Na Nabii Samson Mboya kutoka Geita Piga simu 0756 809209ushauri na maombezi |
Utangulizi:
Ukitaka Mema katika maisha
yako basi anza wewe kufanya mema kwanza
usitake kuvuna katika shamba ambalo hujalipanda kitu, ukitaka Baraka
anza kubariki wengine kwanza, ukitaka heshima
heshimu wengine, ukitaka kupendwa penda wengine ukitaka kuongelewa
vizuri na wengine ongelea wengine vizuri
kwanza, kila jambo unalo litaka katika Maisha yako funguo za kufungua au kufunga unazo wewe
mwenyewe,
Maandiko Matakatifu yanaongelea nini juu ya funguo
hizo,
Mathayo 16:19 Nitakupa funguo za Ufalme
wa mbinguni; kila utakachofunga duniani, kitafungwa pia
mbinguni; kila utakachofungua duniani, kitafunguliwa pia mbinguni."
Bila ya kupewa funguo yaani uwezo mpya katika
kinywa chako huwezi kufunguwa au kufunga chochote katika hii Dunia ,
Unaweza ukawa huru lakini
,usiwe na uwezo wa kufunguwa au kufunga
chochote ukisha zaliwa mara ya
pili fahamu kuwa katika ulimi wako unawekwa uwezo wa kufunga na kufunguwa
chochote kile unachokitaka hata uzima na mauti,
Mithali 18:21 Mauti na uzima huwa katika
uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake
Ø Hatari
ya kutochunga Ulimi
Ø Usipo chunga ulimi wako Unaweza ukashiba mauti/ukafa ki-mwili na ki-roho
Ø Usipo chunga ulimi wako unaweza ukauwa wengine
Ø Usipochunga ulimi wako unaweza ukawanyima wengine Mbingu
Ø Usipochunga ulimi wako unaweza ukauwa huduma za wengine ki-mwili na
kiroho
Ø Usipichunga ulimi wako unaweza ukanajisi maisha yako bila wewe kujuwa
Ø Usipochunga ulimi unaweza ukayakoroga maisha yako
Ø Usipochunga Ulimi wako unaweza ukaharibu kipaji/zawadi yako
Ø Usipochunga ulimi wako unaweza ukajilaani bila kujuwa
Ø Usipochunga ulimi wako unaweza kujifunga wewe mwenyewe bila kujuwa,
Chunguza nini umejitamkia
katika maisha yako au katika maisha ya mwezako kile unapanda tarajia kuvuna,
hicho hicho, kumbuka laana na baraka zinapitia katika kinywa, chunga ulimi
wako,
Yakobo 3:10 Maneno ya laana na ya kusifia hutoka katika kinywa
kimoja. Ndugu zangu, mambo haya hayapaswi kuwa hivyo.
Nitakupa funguo za Ufalme wa
mbinguni; kila utakachofunga duniani, kitafungwa pia mbinguni; kila
utakachofungua duniani, kitafunguliwapia mbinguni."
Mathayo 16 : 19
Mathayo 16 : 19
Usipokuwa makini na Ulimi wako huwezi kupewa uwezo wa
kufungua au kufunga kwakuwa utafunga visivyo fungwa na utafunguwa
visivyofunguliwa na hii ni moja wapo ya
sababu ya wewe wengine kila siku hawaoni mabadiliko kwakuwa hawatumii ulimi
sahihi
Usipokuwa na Neno la Mungu ndani moyo wako na wewe
ukataka kunena yaliyoakilini mwako unaweza ukajitengenezea aibu, ambayo kuifuta
itakugarimu sana,au isiondoke kabisa, si lazima kila unachokiona nilazima ukiongelee au si kila unachokisikia lazima
ukiongelee, ukimya nao ni majibu pia
Tito 2:7 katika mambo yote ukijionyesha wewe
mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na katika mafundisho yako ukionyesha
usahihi na ustahivu,
8 na maneno yenye uzima yasiyoweza kuhukumiwa makosa, ili yule mwenye kupinga atahayarike, kwa kuwa hana neno baya la kunena juu yetu.
8 na maneno yenye uzima yasiyoweza kuhukumiwa makosa, ili yule mwenye kupinga atahayarike, kwa kuwa hana neno baya la kunena juu yetu.
