KUMCHA BWANA NI CHANZO CHA MAARIFA


Na AP Hosea Shabban akihubiri, Ufufuo na Uzima Moshi Kilimanjaro.


Mithali 1:7, Mith 8:13, Mith 9:10, Mith 14:26,
Tunahitaji maaarifa katika utendaji wote wa kazi zetu na zaidi sana Kazi ya Bwana. Na maandiko yanatuambia;
Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu

Ni kweli kwamba tunaweza kupata maarifa kwa kuwaangilia watu wengine namna wanavyotenda, kwa kuwaangalia waliotutangulia lakini biblia imetuelezea KUMCHA BWANA NI CHANZO CHA MAARIFA.

Tukiisha kujua kumcha Bwana ndio chanzo cha maarifa sasa tunamchaje Bwana?
Jibu ni Tunamcha Bwana Kwa kuchukia uovu.

Tunapomcha Bwana, tunapewa maarifa ya Kimungu yanayotuwezesha kukabiliana na changamoto au matatizo mbalimbali. Maarifa haya yatatuongoza kunena kwa usahihi, yatatuelekeza namna ya kutoka kwenye vifungo na matatizo tuliyoshikiliwa kwayo. Ili tuweze kuitenda kazi ya Mungu kwa usahihi tunayahitaji maarifa haya.

Maandiko mengine yametueleza wamba, Kumcha Bwana kwaongeza siku za mtu za kuishi, Kumcha Bwana ni tumaini imara, Kumcha Bwana ni chemchemi ya uzima, Ili kuepukana na tanzi za mauti.


Ni maombi yangu kwamba Mungu afanyike chemichemi ya uzima, siku zako za kuishi ziongezeke, akuepushe na tanzi za mauti, Bwana afanyike tumaini imara kwako wakati ukiongeza maarifa mengi kwa kumcha Bwana na chochote kilichotengenezwa kwa kukosa maarifa haya kivunjike, tanzi za magonjwa na kuonewa ziharibike na ufanikiwe kwa haya Maarifa ya Kimungu Amen.

Hapa chini ni habari picha katika ibada ya juzi ambapo ujumbe huo wa KUMCHA BWANA NI CHANZO CHA MAARIFA ulifundishwa.




 

Comments