KIBARAKA WA MWENYE NGUVU

Na Frank Philip

Kibaraka ni mtu anayefanya kazi kwa kutaka kumpendeza BWANA wake au mtu mwingine MWENYE NGUVU. Kibaraka haishi kwa matakwa yake ila ya MWENYE NGUVU.

Kibaraka anasifa nyingi za kuvutia. Nataja chache: Kibaraka hua na nguvu nyingi bila kuhesabu gharama ya kile afanyacho alimradi bwana wake ameridhika. Mara nyingi kibaraka halalamiki anapotumikishwa, na hata akilalamika bado huendelea kumtumikia bwana wake tu. Kibaraka haangalii muda, mahali wala kuwaza sana juu ya matokeo ya matendo yake japo mara nyingine hapendi afanyacho. Kwa sababu hii ya “ku-take risk” vibaraka hufanikiwa saana katika wayatendayo japo ni kwa ajili ya kumpendeza MWENYE NGUVU na sio Mungu!

Kuna sifa mbaya kadhaa za kibaraka. Nitazitaja chache. Kibaraka hua katika hali ya UHITAJI na KUPUNGUKIWA kila siku. Siku zote ni dhaifu kwa MWENYE NGUVU! Sifa nyingine mbaya zaidi inayomfanya kibaraka azidi kua kibaraka ni ile hali ya ‘kutojua kua yeye ni kibaraka’ na akiambiwa hukasirika na kubisha kwa nguvu!

Katika organizational structure ya Mungu, MUNGU yuko pale juu, punde kidogo akamweka mwanadamu na kisha malaika watakatifu. Kumbuka Shetani na mapepo yote yalikua katika ngazi ya malaika kabla ya kuasi. Hii inamaana Mwanadamu yuko juu ya shetani na mapepeo yote na juu ya malaika pia! Shetani na mapepo yote yatazidi kua CHINI yako daima kama unaishi maisha MATAKATIFU na kumtii Mungu.

Nitatoa mfano. Kila mtu, mvulana au msichana, anakua na nguvu kubwa ya kupambana na ‘uzinzi’ na kuupinga hata kama “hajaokoka”. Asili ya hiyo nguvu sio jina la Yesu, kwa maana hata hajui kuomba na wala sio Mkristo, ila asili ya nguvu hiyo ni ile ngazi ya juu Mungu aliyomweka katika ulimwengu wa roho kuliko mapepo. Siku anajaribiwa na “tamaa zake” na kufungulia ‘uzinzi’, kuna package ya mapepo yanahusika hapo na yanamfanya sasa kua KIBARAKA wa ngono! Anakua dhaifu wa ngono na anaanza sasa kutenda kwa mfano wa KIBARAKA na mapepo ya ngono yakiwa kama MWENYE NGUVU! Ushindi wa mtu huyu dhidi ya ngono sio natural na automatic tena, sasa atatumia jina la Yesu, tena kwa nguvu na kupambana na MWENYE NGUVU kwa maana mwenye nguvu ameshaingia ndani, sharti “umfunge kwanza ndio uweze kuchukua/kutawala vilivyo vyako” la sivyo utabaki kua kibaraka na utatumikishwa kweli hadi mauti. (Warumi 7)

