BREAKING NEWS: KANISA LA AICT LAMPATA ASKOFU WAKE MKUU.


Mkutano mkuu wa Sinodi kuu ya kanisa la African Inland Church Tanzania (AICT) unaofanyika huko jijini Mwanza umemchagua kwa mara nyingine Askofu Silas Kezakubi kuwa askofu mkuu wa kanisa hilo nchini.

Askofu Kezakubi ataendelea na madaraka hayo ya kuliongoza kanisa la AIC Tanzania.

 Pia zoezi la kuchagua maaskofu wa dayosisi za kanisa hilo likingali likiendelea huku wengi wakionyesha hamu ya kujua atakayeshika uaskofu wa jiji la Mwanza.
Tunawatakia uchaguzi mwema wa AICT.
Askofu mkuu wa kanisa la AIC Silas Kezakubi akiwa amevishwa shada kwa kuchaguliwa kwake.
 
Habari hii ni kwa ushirikiano na Gospel kitaa.

Comments