Usidharau Ndoto Unaoyoota. Miaka Michache Iliyopita Niliota Ndoto Ambayo Ilikuwa Ikijirudia Rudia, Niliona Fuvu La Mwanadamu Likiwa Na Mifupa Yake Yote Likitembea yaani Skeleton , Alikua Ni Mtu Kamili Ila Hana Nyama Zote Kwenye Mwili Wake, Nilianza Kuwaombea Ndugu Zangu Niliowapenda Nikijua Kuna 1 Wao Nisiyemjua Atakua Anaumwa, Nilijua Yule Fuvu Ni Mtu Ambaye Namfahamu, Ambaye Natakiwa Kumsaidia, Ndoto Hiyo Ilijirudia Kila Mara Huku Mimi Nikidhani Sio Mimi, Ndipo Jioni Moja Pastor Wangu Akaambiwa Na MUNGU Live Maana Ya Ndoto Yangu Hata Bila Kumwambia Mimi, Niliogopa Sana Maana Nilifahamu Hakuna Ajuaye Ndoto Niliyoota,
Nilijiona hivi kwenye ndoto. |
Uwe Mwangalifu Pale Unapoota Ndoto Maana Ndoto Ni Mwongozo. MUNGU Analinda Kila Kilicho Chako Katika Dunia Hii, Ili Shetani Na Malaika Zake Waovu Wasije Kuharibu Kile MUNGU Ameweka Mbele Yako. Fikiria Kuhusu Farao Mfalme Wa Misri. Ingekuwa Vipi Kama MUNGU Asingemletea Ndoto? Wangekufa Kwa Njaa Karibu Nchi Nzima, Ingekuwaje Kama MUNGU Asingemfanya Yusufu Kuwa Muotaji Na Mfasiri Wa Ndoto? Pengine Angefia Gerezani, Vipi Kama MUNGU Asingempa Ndoto Yusufu, Si angekuwa Amemwacha Bikra Maria? Ndoto Zina Nguvu Na Kwa Jinsi Hiyo MUNGU Huwasiliana Na Watu Kwa Njia Ya Picha Au Maneno.
Comments