YESU ANABADILISHA MAISHA YA WATU; JOSEPH NYUKI ALIKUA CHOKORA MIAKA KUMI.




JOSEPH NYUKI.



BWANA YESU asifiwe.
Katika kupitia profile za watumishi wa MUNGU  nimekutana na ujumbe ambao ulinitia moyo sana.
Ujumbe huo ni kutoka kwa Mwimbaji nyota kwa nyimbo za injili Joseph Nyuki ambaye ameandika ujumbe huu ambao hakika ni wa kumtukuza BWANA YESU.
Joseph Nyuki ameandika hivi.

Nampenda sana Yesu Sababu amebadilisha maisha yangu Amenilinda maisha yangu saana, nilie kua chokora nimeishi kulala nje kwenye mauchafu kwa miaka kumi 10 lakini He changes my life.



Mwimbaji huyu ana albamu 3 mpaka sasa na ambazo zilifanya vizuri sana na hata sasa zinafanya vizuri albamu hizo ni BWANA YESU NITEGEMEO LANGU ambayo ni albamu ya kwanza, ya pili ni SIDANGANYIKI na ya tatu ni MAMBO KWA YESU.

Ni mwimbaji mwenye vipaji tofauti vingi. MUNGU hakika amembariki mtumishi wake huyu na ndio maana anamtukuza BWANA YESU aliyemuokoa na kumtoa kwenye uchokoraa na sasa mpakwa mafuta wa bwana.

Joseph Nyuki.


Mr Nyuki na familia yake.



Muone hapa Mr Nyuki akimtukuza MUNGU katika wimbo sidanganyiki pamoja na acha wewe uitwe MUNGU.









Comments