YESU ANIPONYA NA MAPEPO YA KULA UDONGO


Dada Hawa Lufingo
Mimi namshukuru sana Mungu kwa kuniponya, kabla sijapata mtoto wangu wa kwanza nilikuwa na tabia ya kula udongo pia natafuna sana mchele, hata nilipopata mtoto bado niliendelea kula udongo na mchele, ilifikia hatua sitamani chakula wala hamu ya kula sina nikawa nakula udongo na soda, mchele na chai, hali ilikuja kuwa mbaya sana nilipopata mtoto wa pili nilikuwa naweka chini ya mto mchele na udongo wakati wa kulala usiku naamka kula, ila kuna siku kulikuwa na semina na apostle alifundisha uzao wa nyoka, na mapepo yanavyo watumikisha watu kula mkaa,udongo,mchele, unga wa ugali, na wakati hata nikipaka mafuta napo hayakolei, nilivyoombewa ndo hali ilizidi kuwa mbaya, lakini nilikazana na maombi peke yangu, siku ambayo siijui wala siikumbi nikagundua sijala mchele wala udongo mda mrefu, Yesu alinitoa kwenye kifungo cha shetani, saizi nipo huru, sili tena udongo wala sitafuni tena mchele, namshukulu Mungu kwa neema alinitoa kifungoni, sasa nimenenepa na ngozi yangu ni nzuri, Yesu amenipa mwili mpya, asante Yesu.

Comments