Masanja anasema pamoja na siku hizi makanisa kuwa mengi kama vile vibanda vya mitandao ya simu kwa ajili ya kutolea fedha lakini mwito bado haulidhishi, hivyo anaanzisha hudumya
inayoitwa ‘Street Gospel Ministry’.
“Ninapowaambia watu nimeokoka, wanaziangalia nywele zangu au viatu vyangu, lakini wamesahau Samson alikuwa vipi? Sasa nakuja na Street Gospel Ministry nitahubiri mtaa kwa mtaa iwe kwa bajaji au bodaboda,” alisema Masanja.
Msanii huyo anadai kuwa atawafuata kondoo popote pale walipo ili kuwachunga na mahubiri yake atayarekodi kisha kuyatengenezea video kwa ajili ya kuwapatia wale wanaotingwa na mambo ya kidunia ili wapate kumujua Mungu.
“Siku hizi makanisa ni mengi kama vibanda vya M-Pesa na Tigo Pesa au Airtel Money lakini watu wamekuwa wagumu kumwabudu Mungu sasa nawaletea huduma
Source:Mwanaspot
Comments