Vyombo vya habari vilielezea tukio hilo kama moja ya matukio makubwa katika karne ya 21 kwa kanisa Anglikana, lililoanza tangu miaka 20 iliyopita na hatimaye kukamilika hivi karibuni.
Shirika la habari la kimataifa la sky News limemkariri Askofu Welby akisema kuwa amefurahishwa sana na matokeo ya kura hizo na kwamba ni mwanzo mzuri wa shughuli kubwa ijayo.
Nayo Televisheni ya kimataifa ya CNN katika moja ya vipindi vyake vilivyoripotiwa juu ya tukio hili ilibainisha kwamba huenda kanisa Anglikana likawa na maaskofu wengi wanawake kuanzia mwishoni mwa mwaka huu.
Source: Strictly Gospel
Comments