IMANI YA KWELI HUONGOZA KWENYE FURAHA YA MILELE

Na Charlotte Lyzik

MAANDIKO Matakatifu yanasema: “mwadilifu—ataishi kwa njia ya imani.” (Waroma 1:17) Maneno hayo yana ahadi nzuri inayokuhusu wewe. Kwa njia gani?
Baada ya kumaliza kazi yake duniani, Yesu, yule Masihi, alipanda mbinguni ili kuwa na Mungu. Wanafunzi wake walipokuwa wakitazama, “akainuliwa na wingu likamchukua juu kutoka machoni pao.” (Matendo 1:9) Akiwa mbinguni, Mungu alimweka rasmi kuwa Mfalme wa mbinguni mwenye nguvu. Hivi karibuni, Yesu, “mwana wa binadamu,” atawasili “katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti chake cha ufalme chenye utukufu. Na mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atawatenganisha watu, mmoja kutoka kwa mwenzake, kama vile mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi.” (Mathayo 25:31, 32) Mambo hayo yatatokea wakati gani?
Maandiko Matakatifu yanatabiri wakati ambapo kungekuwa na taabu ulimwenguni ambayo ingekuwa ishara ya kwamba karibuni Masihi atayahukumu mataifa. Yesu alieleza kile ambacho ishara hiyo ingehusisha: “Taifa litasimama kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; na kutakuwa na matetemeko makubwa ya nchi, na katika mahali pamoja baada ya pengine kutakuwa na tauni na upungufu wa chakula; kutakuwa na mambo yenye kuogopesha.”—Luka 21:7, 10, 11.
Leo, tunaona waziwazi maneno ya Yesu yakitimizwa. Karibuni Yesu atakuja kuwaharibu waovu. Mwishowe, hata Shetani ataharibiwa! Dunia yote itakuwa paradiso. Watu wote wataishi kwa amani hata pamoja na wanyama. “Mbwa-mwitu kwa kweli atakaa pamoja na mwana-kondoo kwa muda fulani, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi, na ndama na mwana-simba mwenye manyoya shingoni na mnyama aliyelishwa vizuri wote pamoja; na mvulana mdogo atakuwa kiongozi juu yao. Hawatasababisha madhara yoyote wala kusababisha uharibifu wowote.” (Isaya 11:6, 9) “Hakuna mkaaji atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’ . . . Wakati huo macho ya vipofu yatafunguliwa, na masikio ya viziwi yatazibuliwa.” (Isaya 33:24; 35:5) Hata wafu watafufuliwa. “Yehova hakika atafuta machozi katika nyuso zote,” na “kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.” (Isaya 25:8; Ufunuo 21:4) Kisha, kusudi la awali la Mungu kuhusu dunia litatimizwa. Hilo ni tumaini zuri kama nini!
IMANI YA KWELI HUONGOZA KWENYE FURAHA YA MILELE
MAANDIKO Matakatifu yanasema: “mwadilifu—ataishi kwa njia ya imani.” (Waroma 1:17) Maneno hayo yana ahadi nzuri inayokuhusu wewe. Kwa njia gani?
Baada ya kumaliza kazi yake duniani, Yesu, yule Masihi, alipanda mbinguni ili kuwa na Mungu. Wanafunzi wake walipokuwa wakitazama, “akainuliwa na wingu likamchukua juu kutoka machoni pao.” (Matendo 1:9) Akiwa mbinguni, Mungu alimweka rasmi kuwa Mfalme wa mbinguni mwenye nguvu. Hivi karibuni, Yesu, “mwana wa binadamu,” atawasili “katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti chake cha ufalme chenye utukufu. Na mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atawatenganisha watu, mmoja kutoka kwa mwenzake, kama vile mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi.” (Mathayo 25:31, 32) Mambo hayo yatatokea wakati gani?
Maandiko Matakatifu yanatabiri wakati ambapo kungekuwa na taabu ulimwenguni ambayo ingekuwa ishara ya kwamba karibuni Masihi atayahukumu mataifa. Yesu alieleza kile ambacho ishara hiyo ingehusisha: “Taifa litasimama kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; na kutakuwa na matetemeko makubwa ya nchi, na katika mahali pamoja baada ya pengine kutakuwa na tauni na upungufu wa chakula; kutakuwa na mambo yenye kuogopesha.”—Luka 21:7, 10, 11.

Leo, tunaona waziwazi maneno ya Yesu yakitimizwa. Karibuni Yesu atakuja kuwaharibu waovu. Mwishowe, hata Shetani ataharibiwa! Dunia yote itakuwa paradiso. Watu wote wataishi kwa amani hata pamoja na wanyama. “Mbwa-mwitu kwa kweli atakaa pamoja na mwana-kondoo kwa muda fulani, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi, na ndama na mwana-simba mwenye manyoya shingoni na mnyama aliyelishwa vizuri wote pamoja; na mvulana mdogo atakuwa kiongozi juu yao. Hawatasababisha madhara yoyote wala kusababisha uharibifu wowote.” (Isaya 11:6, 9) “Hakuna mkaaji atakayesema: ‘Mimi ni mgonjwa.’ . . . Wakati huo macho ya vipofu yatafunguliwa, na masikio ya viziwi yatazibuliwa.” (Isaya 33:24; 35:5) Hata wafu watafufuliwa. “Yehova hakika atafuta machozi katika nyuso zote,” na “kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.” (Isaya 25:8; Ufunuo 21:4) Kisha, kusudi la awali la Mungu kuhusu dunia litatimizwa. Hilo ni tumaini zuri kama nini!
MUNGU akubariki.
By  Charlotte Lyzik

Comments