
BWANA YESU
asifiwe ndugu yangu.
Karibu
tujifunze habari za uzima, habari za wokovu mkuu.
Wokovu ni
maana yake ni kuishi maisha ya ushindi dhidi ya dhambi.
Wokovu ni
kukombolewa kutoka kwenye hali mbaya na kuingia kwenye hali nzuri. BWANA
anasema katika Isaya 51:6-7 ‘’ Inueni macho yenu mbinguni, mkaitazame nchi
chini; maana mbingu zitatoweka kama moshi, na nchi itachakaa kama vazi, nao
wakaao ndani yake watakufa kadhalika; bali WOKOVU wangu utakuwa wa milele, na
haki yangu haitatanguka. Nisikilizeni, ninyi mjuao haki, watu ambao mioyoni
mwenu mna sheria yangu; msiogope matukano ya watu, wala msifadhaike kwa sababu
ya dhihaka zao. Maana nondo itawala kama vazi, na funza atawala kama sufu; bali
haki yangu itakuwa ya milele, na WOKOVU wangu hata vizazi vyote. ‘’
Wokovu ni
ukombozi.
Wokovu ni
muhimu sana kwa kila mwanadamu.
Wasio na
wokovu wataangamia milele lakini waliokombolewa na kukubali kuishi maisha ya
wokovu watapona na kuingia katika raha ya milele.
Watakatifu
wote siku ya mwisho watakubali kwamba wokovu una MUNGU kupitia YESU KRISTO
pekee Ufunuo 7: 9-10 {Baada ya hayo nikaona, na tazama, mkutano mkubwa sana
ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na
lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele za Mwana-Kondoo,
wamevikwa mavazi meupe, wana matawi ya mitende mikononi mwao; wakilia kwa sauti
kuu wakisema, WOKOVU una MUNGU wetu aketiye katika kiti cha enzi, na
Mwana-Kondoo. }
Wokovu
unapatikana sasa.
Wokovu ni
zaidi ya huduma yako.
Wokovu ni
zaidi ya kipaji chako.
-Wokovu sio
kuwa Askofu wala mzee wa kanisa .
-Wokovu sio
kuwa mchungaji wala shemasi.
-Wokovu sio
kuwa umesoma sana Biblia.
-Wokovu sio
kwenda kusali tu.
-Wokovu sio
kuwa tajiri.
-Wokovu ni
kumpokea BWANA YESU.
-Wokovu ni
kuliishi neno la MUNGU.
-Wokovu ni
kuishi katika neno la MUNGU.
-Wokovu ni
kutenda mema ambapo ni kumshika BWANA YESU.
Wokovu ni
muhimu sana.
Maisha ya
wokovu ni maisha ya mtu aliyeokoka.
Wokovu
haupatikani kwengine ila kwa BWANA YESU. Matendo 4:12 (Wala hakuna wokovu
katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu
walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.)
Ndugu kama
unataka wokovu lazima umpe YESU maisha yako na uliishi neno lake.
Wengine
hudanganywa na kuambiwa kwamba kuna wokovu mwingine kupitia wengine. Ndugu
zangu hakuna wokovu au ukombozi kwingine kokote ila kwa YESU KRISTO.
Kama unataka
uzima wa mielle lazima umhitaji BWANA YESU maana hakuna wokovu kwingine.
Na kama
umeokoka harafu kwa sasa umeanza kuuchoka wokovu basi tambua kwamba, ukianza
kuuchoka wokovu basi hakika umeanza kuuchoka uzima wa milele. Na kama umeanza
kumchoka BWANA YESU basi hakika jehanamu inakuita maana hakuna wokovu kwingine
kokote.
Ndugu yangu
hakikisha BWANA YESU ni Nuru yako na Wokovu wako(Zaburi 27:1-4 ‘’ BWANA ni nuru
yangu na WOKOVU wangu, Nimwogope nani? BWANA ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu
nani? Watenda
mabaya waliponikaribia, Wanile nyama yangu, Watesi wangu na adui zangu,
Walijikwaa wakaanguka. Jeshi lijapojipanga kupigana nami, Moyo
wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea, Hata hapo nitatumaini. Neno Moja nimelitaka kwa BWANA, Nalo
ndilo nitakalolitafuta, Nikae nyumbani mwa BWANA Siku zote za maisha yangu,
Niutazame uzuri wa BWANA, Na kutafakari hekaluni mwake.)
Tena ndugu
yangu hakikisha unaipokea chapeo ya
wokovu ( Waefeso 6:17”T ena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa ROHO ambao ni neno la MUNGU; ‘’
Kwa sasa naishia hapo,
MUNGU akitupa nafasi tutajifunza tena siku nyingine.na kama hujampokea
BWANA YESU muda wa kumpokea ni leo wala sio kesho, amua leo na
atakuandika jina lako katika kitabu cha uzima na utaanza kuukulia wokovu
kwa mafundisho kanisani. MUNGU ana
makusudi kabisa na wewe, hataki upotelee motoni anataka uende uzimani
aliko KRISTO BWANA.
Comments