KAMBA ZA SHETANI

Na Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima,Ufufuo na uzima


Luka11:21
kwa kawaida mtu mwenye nguvu ambaye anasilaha zake ukifanikiwa kumfunga unamnyanganya kila kitu chake.
Ufuno wa Yohana20:1-2
Haya maono aliyaona Yohana ambapo shetani atafungwa miaka elfu moja na itakuwa miaka ya amaani ambayo kwenye Biblia inasema nyoka atacheza na mtoto, simba atacheza na kondoo ni kwasababu shetani atakuwa amefungwa.
Luka13:10
Yesu aliingia katika sinagogi ambapo leo ingekuwa ni kanisa na akamkuta mwanamke akamwambia umefunguliwa katika udhahifu wako. Shetani anaweza kufunga uzazi, anaweza kufunga nchi, anaweza kufunga bunge, anaweza kufunga elimu, kufunga akili, anaweza kufunga ndoa, anaweza kufunga uchumi, anaweza kufunga mawazo, anaweza kufunga mwili. Yesu aliingia kanisani na akamfungua mtu aliyekuwa na kifungo chenye muda wa miaka kumi na minane. Kumbe kanisani kama hakuna Yesu hauwezi kufunguliwa. Unaweza kumwona mtu anasema anamatatizo anahasira kila mara lakini hajijui kwamba amefungwa, mwingine amefungwa matatizo mengi ya magonjwa. lakini ipo njia ya kutoroka kutoka kwenye vifungo hivyo. ukizoea magonjwa kila ukijisikia hali fulani unatamani dawa fulani. Ukifungwa huwezi kujua umefungwa lakini Yesu ni njia ya kutoka kwenye vifungo tulivyo navyo.
Zaburi18:5
Zaburi116:3
Kamba hizi ni mashetani au mitego ya mauti. Anaweza kuwa rafiki yako, jirani, Baba, au ndugu yako anaweza kuyaita mashetani na kuyatuma kuja kwako na kufanyika kuwa kamba za utasa na akienda hospitalini anaambiwa mirija imeziba, ni tatizo l;a kiafya lakini limeanzia rohoni na wengine wanawatuma waende wakamfunge mtu fulani uso ili kila atakaye mwona amdharau na kumwona hafai hata kuongea naye, ndio maana kuna wegine hawajioni kama wamependeza na wanachukua muda mwingi kujichubua na kujipaka “makeup” kila mara lakini bado hawaoni wanapendeza lakini anakuwa amefungwa.
shetani anaweza kumfunga mtu akiwa nje au akiwa ndani ya mtu na mapepo ambayo ni kamba za kuzimu. Samsoni alipokamatwa akafungwa kwa vifungo vya shaba mikononi na miguuni akawa hana maana. Washikina wanaweza kunuizia jina lako kwa waganga wa kienyeji na wachawi ili kukufunga na kamba za mauti kwa kupiga ngoma ili kuwatuma mashetani kuja kwako kukufunga, namna nyingine wananuizia kwa udi na ubani ili kuwaita mashetani kukufunga ama nje ya mtu au ndani ya mtu kwa kusababisha magonjwa na mikosi. "KIFUNGO"
Inawezekana umefungwa na uoga, laana, mikosi, kujikataa, dharau, kukata tamaa lakini hujijui kwahiyo unatakiwa uwe na matumaini katika Bwana kwamba vifungo hivyo vitafunguka. Mfano wanawake wenye ndoa wanaweza kufungwa kwamba Mumewe anapokuwa yupo kazini anamtumia sms kwamba anampenda sana na amemmisi lakini anaporudi nyumbani hatoki kwenda kumpokea anakaa chumbani anasoma gazeti la uwazi lakini ni vifungo.
Matendo ya Mitume10:34
Ibilisi anaweza akaonea unaweza kuwa umeonewa lakini wewe hujui.
Yohana11:40-
Lazaro alikuwa amefungwa mikononi na miguuni na Yesu akawaambia mfungueni mwache aendee zake kazi ya kumfufua ilikuwa ni ya Yesu.
Matendo ya mitume12:1-
Hii ni stori ya aliyefungwa na palepale alipofungiwa malaika akaja palepale na wewe palepale ulipofungwa Mungu aje akutoe kwa jina la Yesu.
Kuna aina mbalimbali za vifungo
1. kifungo cha mapepo yanakuja kukufunga
2. 2. Watu wanatengeneza maneno wanakufunga mpaka unakosa kibali kwa unaowategemea, kuna yule mtu unayemtegemea ambaye unaona Bwana atamleta kuja kwako kukupigisha hatua lakini ananenenwa maneno na kuacha kukupigisha hatua mahali fulani.
kwenye ulimwengu wa rohoni kuna kamba kabisa zimekufunga bila wewe kujua UKIRI"katika jina la Yesu ninakata kamba zilizofungwa na ndugu wa karibu na marafiki zangu kwa jina la Yesu kristo"
Samsoni aliyachoma mashamba ya wafilisti, na wafilisti na wakawaambia wale ndugu zake wamfunge lasivyo watauwawa na Biblia inasema adui wa mtu ni wa nyumbani mwake anaweza kuwa mjomba, shemeji, kaka au binamu au mtu yeyote yule wa karibu. Kwenye kila familia lazima awepo mtu anayejihusisha na uchawi ndiye anayeweza kukufung. Hawa ndugu wa Samsoni wakamkamata na kumfunga wakaenda kumkabidhi kwa wafilisti, na walipoona amefungwa wakaanza kusheherekea, mara nyingi wale wanaokufunga wanapoona umefungwa kabisa wanaanza kusheherekea na kufurahia na Biblia inasema waziwazi walipokuwa wanasheherekea Roho wa Bwana alimshukia Samsoni na akaanza kumshika mmojammoja na kuanza kuwashughulikia na wewe leo unatakiwa uanze kukata kamba zilizokufunga kwa jina la Yesu "kwa mamlaka ya jina la Yesu kristo mwana wa Mungu aliye hai ninazikata kamba na vifungo vya balaa, mikosi, laana , umasikini, magonjwa kwa jina la Yesu".
