
BWANA YESU
asifiwe.
Kabla sijaokoka
kuna mama mmoja ambaye alikuwa jirani yetu kule Mwanza, mama huyu alikuwa mimba
ya miezi 8, alikua na tatizo la kuchagua
jina la kumpa mtoto wake kifungua mimba wake ambaye angejifungua wiki 2 baadae,
akaamua kuniuliza jina gani ampe mtoto wake, kwa haraka sana nikasema ukizaa
mtoto wa kiume mpe jina la Frank Yule mama akalipenda jina hilo na kweli
alipozaa akamwita mtoto jina hilo yaani frank, huyo Frank yupo hata leo anasoma
shule ya msingi. Lakini mama huyu hakujua kwanini mimi nilichagua jina la
Frank, hakujua kabisa ila siri nilikuwa
nayo mimi moyoni. Nilipendekeza jina la Frank kwa sababu tu kuna mcheza filamu
wa marekani ambaye nilikua nampenda sana anaitwa Frank Zagarino, Hivyo Frank
huyu wa Tanzania ametokana na Frank Zagarino wa Marekani.
Karibu
tujifunze kitu muhimu sana yaani JINA.
Mithali 22:1
‘’Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi; Na neema kuliko fedha na dhahabu.
‘’
Kila mtu ana
jina lake na jina hilo linabeba kitu kikubwa sana.
Chimbuko ya
neno ‘’jina’’ linatokana na neno la kigiriki liitwalo ‘’Sum’’
‘’Sum’’
maana yake ni ukumbusho au kumbukumbu.
Kutoka 17:14
inasema ‘’ BWANA akamwambia Musa, Andika habari hii katika kitabu iwe ukumbusho,
kisha ihubiri masikioni mwa Yoshua; ya kuwa nitaufuta ukumbusho wa
Amaleki kabisa, usiwe tena chini ya mbingu.
‘’
Ukumbusho au
Sum kama ilivyoandikwa katika Biblia ya kigiriki maana yake ni jina Hivyo
kwenye hilo andiko unaweza kusema kwamba ‘’MUNGU atalifuta jina la Amaleki’’
-Kwa hiyo
maana ya kwanza ya jina/sum ni ukumbusho ambao mtu anapewa.
-Jina/sum
maana yake ni alama ya pekee ambayo anapewa mtu ili kumtofautisha na wengine.
-Jina/sum ni
zawadi ya pekee ambayo mtu anapewa.
Vigezo vya
kumpatia mtu jina hutofautiana.
Majina mengine
huwakilisha heshima ya kipekee.
Wafilipi 2:9-11( Kwa hiyo tena MUNGU alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la YESU kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;
na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa MUNGU Baba.
)
Majina
mengine huwakilisha sifa ya huyo anayepewa jina .
Mfano rais wanchi
ni jina la sifa ambalo anapewa mhusika.
Majina
mengine ni kuonyesha mamlaka mfano Askari ni jina ambalo linaonyesha mamlaka.
Kwa sababu
ya tabia Fulani Fulani baadhi ya majina hutokea.
Mfano
mwingine JEHOVAH SHALOM maana yake MUNGU ni mani yetu hili ni jina jema ambalo
linatokana na sifa ya MUNGU katika kuleta amani kwa watu wake.
Mfano Paka
amepewa jina la Nyau kwa sababu tu ya kulia nyauuuuu.
Kuna mtu
anaitwa Chausiku na jina hilo alilipata baada tu ya kuzaliwa usiku.
Mimi sijui
wewe unaitwa nani na jina lako linatokana na nini. Maana majina yanabeba jambo
kubwa sana kwa mhusika.
Mfano mtu
mchafu anaweza kupewa jina kutokana na uchafu wake ni jina hilo likamshika na
kushika maisha ya mtu husika huyo.
Hata mpole
anaweza kupewa jina kwa sababu tu ya upole wake, je jina lako ni nani? Na linatokana
na nini, je jina lako linatokana na kitu chema au kibaya?
Je jina lako
limebeba Baraka? Au laana?
Mfano hai ni
hivi Mimi naitwa PETER MICHAEL MABULA.
Maana ya
majina yangu ni hii;
-Peter maana yake mwamba au jiwe Yohana 1:42.
