ADUI WA NDOA YAKO


UJUMBE UNATOKA: Warumi 16:19-20
“Maana UTII wenu umewafikilia watu wote; basi nafurahi kwa ajili yenu, lakini nataka ninyi kuwa wenye HEKIMA katika mambo MEMA, na wajinga katika mambo mabaya. NAYE MUNGU WA AMANI ATAMSETA SHETANI CHINI YA MIGUU YENU UPESI…..”

Baada ya kufanya uchunguzi, imebainika kuwa kadri tunavyoendelea kuishi, kati ya ndoa 100, ndoa 95 zinapitia changamoto za Migogoro ambayo mwisho wake ni kuachana, na hata kama hawajapeana talaka, basi wanaishi kwa matumaini. Yaani wanaomba lolote litokee ili waondokane na Adha ya maisha ya Ndoa. Utakuta watu wanatembea Barabarani wanaongea peke yao, au wanafika maofisini wakiwa na MALUWELUWE “Upset Minded”.
Wapendwa kuna adui wa Ndoa yako, anayekuonea wivu unapokula Maraha na mpenzi wako, kila wakati anapanga njama namna ya kulihujumu Penzi lenu – naye ni SHETANI. Hata kama ndoa yako haijawahi kupitia migogoro, jua huyu adui anaipigia mahesabu, siku moja utashangaa mambo yamebadilika, Kitanda cha futi sita kitakuwa kama Mahabusu. Mwingine utasikia ansema, mume wangu siku hizi ni USINIGUSE. Hii ndiyo kazi ya Huyu adui, kuleta huzuni sehemu ya Furaha, kama alivyoleta kwa wazazi wetu wa Kale ADAM na HAWA. Ukiona tatizo limeingia, usihangaike kutafuta mchawi au kumuona mwenzio ni Mbaya, wala usitafute kulipa kisasi – Dawa ni kupeleka shitaka kwa Mungu, Mwenye uwezo wa KUMSETA (TO CRUSH) yaani kumharibu Shetani.
Mama mmoja alikuja analia, macho mekundu, nikamuuliza nini kimemsibu, kumbe mume wake anatembea na shoga yake, na mwishowe akaamua kuhamia kabisa. Nilimpa Dawa ambayo hadi sasa anaisifia, Mume amerudi nyumabani. Nilimwambia – Kwanza amsamehe mume wake, kwani kuna adui aliyesababisha hayo yote – Pili amuombe Mungu Aharibu kazi hizo za Shetani. Baada ya Maombi – Mwanaume kila akienda kucheza MECHI na nyumba ndogo hafanyi kazi, akafikiri amelogwa, akaenda kwa wanganga hadi WAMASAI, nguvu za KI - hazikurudi, akienda kwa mkewe anakuwa na Nguvu kama Simba. Mwishowe akaona hana jinsi, akarudisha majeshi nyumbani, na Mama sasa anakula kwa Raha zake.
Rafiki usitumie nguvu na akili zako kutatua matatizo ya Ndoa yako, salimisha maisha yako kwa Mungu, halafu Mtwishe yeye Fadhaha zako, ana njia maelfu za kukushindia. Shetani si chochote si lolote, ndiyo maana anafanya kila mbinu kututenga na Mungu, anajua tukiwa na Mungu hana uwezo wa nasi – MUNGU WA AMANI ATAMSETA CHINI YA MIGUU YETU UPESI, (GOD WILL BRUISE SATAN UNDER OUR FEET SHORTLY).
MUNGU ATUANGAZIE NURU YA USO WAKE NA KUTUPATIA AMANI TELE
By Faith Kaingu

Comments