Nabii
maarufu ndani na nje ya bara la Afrika TB Joshua wa kanisa la All
nations (Scoan) la nchini Nigeria ametuma chupa 4000 za maji ya upako
pamoja na dola za kimarekani 50,000 nchini Sierra Leon ili kusaidia
kutibu ugonjwa wa ebola ambao umeikamata nchi hiyo.Nabii Joshua amesema kupitia tovuti ya kanisa lake kwamba maji hayo yamesafirishwa kwa ndege maalumu ya kukodi ambayo gharama yake pia ni dola 50,000 na kufanya gharama kamili dola 100,000 (laki moja) kwa msaada alioutoa akishirikiana na wadau wa Emanuel TV ya kanisa lake.
Katika taarifa yake kupitia tovuti hiyo nabii TB Joshua amesema Mungu mwenye nguvu atajidhihirisha uweza wake kupitia maji hayo ya upako ambayo yametolewa kwa watu waliokumbwa na ebola. "Sio maji ndiyo ya ponya ya wagonjwa ila ni Yesu mwenyewe, lazima mtu anayemuombea mwingine na yule anayeombewa wawe na imani. lazima imani iwe hai ili kupata uponyaji kwasababu ndiyo husababisha uponyaji na sio maji ya upako" amekaririwa nabii Joshua.
![]() |

Comments