Kumbuka pia
BWANA YESU alimwambia mtume Petro kwamba ‘’ Juu ya Mwamba huu nitalijenga kanisa langu
na wala milango ya kuzimu haitaliweza.’’ Mwamba ni maana ya Peter lakini hapa BWANA YESU alikuwa
anazungumzia mitume wote yaani juu ya mitume injili ya KRISTO itasonga mbele na
ndio maana Imani yetu imejengwa juu ya mitume na manabii’.
-Michael
maana yake ‘’Ni nani aliye kama MUNGU?’’
-Mabula ni
jina la kisukuma ambalo maana yake ni ‘’mtoto wa kiume aliyezaliwa wakati wa
mvua.’’
Mabula
inatokana na mbula kwa kisukuma ambapo mbula maana yake mvua, hivyo mtoto wa
kiume akizaliwa wakati wa mvua anaweza akaitwa Mabula na majina haya ni mengi
sana usukumani yaani Mwanza kwetu, na kama mtoto akizaliwa wa kike wakati wa
mvua huitwa Kabula ikiwa na maana sawa na Mabula ila tu Mabula ni wa kiume na
Kabula ni wa kike.
Je jina lako
ni nani?
Je jina lako
limebeba nini?
Limebeba uzima
au mikosi, limebeba Baraka au lina maagano na mashetani?
Kwa msaada tu kama utapenda kujua maana ya
jina lako fungua Blog yangu ya Maisha ya
ushindi na kwenye Research/ Tafuta
andika maneno haya ‘’MAJINA NA MAANA ZAKE’’ Utaona majina zaidi ya 200 na maana
zake. Ubarikiwe na tunaendelea na somo.
Kwa hiyo mtu
anaweza kupewa jina kulingana na cheo au sifa.
AINA KUU 2
ZA MAJINA.
1.
Jina
ambalo mtu anapewa na wazazi wake au jina la Asili.
2.
Jina
kutoka nje ya familia kutokana na sifa za mtu huyo.
Mfano kuna
watu wanaitwa ‘’Kahaba’’ au ‘’Mwizi’’ hayo ni majina ila yanatokana na tabia.
Je jina lako
ni nani?
Tafakari
jina lako je umelipataje?
Je jina lako linatokana na nini?
Ni muhimu
sana kujua maana ya jina lako na chanzo chake maana jina linaweza kubeba laana
au Baraka.
Kuna majina
hutokana na ukoo au kabila, haya ni ya kuchunga sana maana koo zetu nyingi
hawajaokoka hivyo ni rahisi sana kupewa jina ambalo lina maagano na mizimu na
kukupelekea kupata majanga maishani.
Luka 1:59-61”
Ikawa siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto; wakataka kumpa jina la babaye, Zakaria.
Mamaye akajibu akasema La, sivyo; bali, ataitwa Yohana.
Wakamwambia, Hapana mtu katika jamaa zako aitwaye jina hilo.
“
Kwenye hayo
maandiko juu Unaweza kujiuliza kwanini MUNGU aliamua kutoa jina kwa Yohana
mbatizaji? Huku ndugu wakitaka jina la
ukoo?
MUNGU alijua
kabisa kwamba jina hilo la ukoo lisingeweza kulitimiza kusudi lake.
Kumbe kuna
majina hayawezi kutimiza makusudi ya MUNGU. Ndio maana kuna kuokoka, pia ndio
maana kuna ubatizo ili tu kuzika utu wa kale na maagano ya ukoo na mizimu na
kabila ambao mengine hutokana na maagano
ya kishetani.
Wazazi na
wale ambao mtakuwa wazazi baadaye nawaombeni mliangalie sana jambo hili yaani
jina ambalo mtampa mtoto wenu.
Sio vizuri
kuiga jina.
Nampenda
sana BWANA YESU maana jina YESU maana yake ni ‘’Mtu mwenye kuokoa’’
Wapo watu
wengi kutokana na majina yao wameshindwa kutimiza kusudi la MUNGU.
Ibrahimu
kabla hajaitwa hivyo aliitwa Abram, MUNGU aliona Abram haiwezi kulitimiza
kusudi lake ndio maana akambadili jina la kumwita Ibrahimu. Mwanzo 17:5 (wala jina lako hutaitwa tena Abramu, lakini jina lako litakuwa Ibrahimu, kwani nimekuweka uwe baba wa mataifa mengi.
