APONA UKIMWI BAADA YA MAOMBEZI.

Mtume Peter Rashid akifafanua jambo baada ya Beatrice kumaliza kushuhudia muujiza wa kupona ukimwi..
Ibada ya jumapili iliyopita katika huduma ya Glory to God Miracle Center(House of Prayer For All Nations)  Mbezi mwisho  jijini Dar es Salaam, ambayo ipo chini ya Mtume Peter Rashid Abubakar, ilishuhudia shuhuda mbalimbali ambazo watu wa MUNGU walishuhudia kile ambacho MUNGU amewatendea kupitia maombezi yanayofanyika kanisani hapo.

Nakuletea shududa 2 ambazo wahusika walishuhudia kanisani hapo.

Apona Ukimwi baada ya kuombewa na Mtume Peter Rashid.


Mama mmoja ambaye alijitambulisha kwa jina la Beatrice John alishuhudia matendo makuu ya MUNGU kupitia maombezi ya Mtume Peter Rashid. Beatrice alisema ''Namshukuru sana MUNGU kwa kuniponya ukimwi kupitia maombezi ya Mtumishi wake Peter Rashid, Niliteseka muda mrefu na hakika nilipoteza tumaini lakini MUNGU alinihurumia na sana nimepona kabisa. Hakika MUNGU anajibu maombi na hakika amejibu.''
Beatrice John akishuhudia kanisani baada ya kupona ukimwi kupitia maombezi ya Mtume Peter Abubakar.

Baada ya maombezi, mdogo wake asomesha bure na wafadhili.

Josephine Francis  akishuhudia na pembeni ni Mtume Peter Rashid wakati wa ibada.

Mama mmjoa kwa jina Josephine Francis  alimshukuru MUNGU kwa matendo yake makuu maana aliteseka kwa muda mrefu sana kuhusu jinsi ya kumsaidia mdogo wake ambaye ambaye anasoma chuo, alitafuta wafadhili lakini hakuwapata,  akaamua kwenda kwenye maombezi kanisani hapo. Baada ya kuombewa na kutabiriwa ushindi kupitia jina la YESU KRISTO, wafadhili walikuja wengi na hakika kila kitu kiko sawa, mdogo wake anasoma na hakika MUNGU ni mwema.

Comments