![]() |
Maombi ni silaha ya kila mkristo. |
Kitabu cha Nahumu sura 1:9, inasema unawaza nini juu ya Bwana?
Yeye ambaye anaweza kukomesha mateso tunayopitia.
Mpendwa mwana wa Mungu yako mambo mengi tumekuwa tukiomba na kulia mbele za Mungu,
bila kupata majibu. Leo hii Mungu anauliza
unawaza nini juu yake? Hili ni swali gumu lakini kwa mtu aliye Rohoni ni
jepesi sana.
Ø Kila
mtu aliyeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu,
tambua kuwa kuna vitu vya thamani ndani yako, ambavyo ni vipawa na karama. Na
Mungu leo anataka uvitumie hivyo katika kuujenga ufalme wake ili akuinue na kukupatia
yale mahitaji unayoyaomba kwake. Maana maandiko yanasema utafuteni kwanza
ufalme wa Mungu na mengine yote mtazidishiwa.
Ø Mwana
wa Mungu haijalishi kwamba unapitia magumu kiasi gani au uko katika mazingira gani?
Mungu anataka
akutumie ili uubadilishe huu ulimwengu. Usijidharau hajalishi kuwa wewe ni :-
-Mzee
- Mtoto
-Haujasoma au ni masikini Mungu anataka akutumie vile
ulivyo.
Ø Tukimwangalia
nabiiYeremia katika kitabu kile cha Yeremia sura 1:1……………..
Yeremia yeye alikuwa
anajitetea kuwa ni mtoto lakini Mungu alimwambia kuwa ataweka maneno katika kinywa
chake, na kumpatia uweza wakung’oa, kubomoa na kuharibu.
Ø Mungu
anaangalia mtu aliyeko tayari ili amtumie. Ni mara ngapi Mungu amesema na wewe lakini
unatoa uzuru? Ondoa hofu, woga, kutokujiamini ili Mungu akutumie.
Ø Mungu
anapokupa maono wewe usisite wala usiangalie kwamba huna pesa au haujasoma Chukua
hatua na Mungu atainua watu wa kuyategemeza hayo maono.
Tukiangalia katika kitabu
cha Nehemia 2:1…………, tunaona jinsi Mungu alivyompa Nehemia Maono ya kuujenga ukuta
ule wa Yerusalemu, Nehemia baada ya Mungu kusema naye alibeba mzigo wa yale maono
kasha akafunga na kuomba na Mungu akamwinulia watu wakuifanikisha ile kazi ya kuujenga
ukuta wa Yerusalemu.
Ø Tumeomba
miaka mingi , tumefunga, lakini bado hatujajibiwa haja zetu, wengine tunaomba,
Wenzi wa maisha, watoto,
ndoa zetu kupona, kuinuliwa uchumi,
biashara zetu kuongezeka,kuponywa magonjwa nk. Lakini bado hivi vyote havijatimia,
hatatumefikiahatuayakumlaumuMungu,nakudhanikuwaanaubaguzi la hasha! Mungu anataka
ufanye ya kwake na yeye afanye ya kwako.
Ø Wengine
tunajisifia tumeokoka siku nyingi tunasema tuna miaka ishirini ya mwokovu,
lakini hatujaweza kufanya kitu chochote kwenye ufalme wa Mungu. Hata kumshuhudia
mtu mmoja hatujawahi? Wako watu wagonjwa wamekosa tumaini, wako walevi wako makahaba,
usiache wakafia dhambini,Unasubiriwa wewe ufungue kinywa chako useme neno ili waweze
kuwekwa huru.
( Yohana 12:
26) inasema mtu akinitumikia na anifuate
name nilipo na mtumishi wangu atakuwepo. Tena mtu akinitumikia baba atamheshimu.
Jina la Yesu libarikiwe
Haleluyaa,
mtumikie Mungu ili na yeye akutumikie.
Amen.
E Lyimo.
Comments