
BWANA YESU
asifiwe ndugu yangu.
Karibu
tujifunze somo hili ambalo MUNGU anataka tujue Matokeo ya Neno lake kama
likikaa kwa wingi ndani yetu.
Yohana
8:31-32 inasema ‘’Basi YESU akawaambia wale wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa
katika neno langu, mmekuwa wanafunzi
wangu kwelikweli tena mtaifahamu kweli nayo hiyo kweli itawaweka huru.’’
-
-Huwezi
huwezi kuwekwa huru pasipo kweli.
-
-Neno
la MUNGU linaweka huru.
-
-Tamani
neno ambalo halijaghoshiwa.
-
-Watu
hutenda dhambi kwa sababu kweli/Neno la MUNGU halimo ndani yao kwa wingi.
Katika Ayubu 22:21-22 Biblia inatufundisha jambo kubwa sana
inasema ‘’ Mjue sana MUNGU ili uwe na amani, Ndivyo mema yatakavyokujia,
Uyapokee tafadhali Mafunzo yatokayo kinywani mwake. Na maneno yake yaweke
moyoni mwako.''
Hapa Biblia inatupa sababu za kumwamini MUNGU na pia sababu
za kuyaweka maagizo yake yaani neno lake mioyoni mwetu.
Siku moja BWANA YESU alikuwa anatembea na wanafunzi njiani
akaulaani mtu, wanafunzi wake wakashtuka sana na kwa sababu neno lake lilikuwa
halijawakaa ipasavyo maana imani yao ilikuwa bado ndogo walihoji juu ya jambo
hilo, BWANA YESU yeye aliwajibu kwamba ‘’Mwaminini MUNGU’’. Kumwamini MUNGU ni
kitu muhimu sana na MUNGU analiangalia neno lake ili alitimize, itatuchanganya
sana kama neno lake MUNGU tutakuwa hatulieweli.
KWANINI NENO LIMEBEBA HATIMA YAKO?
Ni kwa sababu MUNGU huliangalia neno lake ili atende jambo Fulani,
na ili afanye kitu chochote kwetu huliangalia neno lake ambalo alikwishalitoa.
Isaya 55:11 MUNGU BABA anasema ‘’Ndivyo litakavyokuwa neno
langu, litokalo katika kinywa changu halitanirudia bure, bali litatimiza
mapenzi yangu, nalo litafanikiwa sana katika mambo yale niliyolituma.''
-MUNGU atahukumu kwa neno.
-MUNGU atabariki kwa neno.
-Atasamehe dhambi kwa neno N.k
KINACHOFANYWA NA NENO LA MUNGU LIKIKAA KWA WINGI MOYONI
MWAKO.
1.
Neno
litakufanya usitende dhambi.
Zaburi 119:11 (Moyoni
mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi. ).
2.
Neno
litakufanya ujue hila za shetani.
2 Kor 2:11 ( shetani asije akapata kutushinda
kwa maana hatukosi kuzijua fikra zake.)
3.
Neno
hukutambulisha wewe ni nani na pia litakufanya ujijue wewe ni nani.
Yohana
1:19-22(Na huu ndio ushuhuda wake Yohana, Wayahudi walipotuma kwake makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamwulize, Wewe u nani?
Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye KRISTO.
Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La. Basi wakamwambia, U nani? Tuwape majibu wale waliotupeleka. Wanenaje juu ya nafsi yako?
).
4.
Neno
hutakasa na kukufanya hai zaidi kiroho.
Yohana 17:17 ( Uwatakase kwa ile kweli,
neno lako ndio kweli.)
5.
Neno la MUNGU huleta tabia ya uungu.
Zaburi
125:1 (Wamtumainio BWANA ni kama mlima sayuni ambao hautatikisika milele).
MUNGU hatikisiki na mwenye neno lake hatikisiki. Utadumu maana uko katika kweli ya MUNGU.
6.
Neno litakufanya kujua mpango wa MUNGU kwako
Kumbukumbu 2:24 ( Ondokeni mshike njia……. Tazama nimewapa nchi hii muimiliki, anzeni
kuimiliki,Mshindane nae katika mapigano)
7.
