiwezekani
kufikiria upendo mkuu kuliko huo.
Umelipa
wokovu wangu kwa uhai wako.
|
MARTIN WA TOURS (316-397)
|
Ee Bwana, nikihitajiwa bado na watu wako, sikatai uchovu wa
kazi:
utakalo lifanyike!
|
MT. AMBROSI (340-397)
|
Ee Bwana, mwenye huruma
kwa wote, uniondolee dhambi zangu,
na kwa huruma washa ndani mwangu moto wa Roho wako Mtakatifu.
Uniondolee moyo wa
jiwe na kunipa moyo wa nyama,
moyo wa
kukupenda na kukuabudu wewe,
moyo wa kupata raha
ndani yako, kukufuata na kukufurahia
kwa ajili ya Kristo.
|
MT. JEROMU (347-420)
|
Ee Bwana, umetupatia Neno lako kama nuru ambayo iangazie njia
yetu;
utujalie
tulitafakari Neno lako na kufuata mafundisho yake
hivi kwamba tuone
hiyo nuru inazidi kuangaza hadi adhuhuri,
|
Comments