Waimbaji wakiwa wana mwabudu BWANA kabla ya kuanza ibada. |
Pata machache kuhusu somo hilo.
Katika somo hili la malango ya kuzimu tutapata kujua kazi za MAJINI na MAPEPO.
MAPEPO: Ni jeshi dogo la kuzimu linaliofanya uharibifu,lakini linaaribu na kuangamiza mambo mengi sana.
Mtu mwenye mapepo mara nyingi hauwezi kumuona kwa macho ya kawahida ni mpaka uwe katika macho ya Rohoni ndo unaweza kumgundua.
Zifuatazo ni dalili za mtu mwenye mapepo:
- Macho yenye kiburi,
- Ulimi wa uongo,
- majigambo mengi na kujifanya mjuaji wa kila kitu.
- Miguu yake ni mwepesi kukimbilia maovu.
JESHI LA KUZIMU
Mapepo ni ajent wadogo sana wa kishetani wanaofanya kazi kwa kiele ele kuliko majini.
Efeso 6:11-12.
Vaeni silaha zote za Mungu,mpate kuweza kuzipinga hila za shetani.Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali juu ya falme na mamlaka,juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya mapepo wabaya katika ulimwengu wa roho.
Mapepo wabaya katika ulimwengu wa roho ni hawa ambao wanakuwa ajent wadogo sana kwa ajili ya uharibifu.
MAJINI:
Ni shetani aliyepewa ruhusa kutoka kwa mmiliki wake ili atawale kwa jambo fulani
Yanamilikiwa na yanafugwa,yana nguvu kuliko mizimu, yana uwezo mkubwa wa kuangusha ata ndege ,meli magari kwa kutaka damu za watu.
Mapepo yenyewe hayatumii damu,bali yenyewe unyonga na kutesa tuu,na usababisha maradhi makubwa makubwa kama KISUKARI, H.I.V, KANSA, UVIMBE TUMBONI,BP nk.
MUNGU akubariki na zifuatazo ni Habari picha katika ibada hiyo.
Waimbaji wakiwa wana mwabudu BWANA kabla ya kuanza ibada.
Ibada hiyo ilifunikwa na nguvu za BWANA
Kulia ni mtumishi wa Mungu ELIUDI ambaye Mungu anamtumia katika kiwango kikubwa mno.
Mwimbaji wa nyimbo za injili akimtukuza MUNGU.
Mtumishi wa MUNGU ELIUDI MJWAUZI akifundisha kuhusu tofauti ya MAJINI na MAPEPO.
Mtumishi wa Mungu ELIUDI MJWAUZI akiwaombea wagonjwa waliokuwa wanasumbuliwa na nguvu za giza.
Mtumishi wa Mungu ELIUDI MJWAUZI akimwombea mama aliyekuwa na nguvu za giza.
Watumishi wa Mungu wakimwombea dada aliyekuwa na ngome za Majini na kumtesa lakini alipata kufunguliwa na kwa sasa yuko huru akimtukuza Mungu.
Barikiwa sana mtu wa Mungu
Ni mimi ndugu yako
Baraka Audax
0717 461006
Injili ya Kristo Zanzibar.
Comments