
BWANA YESU
asifiwe!
Karibu tule
chakula cha uzima.
ROHO
MTAKATIFU amefunua vitu hivi adimu ili tujifunze na kuijua kweli inayoweka
huru.
Mithali 4:23
‘’Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.
‘’
Kwanini kila
mtu analazimika kuulinda moyo kuliko yote ayalindayo?
Ni kwasababu
tabia ya mtu hutoka moyoni na sio rohoni.
SABABU 8
ZINAZOTUFANYA TUULINDE MOYO KULIKO VYOTE TULINDAVYO.
1.
Kwa
sababu kwa moyo mtu huamini hata kupata uzima. Warumi 10:10 ‘’ Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.
‘’
2.
Moyo
unalindwa ili usitoe mabaya. Yeremia 4:14 '' ... jioshe moyo wako usiwe na uovu, upate kuokoka. Mawazo yako mabaya yatakaa ndani yako hata lini?
'' pia Mathayo 15:19 ‘’Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano;
‘’
3.Moyo
ni shamba la kupandwa Neno la MUNGU. Mathayo 13:15 ‘’Maana mioyo ya watu hawa imekuwa mizito, Na kwa masikio yao hawasikii
vema, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakasikia
kwa masikio yao, Wakaelewa kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya.
‘’
4.
Moyo
hutoa Chemichemi za uzima. Mathayo 5:8 ‘’Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona MUNGU.
‘’
5.
Moyoni hukaa KRISTO.Waefeso 3:17 ‘’ KRISTO akae mioyoni mwenu kwa imani mkiwa na shina na msingi katika upendo;
‘’
6.
Moyoni ni mahali pa amani ya MUNGU. Wakolosai
3:15 ‘’ Na amani ya KRISTO iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani.
‘’
7.
Moyoni
ni makao ya ROHO MTAKATIFU. 2 Kor 1:22 ‘’ naye ndiye aliyetutia muhuri akatupa arabuni ya ROHO mioyoni mwetu.
‘’
8.
Moyoni ni mahali pa upendo wa MUNGU . Warumi
5:5 ‘’ na tumaini halitahayarishi; kwa maana pendo la MUNGU limekwisha kumiminwa katika mioyo yetu na ROHO MTAKATIFU tuliyepewa sisi.
‘’
Ni namna
gani nitaulinda moyo wangu?
Kuna njia za
kuulinda moyo wako? Njia hizo ni muhimu sana kwako na zinakuhitaji wewe ili
moyo wako ukae salama daima na moyo wako usikupeleke motoni. Zingatia njia hizo
8 hapo chini.
NJIA 8 ZA KUULINDA MOYO..
1.
Weka
Neno la MUNGU kwa wingi moyoni mwako. Zaburi 119:11 ‘’ Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.
‘’
2.
Epuka
vikundi vibaya. 1 Kor 15:33 ‘’Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.
‘’
3.
Sahau
yaliyopita.Isaya 43:18 ‘’ Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani.
‘’
4.
Usifikiri
mambo ya mwilini.I Kor 3:3 ''kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa
kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena
mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu?
''
5.
Ridhika
na ulichonacho. Mithali 15:16’’Kuwa na mali chache pamoja na kumcha BWANA; Ni bora kuliko mali nyingi pamoja na taabu.
‘’
6.
Jitahidi
sana kuomba mara kwa mara. 1 Thesalonike 5:16 ‘’ ombeni bila kukoma;‘’
7.
Usikubali
mawazo mabaya yakutawale. Zacharia 8:17 ''wala mtu wa kwenu asiwaze mabaya moyoni mwake juu ya jirani yake; wala
msipende kiapo cha uongo; maana hayo yote ndiyo niyachukiayo, asema
BWANA.
''
8.
Mtafute
BWANA YESU kila wakati. Zaburi 34:4 ‘’ Nalimtafuta BWANA akanijibu, Akaniponya na hofu zangu zote.
‘’
Naamini
umekula chakula hiki cha uzima na umeshiba.
Naamini
utatendea kazi hiki ulichojifunza leo.
Unaweza hata
uka-Print ili kuwasaidia na maelfu wengine.
Usiache
ku-share ujumbe huu ili uwe umehubiri pamoja na mimi na watu wengi zaidi
watajua njia za kuwasaidia ili walinde mioyo yao kuliko vyote.
BWANA YESU
anakupenda sana na nakuombea Baraka za BWANA YESU siku zote.
Kwa sasa naishia hapo,
MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea
BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na
atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu
kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana
makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani
aliko KRISTO BWANA.
Comments