BWANA YESU
asifiwe ndugu.
Neno la
MUNGU ni chakula cha uzima, Tamani sana kula chakula hiki maana ndani ya
chakula hiki umo uzima.
Leo ninazungumzia kitu cha muhimu sana yaani
UNYENYEKEVU WA MOYO.
Mathayo
11:29 BWANA YESU anasema (Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;
)
Tuna mengi
sana ya kujifunza kwa BWANA YESU na hili
la unyenyekevu wa moyo ni moja kati ya mambo ya kujifunza kwake.
Kama
ukiushika unyenyekevu wa moyo kinachofuata ni Raha.
Kuna raha ya
dunia hii na kuna raha ya milele ambayo tutaipata mbinguni. Waebrania 4:1,3,11
( Basi, ikiwa ikaliko ahadi ya kuingia katika raha yake, na tuogope, mmoja wenu asije akaonekana ameikosa.
Maana sisi tulioamini tunaingia katika raha ile; kama vile alivyosema,
Kama nilivyoapa kwa hasira yangu, Hawataingia rahani mwangu:
Basi, na tufanye bidii kuingia katika raha ile, ili kwamba mtu ye yote asije akaanguka kwa mfano uo huo wa kuasi.
)
Tufanye
bidii ili tuweze kuingia rahani mwake BWANA YESU .
MUNGU
aliahidi tangu zamani kwamba waasi na wasio wanyenyekevu wa moyo, hawataweza
kuingia rahani mwake.
Biblia
inaendelea kusema maneno haya Ufunuo 14:11 ( Na moshi wa maumivu yao hupanda juu
hata milele na milele, wala hawana raha mchana wala usiku, hao
wamsujuduo huyo mnyama na sanamu yake, na kila aipokeaye chapa ya jina
lake.
)
JINSI YA KUIPATA RAHA YA MILELE.
Bila upole
na unyenyekevu hatuwezi kuipata raha hii ya milele. Mathayo 5:5 (Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi.
).
BWANA YESU
asifiwe.
Unajua
kwanini nasisitiza sana unyenyekevu wa moyo?
Ni kwa
sababu kinyume cha upole na unyenyekevu
ni ujeuri na kiburi Zaburi 147:6 (BWANA huwategemeza wenye upole, Huwaangusha chini wenye jeuri.
) na pia andiko hili ni la muhimu sana
katika hili 1 Petro 5:5 ( Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni
unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu MUNGU huwapinga wenye kiburi,
lakini huwapa wanyenyekevu neema.
).
Kinyume cha
unyenyekevu ni kiburi na MUNGU
huwashusha wenye kiburi.
Ndugu yangu
nyenyekea kwa MUNGU ili akuinue.
Kiburi ni
kibaya sana .
Kiburi
kilimwangusha shetani kutoka kwenye uzima wa milele mbinguni na kwenda kwenye
jehanamu ya milele.
Unyenyekevu
ni syllabus nzuri ya maisha.
Shetani ni
chanzo cha kiburi na jeuri na vitu hivi viwili yaani kiburi na jeuri humpata
mtu baada tu ya kuondoka unyenyekevu na upole wa moyo.
Isaya 14:12-15
inazungumzia kilichomwangusha shetani inasema ( Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni,
Ewe nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa, Ewe
uliyewaangusha mataifa!
Nawe ulisema moyoni mwako,
Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu juu kuliko nyota za
MUNGU; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za mwisho za
kaskazini.
Nitapaa kupita vimo vya mawingu, Nitafanana na yeye Aliye juu.
Lakini utashushwa mpaka kuzimu; Mpaka pande za mwisho za shimo.
).
Kiburi na
jeuri ni vitu vibaya sana, vinashusha watu wengi shimoni yaani kuzimu kama vile
shetani na malaika zake walivyoshushwa.
Wengi kwa
kujawa na kiburi na jeuri hawahitaji kujifunza neno la MUNGU, kwa sababu ya
kiburi na jeuri hawamhitaji BWANA YESU mwenye uzima wao wa milele.
Biblia inaendelea kuzungumza kuhusu shetani
Ezekieli 28:13-17 (Ulikuwa ndani ya Adeni, bustani ya MUNGU; kila jiwe la thamani lilikuwa kifuniko
chako, akiki, na yakuti manjano, na almasi, na zabarajadi, na shohamu, na yaspi, na
yakuti samawi, na zumaridi, na baharamani, na dhahabu; kazi ya matari yako na filimbi
zako ilikuwa ndani yako; katika siku ya kuumbwa kwako zilitengenezwa tayari.
Wewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye; nami nalikuweka hata ukawa
juu ya mlima mtakatifu wa MUNGU, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto.
Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu
ulipoonekana ndani yako.
Kwa wingi wa uchuuzi wako watu walikujaza udhalimu ndani yako, nawe umetenda
dhambi; kwa sababu hiyo nimekutoa kwa nguvu katika mlima wa MUNGU, kama kitu kilicho
najisi; nami nimekuangamiza, Ewe kerubi ufunikaye, utoke katika mawe hayo ya moto.
Moyo wako uliinuka kwa sababu ya uzuri wako; umeiharibu hekima yako kwa sababu
ya mwangaza wako; nimekutupa chini, nimekulaza mbele ya wafalme, wapate kukutazama.
)
Ndugu yangu
ukiona umeishiwa unyenyekevu wa moyo na upole kwa MUNGU basi tambua kabisa
ndani yako kumeingia kiburi na jeuri ambavyo ni mapando ya shetani na tambua
kabisa mapando hayo shetani ameyapanda ndani yako ili tu kukushusha shimoni
yaani kuzimu.
Ukiwa na
kiburi hutahitaji kuchukua muda wako kujifunza neno la uzima.
Kiburi na
jeuri vinawafanya wengi kudharau ibada kanisani.
Ufunuo
12:7-9 ( Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;
nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.
Yule joka akatupwa, yule
mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye
ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja
naye.
)
Kiburi
kilimshusha shetani na malaika zake.
MUNGU
huwashusha wenye kiburi.
Nyenyekea
kwa MUNGU wako ili MUNGU akuinue.
Hata kama
wewe umeokoka ukiona unapungukiwa na unyenyekevu wa moyo basi kiburi kimekuvaa.
Kataa kiburi kwa maombi na utafunguliwa.
Biblia
katika Yakobo 4:7 Inasema tumtii MUNGU na tumpinge shetani naye atatukimbia.
Mwenye utii
hawezi kuwa na kiburi.
Mwenye utii
hawezi kuwa na jeuri.
Ndugu mtii
MUNGU siku zote za maisha yako na
nyenyekea chini ya mkono wake wenye nguvu naye atakuinua tu.
Comments