Umewahi kufikiri gharama ambayo KIBARAKA anaweka katika salon, mavazi, viatu, vipodozi, simu na mawasiliano, gym, nk. Kwa lengo tu la kukaa katika “mkao fulani” ili kumpendezesha MWENYE NGUVU wake? Nakwambia kwenda fellowship na bible study ni bure ila KIBARAKA hataenda huko maana ‘anaswagwa’ kama ng’ombe na mwenye nguvu [“asije akasikia Neno akapona/akaokoka”], atapata muda na hela ya kulipa gym, eti ana-keep shape na tumbo lake liwe dogo! Au anajenga kifua na mkono kwa maana wadada wanapenda hiyo! [Sasa biblia inasema “mazoezi ya mwili yafaa, ila utaua wafaa zaidi”] Shida sio mazoezi, vipodozi wala jitihada zingine, shida iko katika chanzo na sababu na makusudi ya kufanya “hivyo vitu” ndio inayopima kwamba ufanyacho ni dhambi au la!, the motive behind! Je! Kuna mwenye NGUVU anakusukuma katika jitihada zako ziwazo zote? Je! Wewe ni kibaraka wa mwenye nguvu katika maeneo mbalimbali? Tafuta UKOMBOZI WA DAMU YA YESU nawe utakua huru..
Warumi 7: 14 “Tunafahamu kwamba sheria ni ya kiroho. Lakini mimi si wa kiroho; mimi nimeuzwa utumwani, ni mtumwa wa dhambi. 15. Sielewi nitendalo: kwa maana lile ninalotaka kulifanya, sifanyi; badala yake, ninafanya lile ambalo nachukia kulifanya. 16 Kwa hiyo kama ninafanya lile nisilopenda kufanya, hii ina maana kwamba nakubali kuwa sheria ni njema. 17 Basi, kwa kweli si mimi hasa nitendaye lile nisilolipenda bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu.18 Kwa maana ninafahamu kwamba hakuna wema wo wote ndani yangu mimi, yaani katika mwili wangu wa asili. Ingawa nina nia ya kutenda lililo jema, lakini ninashindwa kulitenda. 19 Sitendi lile jema nipendalo bali lile ovu nisilopenda, ndilo nitendalo. 20 Basi kama ninafanya lile nisilopenda kufanya, si mimi tena nifanyaye hivyo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu. 21 Kwa hiyo imekuwa kama ni sheria: kila ninapotaka kufanya jambo jema, jambo ovu hujitokeza. 22 Kwa maana ndani yangu ninaifurahia sheria ya Mungu. 23 Lakini ninaona kuna sheria nyin gine mwilini mwangu inayopingana na ile sheria ninayoikubali akilini mwangu. Sheria hii inanifanya kuwa mateka wa sheria ya dhambi ambayo inafanya kazi mwilini mwangu. 24 Ole wangu, mimi mnyonge! Ni nani atakayeniokoa na huu mwili wa kifo? 25 Ninamshukuru Mungu kwa ajili ya Bwana wetu Yesu Kristo! Kwa hiyo basi, mimi kwa moyo wangu, ninaitumikia sheria ya Mungu, lakini kwa mwili wangu wa asili ninaitumikia sheria ya dhambi.”

Frank Philip.
Mtume Victor Kanyari wa huduma ya Salvation Healing Ministries Church iliyokumbwa na mtikisiko.
Mwanasheria mkuu wa Kenya amepiga marufuku na kuongeza sheria kali ya kutoruhusu usajili wa makanisa ama misikiti mipya baada ya kugundulika baadhi ya watumishi hufanya miujiza ya uongo ili kuvuta waumini kwenye nyumba zao za ibada kwa lengo la kujiongezea kipato.

Kwa mujibu wa mwenyekiti wa umoja wa makanisa ya kiinjilisti nchini humo Askofu Mark Kariuki amesema linapokuja suala la imani watu wapo tayari kufa kulinda imani yao nayeye pamoja na wenzake watasimama kidete na kanisa na kuwataka wakristo wote kuwaunga mkono na kusimama pamoja nao katika hilo.

Askofu Kariuki na mkewe.
Siri ya kuwepo miujiza bandia imekuja baada ya kituo maarufu cha runinga nchini humo cha KTN kupitia moja ya habari zake za kipelelezi kupitia kipindi cha 'Inside story investigative' kilichopewa jina la 'Prayer Predators' kimefichua siri ya mchungaji aitwaye Victor Kanyari wa huduma ya 'Salvation Healing Ministry church' ya jijini Nairobi anayerusha matangazo yake kwenye runinga amekuwa akitoa shuhuda na miujiza bandia kuvutia waumini ambao wamekuwa wakimpatia pesa.
Taarifa ya kituo hicho imedai mchungaji Kanyari amekuwa akiwataka watu kutuma michango yao kwa njia ya simu kabla hawajafanyiwa maombi. Askofu Kariuki ameelezea hisia zake kuhusu vizuizi, amesema 'nyanya moja inapooza haimaanishi zote zimeoza, na ikiwa waumini watakwenda kwa mtumishi huyo inamaana makanisa mengine watapata matatizo, alisema askofu Kariuki alipozungumza na Daily Nation la Kenya.
- See more at: http://www.gospelkitaa.co.tz/2014/11/serikali-kenya-yapiga-marufuku-usajili.html#sthash.nDcS2mTF.dpuf
Mtume Victor Kanyari wa huduma ya Salvation Healing Ministries Church iliyokumbwa na mtikisiko.
Mwanasheria mkuu wa Kenya amepiga marufuku na kuongeza sheria kali ya kutoruhusu usajili wa makanisa ama misikiti mipya baada ya kugundulika baadhi ya watumishi hufanya miujiza ya uongo ili kuvuta waumini kwenye nyumba zao za ibada kwa lengo la kujiongezea kipato.