Kuna wakati mwingine unaweza ukawa umefungwa kichwa usiende kumbe kuna mahala wameshilikilia ili usifanikiwe kuyaendeleza yale mawazo uliyo nayo. Samsoni alifungwa akatobolewa macho ili asione na akafungwa akawa anasaga ngano na siku moja wafilisti wakaanda sherehe kubwa mbele ya mungu wao ili wamchezee na kusheherekea. 'kifungo cha Samsoni kilikuwa ni kwasababu ya makosa yake' unatakiwa usikae kwenye blanketi la kujilaumu kwasababu ya makosa yako songa mbele na Bwana atakusaidia kutoka kwenye vifungo ulivyo navyo kwa jina la Yesu.
"Wakati mwingine tatizo si tatizo bali ni jinsi unavyowaza kuhusu tatizo unaweza kuleta tatizo. Tatizo ni fursa ya kukusogeza karibu na Mungu. Hakuna tatizo la milele matatizo yote yana mwisho wake."
Samsoni aliomba maombi ya kuwa “Bwana naomba mara hii tu nijilipize kisasi kuhusu adui zangu”. Unaweza ukamwona mtu amekaa lakini vimewekwa vitu 'mashetani' ili kumfanya anuke,asisome,asifanikiwe,apatwe ajali na mikosi bila kufahamu chanzo ni vifungo
UKIRI "Kwa jina la Yesu kifungo chochote kilichowekwa juu yangu kivunjike kuanzia leo kwa jina la Yesu"
Yesu akawaambia nendeni mtamkuta mwanapunda mkamfungue mje naye' kumbe mtu anapofunguliwa ni kwasababu Bwana anakuwa anahaja naye.
Kifo ni roho inayotumwa ndani ya mtu na unapofika muda mtu anakufa mfano inapotokea ajali na roho ya kifo ipo ndani yake anakufa kwasababu alikuwa anatembea na roho ya kifo.
Matendo ya mitume10:12
Tumepewa jina ili lolote tukakaloomba litendeke. Yesu alikuja kuwatafuta walioonewa, kwa kusudi hilo mwana wa Adamu alidhihirishwa ili azivunje kazi za ibilisi. Yesu alikuja kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao.
Waebrania4:12
Yohana14:14
UKIRI
Imeandikwa Ombeni lolote kwa jina langu nami nitalifanya ili Baba atukuzwe ndani ya mwana, Imeandikwa akawaita wale thenashara akawapa uwezo juu ya nyoka na n’ge, imeandikwa nao wakamshinda kwa damu ya mwana kondoo, kwa mamlaka ya jina la Yesu ninakata kamba za mashetani kwenye maisha yangu kwa jina la Yesu kamba za mauti, kamba za utasa, kamba za umasikini, kamba za kuachwa kamba za kuimbiwa, kamba za maradhi, kamba za magonjwa, kamba za mauti, kamba za kushindwa ninazikata kamba hizo kwa mamlaka ya jina la Yesu, kwa damu ya mwana kondoo ninakata kamba za kushindwa kwa mamlaka ya damu ya mwana kondoo, kwa jina la Yesu ninazikata kamba zote kuanzia leo imeandikwa huwageuza malaika wake kuwa upepo na watumishi wake kuwa miali ya moto kwa mamlaka ya jina la Yesu kristo mimi ni rungu la Bwana na silaha za vita vyake ninawatekeza mashetani wote wa vifungo vya mwilini, rohoni, na nafsini ninawateketeza wote kwa upanga wa Roho imeandikwa Neno la Bwana ni kali kuliko upanga uuwao wowote, ule kwa damu ya mwanakondoo ninazikata kamba zote zilizo kwenye maisha yangu kutokea angani, ardhini, na Baharini ninaziteketeza kamba zote zilizofungwaa juu ya afya yangu juu ya roho yangu kwa jina la Yesu, kamba za kifo ninazikata kwa damu ya mwanakondoo, kwa jina la Yesu kristo imeandikwa watashindana lakini hawatashinda ninasimama kinyume na kila kamba zilizogusa maisha yangu kwa moto wa Bwana imeandikwa Mungu ni Moto ulao ninatumia moto wa Mungu kuteketeza kila kamba zilizo shikilia uso wangu, moyo wangu, akili yangu, afya yangu na wale wote waliofanya vita na mimi kwa kunitumia kamba za kishetani ninawafyeka kwa upanga wa Roho kwa mamlaka ya Jina la Yesu kristo, kwa jina la Yesu ninafanya vita na kuwateketeza wachawi wote mliofunga nafsi yangu, roho yangu, na akili yangu kwa jina la Yesu kristo enyi mashetani na majini mliotumwa kuja kufunga ndoa yangu ninawateketeza kwa damu ya Yesu, mliotumwa kufunga biashara yangu, elimu yangu, safari zangu ninawateketeza leo kwa damu ya Yesu, ninavunja na kuteketeza vifungo vyote vyilivyofunga maendeleo kwenye maisha yangu kwa jinala Yesu. Kwa mamlaka ya jina la Yesu ninavunja mgereza yote niliyofungwa huko na kamba za kishetani ninayavunja kwa jina la Yesu kristo, kwa damu ya mwanakondoo katika jina la Yesu mwana wa Mungu aliye hai AMEN.


Comments