BWANA YESU
asifiwe.
Somo hili
litakusaidia kujua kiwango chako cha imani.
Karibu.
Yamkini utajifahamu uko kiwango gani cha imani.
Imani ni
kuwa na uhakika wa mambo unayotarajia.
Imani ni
hakika.
Imani yako
itaonekana kwenye maombi yako, sadaka na
chochote ukifanyacho kwa utukufu wa MUNGU.
Imani ni
coordinator wa kuyapeleka maombi yako kwa MUNGU.
Imani ina
macho na inaona.
Unaweza ukaiita kwamba ni IMANI YA KUSAIDIWA NA WENGINE
Hii ni imani lakini ni haba.
Isingekuwa imani YESU asingeizungumzia kwamba ipo imani haba. Mfano Petro
alipotaka kuzama kwenye maji baada ya
kuanza kutembea na baada ya kuona shaka
alianza kuzama, hii ni imani haba . Ndugu mashaka yako yanaweza kuwa msiba kwako,
mashaka yamezaa imani haba. YESU alimshika mkono Petro na kumsaidia.
Imani haba ni imani ya kusaidiwa na wengine.
-Wengi wana imani haba yaani wana imani ya kushikwa mikono ndipo waweze.
-Imani haba yenyewe haiwezi kwenda mpaka isaidiwe Mathayo 14:30-31 (Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, BWANA, niokoe.
Mara YESU akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye IMANI HABA, mbona uliona shaka?
).
Wakati huu Petro alikuwa na imani haba.
Tuangalie pia maandiko ambapo
BWANA YESU anazungumzia imani hapa.
Mathayo 8: 23-26 (Akapanda chomboni, wanafunzi wake wakamfuata.
Kukawa msukosuko mkuu baharini, hata chombo kikafunikizwa na mawimbi; naye alikuwa amelala usingizi.
Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwamsha, wakisema, BWANA, tuokoe, tunaangamia.
Akawaambia, Mbona mmekuwa waoga, enyi wa IMANI HABA? Mara akaondoka, akazikemea pepo na bahari; kukawa shwari kuu.
)
Kipindi hiki wanafunzi wa YESU walikua na imani hapa yaani walikuwa na
imani ya kusaidiwa.
2.
Kiwango
cha pili cha imani ni IMANI INAYOJITEGEMEA.
Tunaweza tukaiita IMANI INAYOJITOSHELEZA.
Mathayo 9:22( YESU akageuka, akamwona, akamwambia, Jipe moyo mkuu, binti yangu; imani yako imekuponya. Yule mwanamke akapona tangu saa ile.
)
Imani inayojitegemea ni imani ambayo haiwasumbui wachungaji.
Imani inayojitosheleza ni imani ambayo inaleta matokeo bila kumsumbua
BWANA YESU ona hapa Marko 2:1-12 ( Akaingia Kapernaumu tena, baada ya siku kadha wa kadha, ikasikiwa ya kwamba yumo nyumbani.
Wakakusanyika watu wengi, isibaki nafasi hata mlangoni; akawa akisema nao neno lake.
Wakaja watu wakimletea mtu mwenye kupooza, anachukuliwa na watu wanne.
Na walipokuwa hawawezi
kumkaribia kwa sababu ya makutano, waliitoboa dari pale alipokuwapo; na
wakiisha kuivunja wakalitelemsha godoro alilolilalia yule mwenye
kupooza.
Naye YESU, alipoiona imani yao, akamwambia yule mwenye kupooza, Mwanangu, umesamehewa dhambi zako.
Na baadhi ya waandishi walikuwako huko, wameketi, wakifikiri mioyoni mwao,
Mbona huyu anasema hivi? Anakufuru. Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa mmoja, ndiye MUNGU?
Mara YESU akafahamu rohoni mwake kwamba wanafikiri hivyo nafsini mwao, akawaambia, Mbona mnafikiri hivi mioyoni mwenu?
Vyepesi ni vipi, kumwambia mwenye kupooza, Umesamehewa dhambi zako, au kusema, Ondoka, ujitwike godoro lako, uende?
Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (hapo amwambia yule mwenye kupooza),
Nakuambia, Ondoka, ujitwike godoro lako uende nyumbani kwako. Mara akaondoka, akajitwika godoro lake, akatoka mbele yao wote; hata wakastaajabu wote, wakamtukuza MUNGU, wakisema, Namna hii hatujapata kuiona kamwe. ).
Nakuambia, Ondoka, ujitwike godoro lako uende nyumbani kwako. Mara akaondoka, akajitwika godoro lake, akatoka mbele yao wote; hata wakastaajabu wote, wakamtukuza MUNGU, wakisema, Namna hii hatujapata kuiona kamwe. ).
Imani hii inaleta matokeo makubwa.
Huyu ndugu alikuwa hajaokoka ndio maana BWANA YESU alimwambia ‘’
Umesamehewa dhambi zako’’ lakini waliomleta pamoja nay eye mwenyewe walikua na
imani inayojitegemea , walikua na imani kwa YESU ndio maana uzima uliingia kwake.
