Mifupa bila nyama kwenye ndoto.


Usidharau Ndoto Unaoyoota. Miaka Michache Iliyopita Niliota Ndoto Ambayo Ilikuwa Ikijirudia Rudia, Niliona Fuvu La Mwanadamu Likiwa Na Mifupa Yake Yote Likitembea yaani Skeleton ,  Alikua Ni Mtu Kamili Ila Hana Nyama Zote Kwenye Mwili Wake, Nilianza Kuwaombea Ndugu Zangu Niliowapenda Nikijua Kuna 1 Wao Nisiyemjua Atakua Anaumwa, Nilijua Yule Fuvu Ni Mtu Ambaye Namfahamu, Ambaye Natakiwa Kumsaidia, Ndoto Hiyo Ilijirudia Kila Mara Huku Mimi Nikidhani Sio Mimi, Ndipo Jioni Moja Pastor Wangu Akaambiwa Na MUNGU Live Maana Ya Ndoto Yangu Hata Bila Kumwambia Mimi, Niliogopa Sana Maana Nilifahamu Hakuna Ajuaye Ndoto Niliyoota,
skeleton photo: Skeleton Skeleton_3575.jpg
Nilijiona hivi kwenye ndoto.
Akaniambia " Peter kuna Ndoto Umeiota, Na Umeidharau, Umeota Umekuwa Fuvu, Hata Ukitembea Unakua Ni Mifupa Mikavu Tu" Nikasema Ni Kweli, Akaniambia Ndoto Hiyo Maana Yake "Siku Hizi Huna Nguvu Za Kiroho,Umezikwa Ukiwa Hai,MUNGU Kwako Ni Ziada tu, Hapo MUNGU Anakuonya" Niliogopa Sana Na Tangu Siku Hiyo Nikakaa Sawa Kwa MUNGU, Na Ndio Maana Baadhi Ya Ndoto Ninazofahamu Maana Zake Nakuletea Hapa Ili Ujue Uombeje. Usidharau ndoto unayoota ndugu yangu maana ndoto ni msimamo wako wa Rohoni, pia ndoto ni matukio ambayo hutokea kwanza Rohoni na wewe ukicheza matukio hayo huja kudhihirika kwenye ulimwengu wa Mwili.

 Uwe Mwangalifu Pale Unapoota Ndoto Maana Ndoto Ni Mwongozo. MUNGU Analinda Kila Kilicho Chako Katika Dunia Hii, Ili Shetani Na Malaika Zake Waovu Wasije Kuharibu Kile MUNGU Ameweka Mbele Yako. Fikiria Kuhusu Farao Mfalme Wa Misri. Ingekuwa Vipi Kama MUNGU Asingemletea Ndoto? Wangekufa Kwa Njaa Karibu Nchi Nzima, Ingekuwaje Kama MUNGU Asingemfanya Yusufu Kuwa Muotaji Na Mfasiri Wa Ndoto? Pengine Angefia Gerezani, Vipi Kama MUNGU Asingempa Ndoto Yusufu, Si angekuwa Amemwacha Bikra Maria? Ndoto Zina Nguvu Na Kwa Jinsi Hiyo MUNGU Huwasiliana Na Watu Kwa Njia Ya Picha Au Maneno.
Kwa sasa naishia hapo, MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani aliko KRISTO BWANA.
                     MUNGU akubariki sana .
                      Ni mimi ndugu yako
                       Peter M Mabula
                 Maisha ya Ushindi Ministry.

                     mabula1986@gmail.com
                 MUNGU akubariki sana uliyesoma somo hili.

Comments