Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova |
Watuhumiwa hao wawili wanadaiwa kuwa, Juni 23,
mwaka huu walifanya mauaji ya Sista huyo eneo la Riverside, Ubungo, Dar
es Salaam na kupora kiasi cha Sh20 milioni na nyaraka mbalimbali.
Katika tukio jingine la Aprili 15, mwaka huu watuhumiwa wengine wanadaiwa kupora Sh500 milioni za benki ya Barclays.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam,
Suleiman Kova alisema majambazi hao walikamatwa kutokana na operesheni
kali inayoendelea jijini hasa baada ya kifo cha sista huyo.
Kamanda Kova alisema watuhumiwa waliokamatwa
kuhusiana na mauaji ya mtawa huyo wa Kanisa Katoliki, mmoja alikuwa
akiendesha bodaboda na alimbeba jambazi mwenzake akiwa na fuko la
mamilioni ya fedha na kutoroka nalo wakati mtuhumiwa wa pili
aliyekamatwa ambaye ni mfanyabiashara, ndiye aliyekuwa kiongozi katika
tukio hilo.
Kova alisema polisi bado inawatafuta watuhumiwa wengine wawili.
Comments