BWANA YESU
asifiwe ndugu yangu.
Siku za
karibuni nikiwa kazini kuna mkubwa wangu mmoja wa kazi ambaye ni mgeni kwangu alinishangaza
sana maana aliniita na kuniambia ‘’Peter Kaninunulie sigara 2’’
Moyo wangu
ulilipuka na kukaja hasira ya rohoni kubwa sana, Nikamjibu kwa nguvu kwamba
haiwezekani na MUNGU hapendi ujinga huo, Yule mzee uoga wa ghafla ukampata, akaanza kuongea kama
ana kigugumizi, akawa mpole sana na hakutoa amri tena bali akaniuliza ‘’Samahani
je umeokoka?’ Nikasema ‘’Ndio nimeokoka kwa neema ya BWANA YESU’’ Akasema ‘’Samahani
sana mtumishi, akaondoka na kuelekea
kwingine ndipo nikakumbuka Neno la MUNGU katika 2 Kor 6:17-18 Linasema ‘’Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema BWANA, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.
Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,
‘’.
Kumbe kuna
haja ya kutoka kati yao.
Hatutoki
yaani hatuhami nyumba zetu ambazo tunakaa na wasioamini au walikamatwa na
dhambi mbaya ila tunatoka kwa jinsi ya
kutokushirikiana nao katika uovu wao.
Wewe mama
ambaye mmeo ni mlevi na wewe umeokoka hakikisha unatengwa naye kwa jinsi ya
matendo yake yaani usishiriki uovu wake, Isitokee kwa sababu unaenda sokoni
harafu akakuambia ‘’Hiyo chenji itakayobaki niletee bia 2 za kopo’’ Mkatalie
maana hapo utakuwa umeshiriki uovu wake. NI BORA KUMTII MUNGU NA SIO KUWATII
WANADAMU AMBAO HAWANA MBINGU YA KUKUPELEKA. Na kama una ndoa ya aina hii maombi
kwako itakuwa ni silaha namba moja na kuhakikisha mpaka kati yako na mmeo mlevi
ni mkubwa sana kiasi kwamba hawezi
kukushirikisha uovu wake.
Hiyo ni
mifano miwili tu katika makumi elfu ya mambo kama hayo yanayowapata watu wengi lakini Biblia inatuambia tokeni mkatengwe nao
kwa habari ya matendo yao maovu.
Ni marufuku
kuchangia uovu wa mtu mwovu.
Vijana wengi
wa kiume huwatongozea marafiki zao mabinti wakidhani wako salama na dhambi,
kumbe hata wao wanachukua ujira wa wazinzi.
Unabuniwa uongo
mahali Fulani na wewe unashirikishwa ili
tu umwambie uongo mtu mwingine ukidhani kwamba dhambi yako ni ndogo kumbe
umebeba kapu zima la dhambi hiyo.
Wengi
wanawaficha wezi wakidhani kwamba wao wako salama kumbe hata wao wametabeba
dhambi ya wezi vilele na kwa kiwango kile kile cha mwizi halisi.
Tunatakiwa
tume makini sana, tunatakiwa tukatengwe nao waovu kwa habari ya kuzishiriki
dhambi zao.
Nikiwa
Zanzibar miaka michache iliyopita, yaani miezi kadhaa baada ya kuokoka,
marafiki zangu wengi kama sio wote kabisa walikuwa na tabia ya kuongea matusi,
lakini namshukuru MUNGU kwa msimamo wangu wa kiroho ulipelekea kila nikifika tu
wanaacha mada ya matusi na kuanza kuongea yasiyo matusi, unashangaa ukitokea tu kazini unasikia ‘’mtu
wa MUNGU amefika hivyo tuache matusi’’, mwanzoni niliona kama wananikebehi
lakini nilikuja kugundua kwamba walikuwa wananisaidia sana ili siku zote niwe
mbali na baraza la wenye mizaha. Na pia msimamo wangu ulisaidia kuwafanya
wasiongee uovu mbele yangu. Kumbe kuwa na msimamo ni jambo jema sana.
Hata wewe
ndugu yangu tambua kwamba msimamo wako kiroho utasababisha mtu yeyote asikushirikishe uovu wake.
