KANUNI ZA KUPOKEA KUTOKA KWA MUNGU:

Na Mchungaji kiongozi Ufufuo na uzima Arusha.


Watu wengi wanajua kuomba lakini kati
yao wengi hawajajua namna ya kupokea.
Kwasababu kuna namna ya kuomba na
namna ya kupokea. Watu wengine
wanajua kuomba lakini hawajui jinsi ya
kupokea haja zao. Haifaidii kitu kujua
kuomba na huku ukiwa hujui jinsi ya
kupokea. Kuna mambo kadhaa ambayo
unatakiwa uyatilie maanani unapokuwa
unaomba kama ifuatavyo:-


1. Tengeneza uhusiano wako na
Mungu:-


Maandiko yanasema “haja zenu na
zijulikane mbele za Mungu” pamoja na
kuwa Mungu anajua haja zetu lakini bado
anahitaji sisi tumuombe. Hii ni sawa na
kuomba kwa jirani wakati baba yako
mzazi yupo; utajisikiaje mtoto wako
anapokuwa na shida alafu akuombi
wewe baba yake, alafu yeye
anajitengenezea sanamu na kuiomba.
Utakavyojisikia ni sawa kabisa na Mungu
anavyojisikia kwetu ndio maana Mungu
anasema kuwa anaona wivu (kutoka
20:4) . Mungu anataka tumuombeYeye
ili kujenga uhusiano na yeye. Ukiomba
au kuiabudu sanamu unamfanya Mungu
awe na wivu.


2. Unaongea nini ukiwa katika
maombi yako:-


Maombi unayoongea kwenye maombi ni
ya muhimu sana kwenye kupokea haja
zako kutoka kwa BWANA. Ttuangalie
kwa habari ya Hana; 1Samweli1:1-24; Elikana
alikuwa na wake wawili
Penina na Hana, kama lilivyojina lake
Hana hakuwa na watoto kwasababu
tumbo lake lilikuwa limefungwa. Hana
hapo kwanza alikuwa anaenda na
malalamiko na kulia. Watu wengi
hupeleka malalamiko kwa BWANA,
badala ya kupeleka hoja kwa Mungu.
Hata siku moja Mungu atendi jambo bila
kusudi, na ndio maana tumbo la Hana
lilikuwa limefungwa kwa muda wote ule.
Emu tuangalie mambo kadhaa
yaliyokuwa yakimzuia Hana.
>Sababu ya kuomba:-
1Samweli 1:1-24 Hana alikuwa
anamuomba Mungu ampe mtoto ili
amkumeshe penina, na ndio sababu
inayowafanya wengi washindwe kupokea
kwa BWANA kwasababu hawana sababu
ya Kibiblia inayowafanya Mungu awape
mahitaji yao. Mfano mtu anamwomba
Mungu mke ili amfulie nguo au
amechoka kuishi mwenyewe. Hiyo si
sababu; Mungu anahitaji hoja yenye
nguvu ili upokee mwambie jukumu lako
la kutimiza kwenye maisha yako na
nafasi ya mke katika kumtumikia Mungu;
hapo lazima akutendee.
>Peleka haja ya moyo wako:-
Mungu haitaji hali yako ikoje sasa bali
anahitaji kujua unataka nini. Picha ya
tatizo lako unatakiwa uwe nayo wewe
lakini mbele za Mungu unatakiwa
upeleka haja ya moyo wako na si
malalamiko. Kwa wakati ule Hana
alikuwa anapeleka hali yake ilivyo na
penina na si uhitaji wake kwa BWANA.y
Unakuta mtu anamuomba Mungu gari ili
awaonyeshe wengine, huyo hawezi pata
kwasababu si sawa na mapenzi ya
Mungu.
>Mwangalie Mungu na si jambo
unalohitaji:
Ibarahimu alipompokea Isaka
ilimradhimu Mungu kumjaribu ili ajue
upendo wake upo kwa Isaka au kwa
Mungu. Watu wengi wanamuomba
Mungu jambo lakini wakilipokea ndilo
linalofanyika mzigo mkubwa wa
kutokumtumikia Mungu, mfano mtu
anaomba mume akipokea tu; baada ya
siku chache haji kanisani anasema eti
anamuhudumia mumewe. Kwasababu
hii hata Hana akupata mtoto mpaka
alipobadilisha maombi na kumuomba
Mungu mtoto, kwa kumuahidi BWANA
kumtoa mtoto huyo awe mtumishi
wake.


3. Imani na Bidii:


Watu wengi wanafikiri bidii ni kutumia
nguvu tu katika maombi, bali bidii ni ule
mzigo; ni muhimu unapokuwa unaomba
uwe na mzigo wa kuombea. Ili uzae
matunda katika maombi ni lazima uwe
sawa na mama mjauzito aliye katika
kuzaa; lazima uwe na uchungu yaani
umaanishe. Vivyohivyo kupokea kutoka
kwa BWANA Unatakiwa umaanishe na
lazima uamini pia kuwa ni wakati wako
wa kupokea kutoka kwa BWANA.
Unapoomba unatakiwa moyo na akili
yako iwe kwenye kile unachohitaji. Kuna
watu wanabidili maombi kila kukicha kwa
kuhisi kuwa Mungu awasikii lakini bidii ni
kubaki kwenye jambo hilo hadi uone
amani moyoni kuwa BWANA
ameshatenda na hili jambo ndilo ambalo
Eliya alilifanya alipokuwa anaomba mvua
kunyesha tena. Eliya alikuwa
mwanadamu wa namna moja na sisiy
alikuwa na Bidii katika maombi.


JAMBO LA KUFANYA:


Baada ya kujua mambo haya ni muhimu
kubadili mtazamo wako na jinsi
unavyoomba. Mungu anajibu maombi
kama ukiomba sawasawa na neno lake.
Kwanza uwe na picha ya kile ambacho
unataka BWANA akutendee, uombe na
imani na bidii. Hapo lazima Mungu
akutendee kwasababu hakuna baba
ambaye mwanaye atamwomba mkate
akampa jiwe au samaki akampa nyoka.
Badili mtazamo wako katika maombi
yako ili uwe mpokeaji wa maombi yako
ni si mwombaji asiyepokea chochote!!!
-FRANK ANDREW-

Ufufuo na Uzima Arusha.
BAHATI BUKUKU AMTEMBELEA MWANAMUZIKI MWENZAKE SARAH MVUNGI HOSPITALINI ALIKOLAZWA (TMJ) Mwimbaji wa nyimbo za Injili Bongo, Sara Mvungi akiwa katika Hospitali ya TMJ, Dar. Sara Mvungi akiwa na Bahati Bukuku alipomtembelea katika hospitali hiyo.

Make Money at : http://bit.ly/best_tips

Comments