IBADA YA SIKU YA WAMAMA PAG ZANZIBAR.

Sherehe  wa  wamama wa kanisa la PENTECOSTE ASSEMBLY OD GOD ZANZIBAR (P A G} iliyofanyika   leo jumapili imewagusa  watu  wengi   walio  hudhuria  kanisani  hapo.

Kanisa  la  PENTECOSTE ASSEMBLY OD GOD TANZANIA,Lilijiwekea  utaratibu  mzuri  wa  kuwa  kwa  kila mwaka  kunakuwepo  sherehe  mbali mbali ya  vijana  na  sherehe  ya  wamama, hivyo mnamo  wiki hii ilikuwa  ndo  sherehe  ya  wamama  kwakweli  ilikuwa  ni  sherehe  kubwa  mno  na  nzuri  sana  ambayo  iliwabariki  maelfu  ya  watu  waliofika  kanisani  na  wageni  waliofika  hapo  kanisani.


Mnamo  Juma pili  ya leo  ilikuwa  ni  sherehe  ya  wamama,ambayo  ilianza  toka  asubuhi  mpaka  saa nane mchana,Sherehe  hiyo ilihudhuliwa  na  watu  mbali mbali  kutoka  madhehebu  mbali mbali na tofauti  tofauti.
Hebu  tuangalie  matukio  mbali  mbali  yaliyojilia  hapo  kanisani.

1:Picha hiyo  hapo  juu  inawanesha  baadhi  ya wamama  wachache wakiwa  wana cheza  igizo  lililobeba  ujumbe wa Mwanamke  kumjali mume  wake ilikuruhusu  nguvu  za BWANA zitawale  familia nzima
2:Picha hiyo  hapo  juu  ni moja   ya wamama waliokuwa  wanamsikiliza  muhubiri  aliyekuwa  naigiza  namna  ya  kuwafundisha  kushuhudia  nyumba  kwa  nyumba.
 

3:Picha  inayofuata  hapo  chini ni baada ya  kuwa  wapimepita  mtaani  kushuhudia  watu  walikubali  kuokoka  na  kumpokea  BWANA YESU awe ni  BWANA na  mwokozi  wa maisha  yao,
Pamoja  na wamama  kuandaa  sherehe  kubwa  pia  waliwza  kuandaa  nyimbo  mbali mbali ,Vyakula  pamoja  na  vinywaji  vya  kutosha  kanisa  zima.


4:Picha  hiyo  hapo  chini ni moja  ya kwaya  ya  wamama  wakimtukuza  MUNGU.Wakiimba  wimbo  ulio  kuwa  na  ujumbe  wa  Mwanamke  ndiye  MLEZI  WA FAMILIA.Hivo  inampasa  kuwa  na hekima,Busara, Ufahamu, Upendo  na adabu  kwa mume  wake  na majirani  zake  wote  wanaomzunguka.
5:Aliyejifunga   kanga kwa picha  za   hapo  chini  mbele  ni  mama  Mchungaji  wakiwa wana mwimbia  BWANA nyimbo  za  sifa.Zilizo  jaa  shangwe  nyingi  na  nderemo, vigeregere  na vifijo. Akika  siku  hiyo  ilikuwa  ni  siku  ya  kipekee  sana  na  imeacha  historia  kubwa  mno  kwa  maana  ni  mengi  sana  na mazuri  mno  wamama  waliyoyafanya .Na kuzigusa  mioyo  ya  watu  wengi kwakuwa  mtu  yoyote  yule  akifanya  jambo  zuri  nilazima  atasifiwa  na kusemewa  mazuri.

Wamama  mnastahiri  pongezi  na  hongereni  sana  na MUNGU  wa  mbingunu  awabariki  sana.


Pamoja  na zawadi nyingi na nzuri walizo mpa Mchungaji AMOSI wa  kanisa  hilo hawakusahu  kumpa  pole na  hongera  kwa  kazi  nzito ya kueneza  Injili  visiwani  Zanzibar  kwa kumpa fedha taslimu  laki  mbili kama  sehemu kumshukuru  kwa  kazi  nzuri anayofanya .

Kama  mnavojua  kazi   ya kuhubiri  Injili  ya Kristo  Zanzibar  imekuwa  na  changamoto  nyingi  mno  lakini  changamoto  hizo  haziwazuhii wachungaji  kuendelea  kumuhubiri  KRISTO.
Mchungaji Kiongozi wa PAG Zanzibar Amos Lukanula akifurahi wakati wa kupewa zawadi na wamama.
6:Picha  hiyo  hapo   ni Mchungaji  AMOSI wa Kanisa  hilo  la PENTECOSTE  akiwa  anatabasamu  kwa mambo  makubwa  ya wamama  waliyomfanyia  kwenye  sherehe  yao.
Ninaamini  utakuwa  umebarikiwa sana Injili  ya Kristo  Zanzibar .tutazidi  kukuabarisha  mengi.

Comments