WALIOKUFA KWENYE MOJA YA MAJENGO KATIKA KANISA LA TB JOSHUA WAFIKIA 50



A photo taken and released by Nigeria's National Emergency Management Agency (NEMA) on September 12, 2014 shows emergency workers transporting a man after he was pulled out from the rubble of The Synagogue Church of All Nations
Mmoja wa majeruhi waliookolewa kwenye kanisa hilo akiwa hajitambui.
LAGOS – Idadi ya watu waliokufa kwenye ghorofa moja ambalo lilikuwa kwenye ujuenzi kwa ajili ya kulala wageni la makao makuu ya Kanisa la SCOAN (Synagogue Church of All Nations) la Nabii TB Joshua wamefikia 50.
Jengo hilo la ghorofa tano ambalo lipo makao makuu ya kanisa ni nyumba ya kulala wageni na  liliporomoka Jumamosi  wakati ujenzi ukiendelea.
Hadi kufikia jana Jumapili jumla ya watu 41 walikuwa wameripotiwa kufa, lakini maiti nyingine tisa zimeongezeka leo hii.
Uokoaji bado unaendelea na watu wengine 124 walikuwa wameokolewa wakiwa hai hadi kufikia jana Jumapili.
Jengo hilo liko katika eneo la Ikotun magharibi mwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Lagos.

Comments