
BWANA YESU
asifiwe.
Karibu tena
katika ujumbe huu ambao MUNGU amenipa kwa ajili ya kila mwanadamu kujua.
Katika
maisha ya mwanadamu yeyote kuna njia mbili
ambapo moja kati ya hizo kila mwanadamu anapita.
Kila njia
ina matokeo yake na kila mwisho wa kila
mwanadamu huenda katika hitimisho la
mojawapo ya njia hizi mbili.
Kuna njia ya
uzima wa milele na kuna njia ya jehanamu ya milele.
Mathayo
7:13-14 ( Ingieni kwa kupitia mlango ulio
mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao
ni wengi waingiao kwa mlango huo.
Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache.
)
Hapa unapata
njia mbili.
Kuna njia ya WOKOVU WA MILELE.
FURAHA YA MILELE.
UTUKUFU WA MILELE.
Pia kuna njia ya MATESO YA MILELE.
UPOTEVU WA MILELE.
KILIO CHA MILELE.
Kila mtu
mwisho wake ni katika mojawapo ya njia hizi.
Njia pana
ambayo ni njia ya jehanamu ni njia ambayo huonekana kwa urahisi sana, ni njia
ya dhambi za kila aina, ni njia ya wazinzi, ni njia ya walevi, ni njia ya
waasherati, ni njia ya waongo, ni njia ya waabudu sanamu, ni njia ya
freemasoni, ni njia ya wachawi, ni njia ya wala rushwa ni njia ambao hapa
duniani inaonekana kama njia ya kuwafanya wanadamu waishi kwa starehe ya muda
mfupi sana kama miaka 80 tu lakini wanadamu hawa hawa wanasahau furaha ya
milele ambayo inapatikana katika KRISTO YESU pekee.

NJIA YA UZIMA.
Luka 13:24 ( Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.
).
Wengi
watataka kukingia lakini hawataweza maana watakuwa wamechelewa sana.
Lango la
mbinguni likifungwa wote wali nje watataka kuingia lakini hawataweza.
Ni wachache
hata leo wanaoiona njia hii ya uzima Yohana 10:7-9 ( Basi YESU aliwaambia tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo.
Wote walionitangulia ni wevi na wanyang'anyi; lakini kondoo hawakuwasikia.
Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho.
).
Ndugu yangu
tunamhitaji YESU ili tupone.
Tunamhitaji
BWANA YESU ili tuingie uzimani.
Tunamhitaji
YESU KRISTO ili tukafurahi milele.
YESU ndio
hiyo njia ya uzima wa milele (Yohana 14:6-YESU akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa BABA, ila kwa njia ya mimi.
).
Hakuna
mwingine ambaye kupitia kwake tunaweza kuupata uzima wa milele , Matendo 4:12 (Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina
jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa
kwalo.
)
NJIA
YA MOTO WA MILELE.
Waefeso 2:1-3 (Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;
ambazo mliziendea zamani kwa
kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa
anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi;
ambao zamani, sisi sote nasi
tulienenda kati yao, katika tamaa za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi
ya mwili na ya nia, tukawa kwa tabia yetu watoto wa hasira kama na hao
wengine.
)
YESU kuwa BWANA na MWOKOZI wa maisha yako.Wateule
wngi ambao kwa sasa wako katika njia ya uzima, zamani wote walikuwa
katika njia ya jehanamu, na Biblia inafundisha kwamba ni marufuku kurudi
nyuma tena , yaani kataa kurudi kwenye njia pana ,njia ya upotevuni ,
njia ya maangamizi maana wewe mteule sasa uko mahali salama maana
umempokea
Mathao 7:13
( Ingieni kwa kupitia mlango ulio
mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao
ni wengi waingiao kwa mlango huo. )
Huu ni upendo wa ajabu ambao MUNGU ametupenda yaani kutuletea ukombozi wa roho na miili yetu kupitia YESU KRISTO BWANA wetu, Ndugu zangu kila mmoja ajitahiti kupita katika mlango mwembamba.
Mathayo
19:24 ( Nawaambia tena, Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa MUNGU).
MUNGU hataki
yeyote kati yetu aende njia hii ya jehanamu.
Ndugu yangu
unayesoma ujumbe huu, mbele yako kuna UZIMA na MAUTI nakushauri chagua UZIMA kwa kumpokea BWANA
YESU leo.
Mbele yako kuna BARAKA na LAANA
chagua BARAKA yaani kumpokea BWANA YESU leo.

Naamini
baada ya kusoma ujumbe huu umechagua kabisa njia ya kupita ukiwa duniani yaani
kuishi huku ukiwa na YESU mwenye uzima na kukataa dhambi zote. Mimi naamini
umechagua UZIMA.
Comments