Neno la MUNGU litakufanya uwe na kiwango
kikubwa cha imani. Yohana 20:5-16 ( Akainama na kuchungulia, akaona vitambaa vya sanda vimelala; lakini hakuingia.
6 Basi akaja na Simoni Petro, akaingia ndani ya kaburi; akavitazama vitambaa vilivyolala,
7 na ile leso iliyokuwako kichwani pake; haikulala pamoja na vitambaa, bali imezongwa-zongwa mbali mahali pa peke yake.
8 Basi ndipo alipoingia naye yule mwanafunzi mwingine aliyekuwa wa kwanza wa kufika kaburini, akaona na kuamini.
9 Kwa maana hawajalifahamu bado andiko, ya kwamba imempasa kufufuka.
10 Basi wale wanafunzi wakaenda zao tena nyumbani kwao.
11 Lakini Mariamu alikuwa akisimama karibu na kaburi, nje yake, analia. Basi akilia hivi, aliinama na kuchungulia ndani ya kaburi.
12 Akaona malaika wawili, wenye mavazi meupe, wameketi, mmoja kichwani na mmoja miguuni, hapo ulipolazwa mwili wake Yesu.
13 Nao wakamwambia, Mama, unalilia nini? Akawaambia, Kwa sababu wamemwondoa Bwana wangu, wala mimi sijui walikomweka.
14 Naye akiisha kusema hayo, akageuka nyuma, akamwona Yesu amesimama, asijue ya kuwa ni Yesu.
15 Yesu akamwambia, Mama, unalilia nini? Unamtafuta nani? Naye, huku akidhania ya kuwa ni mtunza bustani, akamwambia, Bwana, ikiwa umemchukua wewe, uniambie ulipomweka, nami nitamwondoa.
16 Yesu akamwambia, Mariamu. Yeye akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, Raboni! (Yaani, Mwalimu wangu). )
6 Basi akaja na Simoni Petro, akaingia ndani ya kaburi; akavitazama vitambaa vilivyolala,
7 na ile leso iliyokuwako kichwani pake; haikulala pamoja na vitambaa, bali imezongwa-zongwa mbali mahali pa peke yake.
8 Basi ndipo alipoingia naye yule mwanafunzi mwingine aliyekuwa wa kwanza wa kufika kaburini, akaona na kuamini.
9 Kwa maana hawajalifahamu bado andiko, ya kwamba imempasa kufufuka.
10 Basi wale wanafunzi wakaenda zao tena nyumbani kwao.
11 Lakini Mariamu alikuwa akisimama karibu na kaburi, nje yake, analia. Basi akilia hivi, aliinama na kuchungulia ndani ya kaburi.
12 Akaona malaika wawili, wenye mavazi meupe, wameketi, mmoja kichwani na mmoja miguuni, hapo ulipolazwa mwili wake Yesu.
13 Nao wakamwambia, Mama, unalilia nini? Akawaambia, Kwa sababu wamemwondoa Bwana wangu, wala mimi sijui walikomweka.
14 Naye akiisha kusema hayo, akageuka nyuma, akamwona Yesu amesimama, asijue ya kuwa ni Yesu.
15 Yesu akamwambia, Mama, unalilia nini? Unamtafuta nani? Naye, huku akidhania ya kuwa ni mtunza bustani, akamwambia, Bwana, ikiwa umemchukua wewe, uniambie ulipomweka, nami nitamwondoa.
16 Yesu akamwambia, Mariamu. Yeye akageuka, akamwambia kwa Kiebrania, Raboni! (Yaani, Mwalimu wangu). )
-Kiwango kidogo cha imani ni
tatizo.
Wa kwanza akaona sanda.
Wa pili akaona sanda na
leso.
Wa tatu akamwona YESU.
Wa imani akangoja na hatimaye akamwona BWANA.
Neno la
MUNGU lingekuwa limewakaa wana wa Israeli wakati wakitoka misri naamini
wasingeabudu ndama maana neno lingekuwa sababu yao ya kutokuabudu chochote
zaidi ya MUNGU aliye hai, na hata kama mmoja wao angeshawishi wale wengine
wasingelimsikiliza, hata Haruni angekuwa na ufahamu mzuri wa neno la MUNGU
naamini angekataa kuwatengenezea ndama watu wale.
Comments