Kila unalofanya uwe mfano wa
kuigwa kwa wengine ukiongea Neno kila
mmoja alitamani kulitumia ,katika mafundisho yako ukionyesha usahihi na
ustahivu, usiwe mwepesi wa kuongea uwe mwepesi wakusikia lakini mzito wa
kuongea, siyo unakuwa mwepesi hadi unajikwaa unamkosea Mungu
Chunga ulimi wako juu ya kile unachotakakukisema kwakuwa fahamu
unapanda sasa katika kupanda kaguwa unapanda nini, maana subiri kuvuna baada ya
kupanda,
Mathayo 12:22H apo
watu wakamletea Yesu kipofu mmoja ambaye alikuwa bubu
kwa sababu alikuwa amepagawa na pepo. Yesu akamponya hata, akaweza kusemana
kuona.
ulimi unatumika sana na Mungu kufanya mapenzi ya Mungu na Mapepo yanataka
sana kutumia kinywa hicho hicho kuwa na Maneno mengi sana yasiyo ya ki-Mungu
ni Roho ya mapepo inakuwa inamtumikisha mtu kuongea Dawa ni kumuombea sala ya
toba,
Markop 9:17 Hapo mtu mmoja katika ule umati wa watu akamjibu,
"Mwalimu, nimemleta mwanangu kwako, ana pepo aliyemfanya kuwa bubu.
Ukiona huwezi kushuhudia hata neno mmoja kwamba umeokoka
au Mungu amekutendea nini, fahamu wewe ni utakuwa na roho inayokuzuwia kunena,
kwakuwa utamwaibisha shetani na yeye hataki aibuna hii ni sababu mmoja wapo Mtu
anapozaliwa maya ya pili awali anakuwa moto sana baada na kitambo anajikuta
kimywa kabisa sababu nini? Amevamiwa akabigwa na ububu,
Luka 1:20 Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu
huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayoniliyokuambia
yatakapotimia."
Upo wakati Mungu anaweza kukunyamazisha kwa sababu
maalumu anazozijuwa yeye unaweza ukaenda
maeneoflani Mungu akakuzuwia kuongea kabisa hata ukijilazimisha unashindwa,
kama anavyoweza kukulazimisha useme Neno mahalifulani ulipo,
1 Wakoritho 14:9Hali kadhalika na ninyi, kama ulimi
wenu hausemi kitu chenye kueleweka, nani ataweza kufahamu mnayosema? Maneno
yenu yatapotea hewani.
Kunawatu kutwa nzima
nikupoteza tu chunga ulimi wako usijeukapotesa hewani maneno,
Yakobo 1:26 Kama mtu akijiona kuwa ni mtu mwenye dini, lakini hawezi kuutawala ulimi wake, dini yake haifai kitu, na anajidanganya mwenyewe.
Yakobo 3:5 Vivyo
hivyo, ulimi, ingawa ni kiungo kidogo cha mwili, hujisifia makuu sana. ic Moto
mdogo waweza kuteketeza msitu mkubwa.
Yakobo 3;6 Hali
kadhalika ulimi ni kama moto. Umejaa maovu chungu nzima, unayo nafasi yake
katika miili yetu na hueneza ubaya katika nafsi zetu zote.Huteketeza maisha
yetu yote kwa moto utokao Jehanamu kwenyewe.
Lakini hakuna
mtu aliyeweza kuufuga ulimi. Ulimi ni kitu kiovu, hakitawaliki, na kimejaa sumu
inayoua.
Yakobo 3 : 8
Yakobo 3 : 8
Kwa ulimi sisi twamshukuru Bwana na Baba yetu. Kwa ulimi huohuo twawalaani watu, watu ambao wameumbwa kwa mfano wa Mungu.
Yakobo 3 : 9
Zaburi ya
119:11 Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.
Kile kilichomjaa mtu moyoni ndicho anakinena hivyo kumfahamu huyu nimtu wa namna gani ni
Rahisi sana kupitia ulimi anajitambulisha ndani ya mtu kukiwa na uzima atanena
uzima kukiwa na mauti atanena mauti,
Maombi
Mathayo 3:8 Basi zaeni matunda yapasayo toba;
Matendo
ya mitume 11:18 Waliposikia maneno haya wakanyamaza, wakamtukuza Mungu,
wakisema, Basi, Mungu amewajalia hata mataifa nao toba
liletalo uzima.
Anza kumtamkia mema yule uliyekuwa umemsababisia matatizo kwa ulimi wako wengine uliwakwaza ,ukawaua ki-Roho na kimwili omba sasa,
Anza kumtamkia mema yule uliyekuwa umemsababisia matatizo kwa ulimi wako wengine uliwakwaza ,ukawaua ki-Roho na kimwili omba sasa,
Comments