"UJUE ULIMWENGU WA ROHO" na Mwl. Christopher Mwakasege

Ujue Ulimwengu wa roho.


Kwa wewe unayetaka kujifunza mambo mengi ya MUNGU na kujifunza kuhusu ulimwengu wa ROHO tafuta kitabu hiki kitakusaidia sana.
Katika kitabu hiki utajifunza mambo mengi yanayohusu ulimwengu wa roho katika mpangilio wa sura kumi kama ifuatavyo;

1. Kufahamu umuhimu wa kujua uhalisi wa kuwepo kwa ulimwengu wa roho. 

2. Kwa njia ya maombi unaweza kuwa mahali kiroho ambapo huwezi kuwa kimwili. 

3. Mtu aliumbwa aishi katika maeneo mawili kwa wakati mmoja. 

4. Mungu anakukaribisa katika ulimwengu wa roho ushiriki maamuzi pamoja naye kwa njia ya maombi yako.


  5. Kufanikiwa kwako katika maombi kunategemea unavyoitunza na unavyoitumia nafasi yako uliyonaayo katika ulimwengu wa roho. 

6. Tambua umuhimu wa nafasi unayoitumia unapomwomba Mungu. 

7. Chanzo cha mamlaka uliyonayo katika ulimwengu wa roho kwa njia ya maombi. 

8. Umuhimu wa kujijua unajulikanaje katika ulimwengu wa Kiroho.

9. Inawezekana Mungu amejibu maombi yako ila yamekwama katika ulimwengu wa roho. 

10. Kwa maombi yako ingia katika ulimwengu wa roho ili ubadili hali ya ulimwengu wa kimwili.

Unaweza kupata nakala yako katika ofisi zao  zilizopo Dar es salaam jengo la Luther house au Arusha mjini karibu na ofisi za tanesco. Pia kinapatikana katika semina  mbalimbali za Mwl. Mwakasege. 
Na Mwl. Christopher Mwakasege

Comments