Kwa mujibu wa mwenyekiti wa umoja wa makanisa ya kiinjilisti nchini humo Askofu Mark Kariuki amesema linapokuja suala la imani watu wapo tayari kufa kulinda imani yao nayeye pamoja na wenzake watasimama kidete na kanisa na kuwataka wakristo wote kuwaunga mkono na kusimama pamoja nao katika hilo.

Askofu Kariuki na mkewe.
Siri ya kuwepo miujiza bandia imekuja baada ya kituo maarufu cha runinga nchini humo cha KTN kupitia moja ya habari zake za kipelelezi kupitia kipindi cha 'Inside story investigative' kilichopewa jina la 'Prayer Predators' kimefichua siri ya mchungaji aitwaye Victor Kanyari wa huduma ya 'Salvation Healing Ministry church' ya jijini Nairobi anayerusha matangazo yake kwenye runinga amekuwa akitoa shuhuda na miujiza bandia kuvutia waumini ambao wamekuwa wakimpatia pesa.
Taarifa ya kituo hicho imedai mchungaji Kanyari amekuwa akiwataka watu kutuma michango yao kwa njia ya simu kabla hawajafanyiwa maombi. Askofu Kariuki ameelezea hisia zake kuhusu vizuizi, amesema 'nyanya moja inapooza haimaanishi zote zimeoza, na ikiwa waumini watakwenda kwa mtumishi huyo inamaana makanisa mengine watapata matatizo, alisema askofu Kariuki alipozungumza na Daily Nation la Kenya.
- See more at: http://www.gospelkitaa.co.tz/2014/11/serikali-kenya-yapiga-marufuku-usajili.html#sthash.nDcS2mTF.dpuf
Mtume Victor Kanyari wa huduma ya Salvation Healing Ministries Church iliyokumbwa na mtikisiko.
Mwanasheria mkuu wa Kenya amepiga marufuku na kuongeza sheria kali ya kutoruhusu usajili wa makanisa ama misikiti mipya baada ya kugundulika baadhi ya watumishi hufanya miujiza ya uongo ili kuvuta waumini kwenye nyumba zao za ibada kwa lengo la kujiongezea kipato.

Kwa mujibu wa mwenyekiti wa umoja wa makanisa ya kiinjilisti nchini humo Askofu Mark Kariuki amesema linapokuja suala la imani watu wapo tayari kufa kulinda imani yao nayeye pamoja na wenzake watasimama kidete na kanisa na kuwataka wakristo wote kuwaunga mkono na kusimama pamoja nao katika hilo.

Askofu Kariuki na mkewe.
Siri ya kuwepo miujiza bandia imekuja baada ya kituo maarufu cha runinga nchini humo cha KTN kupitia moja ya habari zake za kipelelezi kupitia kipindi cha 'Inside story investigative' kilichopewa jina la 'Prayer Predators' kimefichua siri ya mchungaji aitwaye Victor Kanyari wa huduma ya 'Salvation Healing Ministry church' ya jijini Nairobi anayerusha matangazo yake kwenye runinga amekuwa akitoa shuhuda na miujiza bandia kuvutia waumini ambao wamekuwa wakimpatia pesa.
Taarifa ya kituo hicho imedai mchungaji Kanyari amekuwa akiwataka watu kutuma michango yao kwa njia ya simu kabla hawajafanyiwa maombi. Askofu Kariuki ameelezea hisia zake kuhusu vizuizi, amesema 'nyanya moja inapooza haimaanishi zote zimeoza, na ikiwa waumini watakwenda kwa mtumishi huyo inamaana makanisa mengine watapata matatizo, alisema askofu Kariuki alipozungumza na Daily Nation la Kenya.
- See more at: http://www.gospelkitaa.co.tz/2014/11/serikali-kenya-yapiga-marufuku-usajili.html#sthash.nDcS2mTF.dpuf

Comments