Mageuzi na ujio mpya wa Steve Wamara

Mwimbaji nguli wa muziki wa Injili hapa Tanzania,aliyefahamika kwa wengi kama Steven Mwikwabe, ameamua kufumua michakato yote na malengo yote ya ndoto ya  kizamani na kuja na mtazamo mpya.
Uamuzi huu ameufanya baada ya kuwa ametoa albamu tatu tangu mwaka 2007 hadi mwaka 2013.Albamu ya kwanza ilikuwa Roho kaa ndani yangu,ya pili ilikuwa Rafiki wa kweli ambayo ilimtambulisha sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi na kumfanya kuingia katika "AMERICAN SONGWRITTING COMPETITION" mwaka 2012.
Kupitia changamoto hii wimbo wake wa Rafiki wa kweli aliouweka katika kinyang'anyiro hicho,alijikuta akijifunza vitu kutoka kwa watu ambao walikuwa ni wapinzani wake.
Ndipo alipoamua kufanya mabadiliko ya muziki wake.Japo alitoa toleo jingine ambalo halikuwa na mabadiliko makubwa,ambalo ni "WEWE WAJUA".Baada ya kusikiliza kazi hii ya tatu,aliamua kubadilisha mazingira ili kupata mwelekeo mpya wa kimziki,utokanao na asili yake.
Sasa,kutokana na historia ya hapo nyuma na kuona kwa mtazamo jinsi nyimbo za Tanzania zinavyochukuliwa nje ya nchi,akagundua panahitajika ubunifu mpya.Baada ya kutulia na kumuomba Mungu kwa muda mrefu,ameweza kuchukua maamuzi magumu ya kuanza moja na miundo mipya kihuduma,kimasoko,kimahadhi na maudhui yenye taswira mpya.
Ni gharama kubwa kuchukua maamuzi kama haya kisaikolojia,lakini Mungu aliepanda mbegu ya uimbaji ndani yake hakuwahi kubadilisha majina ya waliotangulia ikawa shida,hivyo hata kwake anaona ni uzao mpya utakaoleta mapya katika jamii inayomjua Mungu na isiyomjua.
Kwa sasa ni wakati wa kuendelea kutengeneza na kuvumbua kilichojificha ili kiweze kuwa wazi kwa walio wengi,zoezi hili ni zoezi gumu ambalo hutumia muda mwingi kufikiria namna itakavyowezekana kwa nguvu za Mungu kupenya ndani ya wote wasiokijua kile kijacho.
Anawashukuru wote waliokuwa naye bega kwa bega katika huduma na tarajia ujio mpya wenye mlengo mpya,nia mpya mpya,mahadhi mapya na huduma yenye mtazamo mpya unaoendana na mabadiliko ya kiteknolojia.

Kumpata Steve Wamara,tumia namba hizi:-
+255 684-107 900
+255 656-999 965
Au
Email:stevewamara@gmail.com

Comments