Dhihirisha imani yako hadharani, na kila mtu ajue kwamba umeokoka, linda imani
yako ya uzima, wala sio kila siku ukienda kanisani unaficha Biblia hadi ukifika
kanisani ndio unaitoa hiyo ni imani haba zaidi. Onyesha msimamo wako na onyesha
kwamba YESU uliyempokea hafananishwi na chochote na hakuna wa kumwondoa ndani
yako.
Waefeso
5:7-12 (Basi msishirikiane nao.
Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, bali sasa mmekuwa nuru katika BWANA; enendeni kama watoto wa nuru,
kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli;
mkihakiki ni nini impendezayo BWANA. Wala msishirikiane na matendo yasiyozaa ya giza, bali myakemee;
kwa kuwa yanayotendeka kwao kwa siri, ni aibu hata kuyanena.
)
-Msishirikiane
nao katika uovu.
-Mlikuwa hivyo
zamani lakini sasa hivi mko na YESU.
-Enendeni
kama watoto wa MUNGU wanaokataa kila dhambi iwe ya kutenda au kushawishiwa
kutenda.
-Kwa kila
jambo mkihakiki kama mnampendeza MUNGU.
-Msifanye
matendo yasiyofaa yaani matendo ya giza bali myakemee siku zote.
Tusiichezee
neema kuu namna hii maana ‘’Wema wake Mwokozi wetu MUNGU na upendo wake kwa
wanadamu ulipofunuliwa, ALITUOKOA-Tito 3:4.
Hakuna siri
kwa MUNGU.
Mathayo
12:36(Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu.
).
Usikubali
kushiriki uovu wa waovu, Biblia katika Ufunuo 18:1,4 inatuonya kwamba ‘’Baada ya hayo naliona malaika mwingine, akishuka kutoka mbinguni, mwenye mamlaka kuu; na nchi ikaangazwa kwa utukufu wake.
Akalia kwa sauti kuu, akisema,
Umeanguka, umeanguka Babeli ule mkuu; umekuwa maskani ya mashetani, na
ngome ya kila roho mchafu, na ngome ya kila ndege mchafu mwenye
kuchukiza;
kwa kuwa mataifa yote
wamekunywa mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake, na wafalme wa nchi
wamezini naye, na wafanya biashara wa nchi wamepata mali kwa nguvu za
kiburi chake. Kisha nikasikia sauti nyingine
kutoka mbinguni, ikisema, TOKENI KWAKE, ENYI WATU WANGU, MSISHIRIKI DHAMBI YAKE, WALA MSIPOKEE MAPIGO YAKE .
‘’
Wafanye
uzinzi wengine harafu uende moyoni na wewe kwa sababu tu ulitoa chumba chako
ili wafanyie uovu wao, kataa leo kama neno linavyokuonya katika Isaya 52:11 ‘’ Nendeni zenu, nendeni zenu, tokeni huko, msiguse kitu kichafu; tokeni kati yake; iweni safi ninyi mnaochukua vyombo vya BWANA.
‘’.
Toka kati wa
waovu wanaokushawishi uovu, Yeremia 51:45 ‘’Enyi watu wangu; tokeni katikati yake, mkajiokoe nafsi zenu na hasira kali ya BWANA, kila mmoja wenu.
‘’
MUNGU
hadhihakikiwi milele Hivyo ‘’APANDACHO MTU NDICHO ATAKACHOVUA- Wagalatia 6:7.’’
Usipande
uovu kwa watu bali panda mema, panda uzima kwa watoto wako, panda uzima kwa mke
wako, panda uzima kwa mme wako, usimtendeshe dhambi maana dhambi ni mbaya , dhambi
inaua na dhambi inapeleka watu kwenye mateso ya milele.
BWANA MUNGU
anasema hivi katika Kutoka 32:33 ‘’ Mtu ye yote aliyenitenda dhambi ndiye nitakayemfuta katika kitabu changu.
‘’
Kwa sasa naishia hapo,
MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea
BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na
atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu
kwa mafundisho kanisani. ROHO MTAKATIFU aliyenipa ujumbe huu ana
makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani
aliko KRISTO BWANA.
Comments