Na Mchungaji Yoshida kutoka Japani akihubiri katika madhabahu ya kanisa la Ufufuo na uzima , kawe. |
Tunapomsifu Mungu, Mungu anatenda kazi, kupitia maombi Mungu
atatenda kazi pia. Sisi wakristo tunatakiwa tuamini Mungu anatenda kazi sehemu
yeyote bila kujali mazingira tuliyo nayo. Kwake Mungu hakuna kitu kisichowezekana
na tunatakiwa kumwangalia Mungu aliye juu Mbinguni.
Mchungaji kiongozi Josephat Gwajima na mchungaji Yoshida kutoka Japani |
Sisi tunamwamini Mungu ambaye anatenda
mambo yote, uraia wetu ni Mbinguni na ni lazima twende mbinguni. Kupitia maombi
Mungu anatusikia, tunapata amani, tunakuwa pamoja na Mungu na tunatenda mapenzi
yake. Kila wakati unapomuomba Mungu mlango unafunguliwa. Unaweza kupokea baraka
nyingi ukisikia sauti ya Mungu na kuitii. Tunatakiwa tuitii sauti ya Mungu. kwa
maana sauti ya Mungu inasikika. Mungu wetu ni Mungu wa uponyaji, tukiwa na imani Mungu anatenda
kazi.
Kwenye maisha yetu kuna matatizo mbalimbali na ili
kuyakabili tunatakiwa tuombe na kwa uwezo wa Roho mtakatifu Mungu anatusaidia
kupitia Roho mtakatifu kwa neno lake. Mungu anatenda kazi kwa mbegu ya neno lake tunalo panda kwenye
Roho zetu.
Mathayo17:26
26 Naye aliposema,
Kwa wageni, Yesu alimwambia, Basi, kama ni hivyo, wana ni mahuru.
Tukitoa sadaka kwa moyo wote Mungu anakusaidia kulingana na
haja ya moyo wako. Tukiomba kwa nguvu zetu zote Mungu anatenda kazi kwa maana baraka
za Mungu hazina mipaka. Ni muhimu sana kuvunja mapenzi yetu binafsi na kufuata
mapenzi ya Mungu. Kuna watu wengi wamefanikiwa kwa kuyafanya mapenzi ya Mungu.
Mungu wetu ni Mungu wa ahadi,miujiza, Mungu anayetimiza ahadi zake ni Mungu wa
Rohoni. Kuna ahadi Ishirini na saba(27) ambazo Mungu ametuahidi na kati ya hizo
ahadi kila kitu tunachokihitaji kimo ndani ya hizo ahadi zake.
Kwenye kitabu cha mwanzo Mungu anasema iwe nuru na ikawa,
maana yake Mungu anatupa mahitaji yetu kupitia neno laketunatakiwa kila wakati
tuwe tunamwomba Mungu kwa kumaanisha kwa Roho na kweli. kwenye kitabu cha Yoeli
Mungu amesema wakati unakujaatamimina Roho yake juu yetu na huo wakati ndio huu.
Yoeli 2: 28.
Ufufuo na Uzima,Tanganyika parkers Kawe |
28 Hata itakuwa,
baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana
wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu
wataona maono;
Comments