BUNDA KWA YESU:watu wengi wafunguliwa na kupokea uponyaji

Ulikuwa ni mkutano mkubwa wa Injili uliodumu kwa wiki moja uliobeba jina la BUNDA KWA YESU,ambapo wakazi wa mji wa Bunda na maeneo ya jirani walipata nafasi ya kupokea miujiza mbalimbali..Watumishi wa Mungu kutoka nchini Kenya Pastor Thomas Odari na Pastor Barnabas Ngare waliongoza mkutano huo...
Kama hiyo haitoshi,mwimbaji wa nyimbo za Injili kutoka ndani ya jiji la Mwanza,anayetamba na Albam yake ya KUNA NGUVU,Betty Lucas aliwabariki kwa nyimbo zake nzuri zenye mafundisho mengi..
Akiongea na mtandao huu,mkazi mmoja wa Bunda ambaye alihakikisha hakosi semina hiyo adhimu Bwana Nyang'ari alisema"Muda mrefu nimekuwa nikitamani kumuona Betty Lucas,namshukuru Mungu kwa kuwezesha ndoto yangu kutimia." 
Aliendelea kusema kuwa katika waimbaji wanaomvutia hapa Tanzania Betty Lucas ni namba moja kwake.
"Napenda sana nyimbo zake,zinanitia moyo hasa ule unaoitwa kuna nguvu katika maombi,naupenda sana."
Hizi ni baadhi ya picha kutoka kwenye mkutano huo...



Picha zote kwa hisani ya Mwimbaji wa nyimbo za injili  BETTY LUCAS

Comments