TAMELA MANN ASHINDA TUZO ZA BET KIPENFELE CHA GOSPO (GOSPEL)


Kila jambo lina mwanzo na mwisho wake, kama mwanadamu anazaliwa na baadae anakufa, basi siku ya jana ilikuwa ndio siku ya mwisho wa tuzo la BET. Wenye kuchaguliwa walichaguliwa na wakupigwa chini walipigwa chini. Lakini Bwana Yesu Kristo hakuangushwa alizidi kutawala katika tuzo hizi. Tunamshukuru mtumishi wa Mungu TAMELA MANN ambaye alishinda katika tuzo hizi zinazofanyika kila mwaka zikishirikisha mataifa mbalimbali.

Katika kipengele cha watu wa Mungu yaani Gospel kulikuwa na waimbaji watano ambao ni kama wafuatao Donnie McClurkin, Erica Campbell, Hezekiah Walker, Tamela Mann*WINNER na Tye Tribbett
Kama unavyojua katika mashindano lazima mmoja aibuke mshindi, basi Tamela aliweza kuwa mkali kwa mavoko yakutisha na uimbaji wake kwa ujumla.

Kazi ya Mungu ukifanya kwa asilimia zote kama vile unavyohakikisha tumbo lako linakuwa limejaa na haliumizwi na njaa, Mungu aweza kukuinua tu hata iweje.

Comments