BWANA YESU
atukuzwe ndugu yangu.
Karibu
tujifunze jambo la muhimu la kuhusu miaka na Baraka ambazo MUNGU anatupa.
Waamuzi
17:1-13 ( Wakati huo alikuwako mtu mmoja wa nchi ya vilima ya Efraimu, ambaye jina lake alikuwa akiitwa Mika.
.........................Mama yake akasema, Mimi naziweka fedha hizi
kabisa ziwe wakfu kwa BWANA, zitoke mkononi mwangu kwa ajili ya
mwanangu, ili kufanya sanamu ya kuchonga, na sanamu ya kusubu; basi kwa
hiyo nakurudishia wewe.
Basi hapo alipomrudishia mama
yake hizo fedha, mama yake akatwaa fedha mia mbili, akampa fundi mwenye
kusubu fedha, naye akafanya sanamu ya kuchonga kwazo, na sanamu ya
kusubu; ambazo zilikuwa ndani ya nyumba ya Mika.
Basi mtu huyo Mika alikuwa na
nyumba ya miungu, naye akafanya naivera, na kinyago, akamweka wakfu
mmoja miongoni mwa wanawe, akawa kuhani wake.
).
Ndugu yangu
unaitumiaje miaka yako ya kuishi?
MUNGU alimpa
Mika vitu vingi lakini Mika alivitumia vibaya.
Kuna njia
unawaza kuiendea lakini ikawa sio nzuri.
Miaka ya
Mika aliitumia vibaya wakiwa na mama yake maana kwa miaka kadhaa aliyumika kama
kuhani wa miungu.
Mika
alimwibia mama yake na tena hata baada
ya hapo mika aliendelea kutumia vibaya miaka yake maana aliitumikia miungu.
Mama yake na
mika alimtumia mika katika ibada ya shetani, Ndugu yangu usikubali mtu yeyote
akakutumia katika mambo yake ya kipepo maana utaitumia vibaya miaka yako.
Zaburi 90:12
(Basi, utujulishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima.
).
Unaitumiaje
miaka yako ya kuishi?
Unaitumiaje
miaka yako ya kukaa Tanzania kama wewe mteule wa KRISTO?
Unaitumiaje
miaka yako ya kukaa Kenya au Uganda wewe mteule wa BWANA YESU?
Unaitumiaje
miaka yako ya kukaa Kongo au Rwanda au Burundi au Ulaya wewe mteule wa KRISTO?
MUNGU
anatufundisha kuitumia vizuri miaka yetu. Mwanzo 5:25-27 ( Mahalaleli akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi.
Mahalaleli akaishi baada ya kumzaa Yaredi miaka mia nane na thelathini, akazaa wana, waume na wake.
Siku zote za Mahalaleli ni miaka mia nane na tisini na mitano, akafa.
)
Methusela
aliishi miaka mingi kuliko wanadamu wote
lakini miaka yake aliitumia sio kwa utumishi mzuri kwa MUNGU. Historia
yake inazungumzia tu kuoa na kuzaa watoto.
-Ukiitumia vibaya
miaka yako utasababisha hasara kubwa
kwako na kwa ndugu zako.
- MUNGU
akulinde miaka yako yote na uache habari njema ambayo itakuwa mfano kwa wengine
kwa miaka mingi ijayo.
Waamuzi
18:27-31 ( Nao wakakitwaa hicho alichokuwa amekifanya Mika, na kuhani aliyekuwa
naye nao wakafikilia Laisha, kwenye watu waliokuwa wenye starehe na
hifadhi, wakawapiga kwa makali ya upanga; wakaupiga moto mji wao.
Wala hakuwako mwokozi, kwa
sababu huo mji ulikuwa ni mbali sana na Sidoni, nao hawakuwa na shughuli
na mtu awaye yote; na mji huo ulikuwa katika hilo bonde lililo karibu
na Bethrehobu. Nao wakaujenga huo mji na kukaa humo.
Wakauita mji jina lake Dani,
kwa kuliandama jina la baba yao Dani, aliyezaliwa kwake Israeli; lakini
jina la mji huo hapo kwanza ulikuwa ukiitwa Laisha.
Kisha wana wa Dani
wakajisimamishia hiyo sanamu ya kuchonga; na Yonathani mwana wa
Gershomu, mwana wa Musa, yeye na wanawe walikuwa ni makuhani katika
kabila ya Wadani hata siku ya kuchukuliwa mateka hiyo nchi.
Basi wakajisimamishia hiyo sanamu ya kuchonga aliyoifanya Mika, wakati wote ile nyumba ya MUNGU ilipokuwako huko Shilo. ).
Hapa tunaona hasara mbaya sana ambayo ilisababishwa na Mika.
-Fanya kitu
ambacho kitamletea hasara shetani na sio faida.
Kwa leo naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
+255714252292
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
Kwa leo naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
+255714252292
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
Comments