-Imani inaongea ndio maana imani iliwaongoza njia, imani iliwaambia toboeni dari, imani
hapo inaongea. Imani inaposema toboa dari haikosei ila inauhakika kwamba YESU
yupo . Dari ndio ilikua kizuizi cha mwisho
na hata kwako ipo dari ambayo ndio kizuizi chako cha mwisho ili upokee muujiza wako ni lazima utoboe dari ndio upone. Dari yako hakikisha
inatoboka na wewe unakutana na YESU na
kupokea muujiza wako. Yawezekana dari yako
hujatoboa ili kukutana na YESU . Dari yako yawezekana ni wewe kufika tu
kwenye mkutano wa injili, yawezekana dari yako ni wewe kufika kanisani ili kuombewe. Toboa dari leo
ili upone.
3.
Kiwango
cha 3 cha imani ni IMANI PUNGUFU.
Imani pungufu ni tofauti na imani
haba yaani hii ni imani ya furaha ya muda lakini yakitokea magumu kidogo tu
inakimbia. Ni kama chupa ya soda ila haijajaa.
Imani hii ni ya rahu ila kukitokea ugumu kidogo au kuzidiwa na jambo
Fulani kwa muda inaweza ikatimua mbio.
Mathayo 17:19-20 ( Kisha wale wanafunzi wakamwendea YESU kwa faragha wakasema Mbona sisi hatukuweza kumtoa?
YESU akawaambia, Kwa sababu
ya UPUNGUFU WA IMANI yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani
kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule;
nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.
).
Imani hii ni furaha ya muda tu
magumu yakitokea inaweza kuzimika au kuhama kanisa kabisa na kukimbia.
Luka 8:13 ( Na wale penye mwamba ndio wale ambao wasikiapo hulipokea lile neno kwa
furaha; nao hawana mizizi, huamini kitambo kidogo, na wakati wa
kujaribiwa hujitenga.
)
Mtu mwenye imani hii anaweza kuwa ni muumini mzuri tu kanisani , anaweza
kuwa mwimbaji,shemasi au kiongozi kanisani lakini kanisa likipita kwenye ugumu
kidogo anahama.
Wengine asipotembelewa tu wakati anaumwa anahama kanisa hiyo ni imani
pungufu.
Wengine kwa sababu wana imani pungufu wanakimbia makanisa yenye idadi
ndogo ya waumini na kwenda kwenye makanisa makubwa ambako wanajua hawataambiwa
mchango wa ujenzi wa kanisa hii ni imani pungufu. Hili ni kundi kubwa sana la
watu. Wenye imani hii hawataki shida ,
ikitokea tu wanakimbia.
Ndugu ningependa utambue kwamba
Kadiri unavyokua kiroho ndivyo na jaribu
lako linakuwa kubwa. Usikimbie bali
mtumikie MUNGU kwa uaminifu.
4.
Kiwango
cha 4 cha imani ni IMANI KUBWA.
Mathayo 15:21-28 ( YESU akaondoka huko, akaenda kando pande za Tiro na Sidoni.
Na tazama, mwanamke
Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu,
BWANA, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.
Wala yeye hakumjibu neno.
Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake;
kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.
Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
Naye akaja akamsujudia, akisema BWANA, unisaidie.
Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.
Akasema, Ndiyo, BWANA, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.
Ndipo YESU akajibu, akamwambia, Mama, IMANI YAKO NI KUBWA; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile.
)
Hiyo ndio imani kubwa na BWANA mwenyewe anathibitishwa kwamba hii ni
imani kubwa.
BWANA YESU alimwambia Yule ndugu mwenye imani kubwa kwamba ‘’ Iwe kama
ulivyotaka’’ kwa sababu alikua na imani kubwa.
Mama huyu kwanza alikutana na wanafunzi, wakamwambia unatupigia kelele
lakini imani kubwa ikavuka kikwazo hicho.
Kikwazo cha pili YESU alimwambia kwa kumjaribu kwamba yeye hakuja kwa
ajili ya watu wasio Waisraeli lakini imani kubwa ikavuka na kikwazo hiki.
Kikwazo cha 3 YESU alimwambia kwa kumjaribu kwamba haiwezekani mbwa kula chakula cha watoto,
yaani aliitwa mbwa lakini imani kubwa ilikivuka kikwazo hiki.
Hebu tusome pia Mathayo 8:10-13 (
YESU aliposikia hayo, alistaajabu, akawaambia wale waliomfuata, Amin,
nawaambieni, Sijaona IMANI KUBWA namna hii, kwa ye yote katika Israeli.
Nami nawaambieni, ya kwamba
wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na
Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni;
bali wana wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Naye YESU akamwambia yule akida, Nenda zako; na iwe kwako kama ulivyoamini. Mtumishi wake akapona saa ile ile.
)
YESU anasema kwamba hajawahi kuona imani kubwa katika Israel kama ya Yule
akida.
Ndugu yangu najua umefahamu kiwango chako cha imani baada ya kujifunza
ujumbe huu. Tunatakiwa viwango vyetu
vikue. Mitume walimwambia BWANA YESU awaongezee imani Luka 17:5 (Mitume wakamwambia Bwana, Tuongezee imani.
).
Je wewe uko kundi gani la imani?
Comments