
BWANA YESU
asifiwe.
Leo
tunazungumzia Maombi ya kukesha.
Maombi ni
mkono mrefu wa kupokea kile ukitakacho kutoka kwa MUNGU.
Kukesha
maana yake ni kudumu.
Maombi
lazima yawe na mkesha au kukesha pia mkesha lazima uwe na maombi.
Mkristo
anatakiwa awe na maombi ya kukesha na anatakiwa adumu katika maombi miaka yake
yote.
Mtu anavuna
alichopanda, ukipanda kwa maombi ya mkesha utapokea.
Zaburi
91:15-16( Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni, Nitamwokoa na kumtukuza;
Kwa siku nyingi nitamshibisha, Nami nitamwonyesha wokovu wangu.
).
-Huwezi
kuitika kama hujaitwa na MUNGU hawezi kukuitikia kama hujamwita.
-Tunamwita
MUNGU katika maombi na tunapaswa tumwite siku zote, Ndipo hata uhusiano wetu na
MUNGU utakuwa imara.
-Mitume
walimwita MUNGU akawaitikia.
-Manabii
walimwita MUNGU akawaitikia.
-Hata wewe
unaweza ukamwita MUNGU leo na ukapokea ila uwe na nia ya kweli.
Nia ya kweli ni ipi? Mathayo
6:5 ( Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali
wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na
watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.
)
1. Kutokupayuka
payuka.
2. Kutojionyesha kwa watu.
Luka
11:11-13( Maana ni yupi kwenu aliye baba, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe au samaki, badala ya samaki atampa nyoka?
Au akimwomba yai, atampa nge?
).
-Tuombe
maombi tukiwa watakatifu.
-Tuombe
tukiwa wasafi wa mioyo.
-Tuombe
tukiwa katika KRISTO YESU na MUNGU atajibu maombi.
Tuwe
waaminifu wa kweli kwa BWANA. Zaburi 55:16-17 (Nami nitamwita MUNGU, Na BWANA ataniokoa;
Jioni, asubuhi, na adhuhuri nitalalama na kuugua, Naye ataisikia sauti yangu.
).
Ndugu yangu
usiende kanisani kuomba tu bali na kukesha.
Zaburi
34:1-4 (Nitamhimidi BWANA kila wakati, Sifa zake zi kinywani mwangu daima. Katika BWANA nafsi yangu itajisifu, Wanyenyekevu wasikie wakafurahi.
Mtukuzeni BWANA pamoja nami, Na tuliadhimishe jina lake pamoja.
Nalimtafuta BWANA akanijibu, Akaniponya na hofu zangu zote.
).
BWANA YESU
asifiwe.
Maombi ya
kukesha ndio maombi yatakayokuzingira siku zote dhidi ya kila mpango wa giza,
utafika ambako wengine hawawezi kufika.
Omba kwa
kukesha na katika maombi yako siku zote
omba kwa imani maana pasipo imani huwezi kupokea.
Luka 21:36(
Basi, kesheni ninyi kila wakati, mkiomba, ili mpate kuokoka katika haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.
).
Maombi ni
maisha.
Kwa leo naishia hapo,
MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea
BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na
atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu
kwa mafundisho kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana
makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani
aliko KRISTO BWANA.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
MUNGU akubariki sana .
Ni mimi ndugu yako
Peter M Mabula
Maisha ya Ushindi Ministry.
0714252292
MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.
Comments