)
Hata Sara
mwanzo aliitwa Sarai, MUNGU akambadilishia jina na kumwita Sara ambalo maana
yake ni ‘’Binti mfalme’’ Mwanzo 17:15 (MUNGU akamwambia Ibrahimu, Sarai mkeo, hutamwita jina lake Sarai, kwa kuwa jina lake litakuwa Sara ).
Je unauona
umuhimu wa jina?
Yakobo
haikuwepo kwenye mikakati ya MUNGU ndio maana akaitwa Israeli.
Ndugu yangu
nakuomba usipokee tu jina mradi ni jina.
Mwanzo 41:45
( Farao akamwita Yusufu, Safenath-panea; akamwoza Asenathi, binti Potifera,
kuhani wa Oni, kuwa mkewe Yusufu akaenda huko na huko katika nchi yote
ya Misri.
)
Hapa Farao alimpa jina jipya Yusufu lakini jina hilo halikufanya kazi na likafutika maana Yusufu ilikuwa jina linalotimiza kusudi la MUNGU.
Hesabu 13:16
( Hayo ndiyo majina ya hao watu waliotumwa na Musa waende kuipeleleza
nchi. Na huyo Hoshea mwana wa Nuni, Musa akamwita jina lake Yoshua.
)
Hapa jina Hoshea halikuwa linatimiza kusudi ndio maana akaitwa Yoshua maana
yake mkombozi.
Kuna watu
wamerithi majina na majina hayo
yanawatesa sasa.
Wapo waliorithi majina ya bibi zao walikuwa
wanasumbuliwa na magonjwa Fulani, lakini licha ya kupita miaka mingi kwa sasa
wajukuu zao waliorithi majina hayo, wanasumbuliwa na magonjwa yale yale
yaliyowatesa hadi kuwaua bibi zao.
Wewe Mzazi
nakusihi; Mpe mwanao jina linalomtukuza MUNGU.
Mithali 18:21
( Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake.
)
Hata MUNGU
aliumba kwa kutamka hivyo kuna nguvu katika kutamka. Hivyo wewe unayeitwa sura
mbaya, hao watu wanaokuita hivyo wanakuumbia sura mbaya , hakika utakuwa sura
mbaya na hakuna atakayetaka kukuoa sura mbaya.
Tafuta maana
ya jina lako.
Inawezekana
jina lako linatengeneza Baraka au laana.
Na kama jina
lako lina maagano ya kiukoo au kikabila, au jina lako limekusababishia mabaya
kila siku dawa yake ni kuokoka tu maana
Biblia inasema katika 2 Kor 5 :17 kwamba ‘’ Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya KRISTO amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.
‘’
Wengine
wanafilisika kwa sababu tu majina yao yanawafilisi.
Mithali 22:1
‘’Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi; Na neema kuliko fedha na dhahabu.
‘’
Usikubali
jina lililo na maagano ya mababu, wala usikubali jina leye ushetani ndani yake.
1 Samweli
25:25 (Nakusihi, bwana wangu, wewe usimwangalie huyu mtu asiyefaa, yaani,
Nabali; kwa maana kama lilivyo jina lake ndivyo alivyo yeye; jina lake
ndilo Nabali, na upumbavu anao; lakini mimi, mjakazi wako, sikuwaona hao
vijana wa bwana wangu aliowatuma.
)
Nabali maana
yake ni mpumbavu.
Sasa kama
jina lako wewe ni mpumbavu je upumbavu utakaa mbali na wewe?
Wewe mzazi
ni vizuri ukaangalia jina Zuri kwenye Biblia ili kumpa mtoto wako.
Mwite mtoto
wako jina linaloleta utukufu kwa MUNGU.
Yawezekana
hujaokoka na ndio maana unaitwa ‘’Mwenye dhambi’’ Hivyo ni vyema kufuta jina
hilo kwa kuokoka.
Yohana 1:12-13 ‘’
Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa MUNGU, ndio wale waliaminio jina lake;
13 waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa MUNGU. ‘’
13 waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa MUNGU. ‘’
Comments